WARUMI
Injili ilifafanuliwa
Waraka wa Warumi ni hazina ya kweli ambayo hupaswa kueleweka kwa watakatifu wa Mungu. Somo hili litakusadiwa kuelewa mafundisho yake ya muhimu.
Paulo alidai kuuandika (1:1). Mtindo wa waraka wa Warumi ni sawa na ule unaopatikana katika Wakorinto 1 na 11 hasahasa kwa Wagalatia. Mtindo wa waraka wa Paulo na mtindo wa Warumi ni wakipekee. Kusoma waraka wa Paulo sawa kama vile unasikia sauti yake. Paulo aliandika kama alivyokuwa anaongea.
Hatua ya maendeleo ya mafundisho ya mkristo ambayo herufi inafunua usawa kwa asili kwenye wakati wa Paulo. Paulo alikuwa katika kiwango cha juu cha huduma katika katikati ya karine ya kwanza kwa wakati ambao maswala ya kawaida yalilisumbua kanisa ndio mambo yaleyale ambayo yalilikumba Warumi.
Paulo alijulikana kama mwandishi wa waraka kwa Warumi mapema mnamo 95 BK. Baadhi ya waandishi walitambuliwa katika mamlaka ya msatari wa Paulo kwa Warumi walikuwa ni:
Paul aliandika hii waraka, lakini yeye hakuanzisha Kanisa la Rumi, walakulitembelea hili Kanisa hadi wakati fulani baada kuandika barua hii. Kanisa la kikristo katika Rumi lilikuwepo tayari kabla ya kuandika waraka kwa Warumi pamoja na kundi ka waamini kukutana majumbani kama vile kwa Priskila na Akula. Kama tutalinganisha War. 1:8, 1:11, na sura ya 16, kwa usalama tunaweza kuhitimisha kwamba kulikuwa na kanisa Rumi kabla ya Paulo hata Petro.
Hapakuwa na historia ilioandikwa ya kupata kanisa huko Roma, lakini tunaweza pia kuhitimisha kwamba Petro hakupata kanisa la kirumi kama inavyosemwa na kanisa la kikatoliki. Paulo hakuwahi kumtamaka Petro kama ilivyothaniwa huko Roma na ngeonekana kimaantiki kama Petro angekuwa kiongozi wa kanisa Paulo angemtaja katika salamu zake katika War 16 badala yake Paulo anaorodhesha watu 28 katika salamu miongoni watu walioorodheshwa wakwanza alikuwa Priska na Akila. Zaidi ya hapo, kitabu cha Matendo kinamweka Petro katika Yerusalemu sio Rumi kulipata kanisa yuko Yerusalemu.
Utawala wa kirumi ulikuwa katika madaraka wakati wa kuandikwa waraka huu na Roma ilikuwa mji mkuu wa utawala huu ulikuwa mji mkuu wa ulimwengu. Imesemekana kuwa barabara zote zilielekezwa Roma—hii ndio ilikuwa sababu kwa warumi kutambulisha na kujenga utaratibu mpya wa barabara kuunganishwa kutoka Mji mkuu wa Roma wenyewe. Rumi ilikuwa mji wa katikati ya ulimwengu na mahali pakimkakati ambapo tokea hapo injili ingeenea.
Kutoka makutano ya watumwa wa kiyahudi kuletwa Rumi na baadaye kuachwa huru, ongezeko (labda wengi kama watu 5) Masinagogi ya kiyahudi yalivunjika. Mwishowe wakristo wa kiyahudi walisafiri kwenda Rumi kama ilivyo na kusababisha ukimwa wa usumbufu uliokuwa nadani ya haya masinagogi ya Kiyahudi. Kwa kadiri Warumi walivyo tishwa na idadiya wayahudi ndani ya mji na makelekele yao kuongeza, hatua zilichukuliwa ilikuvunja ukuaji wa idadi yao. Hatua za kwanza zilizochukuliwa hazikujimuishwa na kuharimisha kwa dini ya kiyahudi, lakini ilizuia makusanyiko yenye mamlaka.
Mwanahistoria Cassius Dio anatoa taarifa ya tendo lilochukuliwa na Kilaudio dhidi ya Wayahudi wa kirumi:
“Kwa ajili ya wayahudi, yeye ambaye alikuwa tena aliongezeka kwa ukubwa ambayo kwa sababu ya makutano yao igekuwa ngumu pasipo kuinua makelele kuwapinga kutoka mjini, yeye hakuwakufuza, bali aliwaagiza, wakati wakiendeleza mtindo wao maisha, sio kushikilia makutano.”
Kutokea hapo wasimamizi waliamriwa na serikali walikuwa ni kanisa la wamataifa. Ni Kanisa hili ambalo lilipokea barua ya paulo mudafulani takribani 57-58 BK. Badala ya masinagogi ya kati au mahali pa mikutano mikubwa, kanisa hili lilikutana katika makundi madogo kuzunguka mji wa Rumi kama majumbani mwa waamini. Kwa kupitia mahali pa makusanyiko yao walipewa madaraka hasa kwa barua ya Warumi, tunaweza kuona kanisa la kikristo likidumisha mawasiliano na umuhimu wa mwili moja katika Kristo.
Warumi iliandikwa kutoka Korinto mnamo 57-58 BK. Katika War 15:19, Hebu jue kuhusu Paulo kwamba yeye alikuwa amekaribia katika hali ya mwisho katika maisha ya kupanda na kushuka kwenye mwisho wa safari yake tatu umisheni. Alikuwa amekwisha kuhubiri injili, anasema kutokea Yerusalemu hata sehemu za Mbali na anaenda kufanya uamuzi wa ajabu kwamba yeye hakuwa tena na nafasi ya kuendelea kufanya kazi katika hiyo sehemu kubwa mno. Anataka kwenda Span kwakuwa Itali ilikuwa imekwisha hubiriwaa Alihubiri, na kutembelea katika kanisa la Rumi katika safari. Lakini hangeweza kufanya kwa mara moja; Yeye aliazimia kwenda Yerusalemu kwanza. Sababu ya hili ni wazi na lina ushahidi. Kwa muda fulani, (2 Wakrinto angependekeza angalau mwaka moja. Paulo anatanagaza kwamba, yeye amejitoa kwa ajili ya kukusanya mchango kwa ajili ya maskini wa Yerusalemu. Wakati wa kuandikwa kitabu cha Warumi, ule mkusanyiko ni kwa bayana, kama haijakamilika kabisa, Paulo anasubiri furusa ya kupokea sadaka kwenda Yerusalemu. 1 na ya 11 Wakorinto hurejea kwenye mkusanyo kama ilikuwa ikifanyiwa kazi (I Kor. 16:1-4; 2 Kor. 8-9) na War. 15:25-28 inaonekana kwa kile kilicho kamilika. Kwa kuwa katika I Corinthians 16:3-4, Paulo alionyesha mpango wake wa kukamilisha kazi kwa ajili ya mchango wa Wakorinto na kisha kuondoka kutoka katika mji ule wa Yerusalemu ni nitu cha kawaida kudhani kwamba aliwaandikia warumi wakati akiwa Korinto. Wasomi wengi huweka wakati wa utume wake takribani 57-58 BK.
Warumi iliandikwa kulingana na utangulizi wa Paulo kwa wakirsto waliokuwa Rumi kutanguliza safari yake kwao. Mtume Paulo alikuwa na muda mrefu wa kusukusudia kutembelea wakristo wa Rumi kwa muda mfupi alipokamilisha kazi yake na alikuwa na kile alichokusanya kwa ajili ya masikini walioko Yerusalemu (1:13; 15:25, 26, 28). Kazi yake huko mashariki;i lipitiliza; na yeye alikuwa katika safari yake ya kwenda Yerusalamu. Alitaka kujitambulisha kwa wakristo walikuwa Rumi kabla ya kusimama pale aliandika huu waraka pamoja na kusudi la kuiandika kuhusu furusa ya upendeo wake wakwanza. Safari ya Phoebe kwenda Rumi alimpatia Paulo furusa kama hiyo (16:1-2).
Ni matengenezo ya kitheologia kwa maana ya Injli. Ingawa kanisa lilikuwa limeongezwa na wamataifa, Uyuda ulikuwa ni nguvu yaziada iliongezwa. Kulikuwa na wayahudi wengi katika Rumi kwa wakati wa kuandikwa kwa waraka huu kwa warumi hata wakristo wa kiyahudi walikuwa wamefungwa na mapokeo na urithi wa kiyahudi, Wayahudi waliamini kwa sababu walikuwa na sheria za Musa na agano la tohara ambayo walikuwa wamewekeana na Mungu kwa ajili ya uzima wa milele. Wao waliamini na wao walikuwa bora katika wapagani wa mataifa na kwa hiyo wao hawakuwa na haja ya kujinyenyekeza kwa watawala wapagani. Paulo anakanusha mafundisho ya wayahudi ambayo hayakuhusiana na maandiko matakatifu.
Mtume ni mtu ALIYETUMWA KWENDA kama mjumbe au mwakilishi wa mamlaka halisi ya mtumaji; mjumbe au balozi (Mdo. 9:3-9, 15-22, 28). Wito wa kitume wa Paulo haukuwa wa kidunia. Wala hakuwa mgombea kwa wale waliopigiwa kura katika Mdo. 1 bali wito wakitume wa Paulo ni kwenda mbele kama mtume aliyekuja toka kwa Kristo (1:5). Paulo anasisitiza kuwa yeye alikuwa ameitwa kuwa mtume; na wito huu ulikuwa wa kimungu na sio wa kibinadamu.
Paulo alikuwa mhubiri wa injili yeye alikuwa mjumbe aliye tengwa mwenye ujumbe maalumu. Injili ni siri (Marko 4:11; I Tim. 3:9, 16; Kol. 2:2; 4:3; Waef. 1:9) ufunuo wa kimungu (Mdo. 9).
Uwekwaji wakifu kamili umezungumzwa katika maneno haya. Paulo alitengwa kuhubiri ujumbe moja na wa pekee. Paulo hakutangaza kwamba ujumbe huo ungemtukuza yeye wala hakufanya zaidi ya nafasi yake mbele ya macho ya watu. Paulo alitangaza kwamba kusudi lake katika maisha llilikuwa ni Injili ya Mungu, na kwahiyo hili lingepaswa kuwa kusudi letu kama wa hudumu Injili.
Ujumbe wa Paulo ni injili. Injili haikutokana na Paulo injili yote inamhusu Yesu Kristo: Bwana wetu, uzao wa daudi, mwana wa Mungu, aliyefufuka.
Wale waliounganishwa na Yesu wameungwa pamoja naye katika wito wake. Walioitwa ambao Paulo anaandika haimanishi waalikwa, bali humaanisha wale walioalikwa ambao wamekuja tayari.
Haina shaka kwamba waandikiwa wa waraka huu walikuwa ni wakristo Warumi (mst. 7, 15). Andiko linaonyesha kwa kanisa la kirumi lililo athiriwa na wamataifa kama Paulo anavyolielezea kanisa akiliacha kwa ugumu na shaka ambayo anawaaandikia wa mataifa. Katika sura ya kwanza, anazugumza habari ya utume kwa ajili ya utii wa imani kati ya mataifa (1:5). Hurejea kwa waandikiwa kama wamataifa mengine na kutoa kama sababu yake kuwa tayari kuhubiri injili kwao kana kwamba yeye anadaiwa kwa Wagriki na kwa wayunani (1:14), kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia (1:16).
Wakati nafasi na matumaini ya taifa la kiyahudi yako chini ya uangalizi na Paulo anakuja kuwaasa, hii ni kwa waumini wa mataifa ambao anaelezea (1:13; 11:13; 15:15-16).
Familia ya Mungu hujumuisha watakatifu walioitwa kwa neema ya Mungu kutoka duniani kuwa watu wake (1 Kor. 1:2). Watakatifu waliotengwa kwa ajili ya ibada na sifa. Ufunguo mwingine wa kufahamu maana ya neno watakatifu; ni waliotakaswa, watakatifu moja kwa moja wako kinyume cha dhambi. Watakatifu ni wale ambao hurusu utakatifu kuwa uhalisia wa maisha yao. Haki ya kweli ni tukio la mapenzi. Haki ya kweli sikuzote huzalisha tendo la inje na matokeo ya ndani. Kila muundo wa dhambi lazima uwekwe inje ya moyo. Kama mawakili wa maadili lazima akili zetu zisikubaliane na dhambi.
Hii ni salamu ya kawaida kwa Paulo katika nyaraka zake. Jina Yesu Kristo au Bwana au Bwana Yesu Kristo limetajwa mara kumi katika Warumi. Yesu ni jina binafsi kama mwokozi (Mat. 1:21). Kristo ni mpakwa mafuta wa Mungu Bwana anadokeza kusema kuwa yeye ni Bwana wa vyote vya mbinguni na duniani (Mdo. 10:36). Yesu kristo ni bwana wetu wa kila hali!
Mstari ya 8-15 inaelezea hisia binafisi za Paulo kwa ajili ya watakatifu wa Rumi.
Dunia yote ni rejea kwa umiliki wa utawala wa kirumi ambao siku zote hujirelea kama dunia yote. Ilikuwa ni Augustino alitoa amri wakati wa kuzaliwa Kristo ambao dunia yote ingetoa ushuru, ambayo ilikuwa ni rejea ya utawala wa Kirumi.
Imani ya watakatifu wa Rumi katika utawala wote. Hawa wakridto wa kirumi walikuwa ni “wapendwa wa Mungu,” “walioitwa kuwa watakatifu,” wapokeaji wa neema na amani “kutoka kwa Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo.” Ushuhuda wao ulitoka kwamba walikuwa wametengwa kwa ajili ya Mungu na kumwakilishi mfalme wa utukufu. Hazina nzuri ya ushuhuda ni Paulo anasimama juu ya uwanja vita katika maombi ambaye imani yao na ushuhuda wao ungeendelea.
Roma ilikuwa ya kimkakati, lakini Paulo anaongozwa na Roho na sio takwimu. Inawezekana kwamba Paulo alitambua thamani ya kimkakati ya kujenga kanisa katika mji mkuu wa Dola la Kirumi, lakini Paulo alikuwa aina ya mhubiri ambayo ingewekeza sana katika jiji ambalo hakuna mtu aliyewahi kusikia. Alibarikiwa kusikia kwamba kulikuwa na watakatifu kule Roma na alitamani kuwatembelea ili kufanya sehemu yake kuimarisha kanisa huko. Ni mantiki kwamba uamsho katika mji wa Roma ungeathiri Dola yote, lakini ukweli ni, Mungu angechagua mahali popote kuwa mwanzo wa uamsho ambao ungeugeuza ulimwengu (Mdo. 17:6).
Alikuwa anataka na hata alipanga kwenda, lakini alikuwa amezuiliwa. Paulo siku moja angeenda Roma kama mfungwa kusimama mbele ya viongozi wa Warumi na kutangaza Injili ya Yesu Kristo. Kitabu cha Matendo kinatuambia kwamba Paulo alikaa miaka miwili huko Roma. Inaaminika kwamba alikuwa chini ya kukamatwa kwa nyumba wakati huu wa kuwa Roma. Alikatwa kichwa huko Roma mnamo 67 BK.
Paulo alikuwa na hamu kubwa ya kuhubiri Injili huko Roma. Yeye hutumia neno “mdaiwa” akimaanisha mwenyewe kuonyesha kuwa amejitolea kuwahubiria watu wote (mst. 14). Alikuwa na deni kwa mwenye dhambi kumwambia juu ya Kristo. “Wayunani” hutumiwa kurejelea Mataifa wenye busara ambao wameelimishwa kwa tamaduni na falsafa ya Uigiriki. “Wasio Wayunani” hutumiwa kurejelea wale walio nje ya tamaduni ya Uigiriki, ambayo isingeelimishwa. Paulo yuko tayari kuhubiria kila mtu.
Mistr ya 16 na 17 ni mistr ya ufunguo wa waraka huu na vifupusho vingi vya waraka.
Maandiko matakatifu hutangaza kwamba Injili ya Kristo ni kwa kila mtu aminiye. Baadhi ya watu kwa uwongo hufundisha kwamba Mungu huchagua baadhi ya watu tu kwa ajili ya kuwaokoa. Injili sio kwa ajili ya wachache walioteuliwa, bali kwa yeyote atakayekuja kunywa maji ya uzima. Kwa yeyote amwaminiye Yesu atakuwa na uzima wa milele (Yoh. 3:16). Watu wote wanauwezo wa kuamini, bali watu hawachagui kumwamini Yesu na kukubali utoaji wake wa ukombozi kwa njia ya damu yake.
Mtu hawezi kufanya chochote kwa ajili ya kujiokoa. Alizaliwa katika dhambi pamoja na njia zisizo na matumaini za mwanadamu. Mtu hana wema wakutosha kukidhi matakwa ya sheria ya Mungu. Yeye ana hatia na amehukumiwa kwenda jehanamu. Hakuna gharama ambayo mtu anaweza kulipa ilikununua wokovu wake. Wokovu ni kazi ya Mungu iliotolewa kwa neema na kupokelewa kwa njia ya imani katika kumwamini Yesu Kristo. Wengi huchanganywa na urahisi wa injili na hawezi kukubali mwenye dhambi anaweza kufanywa upya na kubadilishwa kwa nguvu za Mungu kadiri anavyoifikisha imani katika mikono ya Yesu iliopigwa misumari.
Mtu hana haki yake mwenyewe (Isa. 64:6). Haki ya Kristo inawekwa katika hesabu ya mwenye dhambi. Hii ndio inayomaanishwa kuwekewa haki. Kuwekewa ni neno la toleo KJV kuweka hesabu ya. MAELEZO YA MFANO: mtu ambaye hana fedha katika akaunti ya benk anahitaji mtu wa kumwanzishia akaunti yake. Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu (Yakobo 2:23). Ibrahimu alikuwa na haki ya Mungu iliowekwa katika hesabu yake (War. 4:3). Mungu humwangalia mwenye kutubu kupitia damu ya Kristo.
Haki hupokelewa kwa imani kwenye wokovu. Kuna tofauti kati ya haki iliowekwa na haki ya kupewa. Kupewa humaanisha kuweka kwenye. Mungu huweka haki yake ndani ya mtu kwenye wokovu. Kuna badiliko la asili ambalo huambatana na kuzaliwa upya (Wafl 3:9).
Maelezo kutoka imani hata imani hurejea kwenye ongezeko la imani; kuonyesho ukuaji kutoka imani ya mwanzo ya wokovu kwenda imani kubwa katika Mungu ambayo huja pamoja na ukuaji wa mkristo. Maandiko hutuambia kwamba kila mtu amegawiwa kipimo cha imani (War. 12:3). Watu wote wana uwezo wa kuamini, lakini bado hawafanyii kazi imani yao kumwamini Yesu Kristo. Mitume waliuliza Bwana tuongezee imani (Luka 17:5). Imani huongezeka kwa kadir inavyo fanyiwa kazi. Kwa ukomavu wa mkristo huja ongezeko la imani. Haki ya mungu hufunuliwa toka imani hata imani kwa njia ya Injili.
Ufunuo wa tabia ya Mungu na asili sio kitu cha kutenga mbali na Injili, bali yamefungana katika Injili kwamba sisi kama wasikiaji tuweze KUISHI. Uzima huu na haki sio vitu vinavyopokelewa kwa mara moja, bali hufunuliwa kwetu toka imani hata imani, kadiri tunavyotii na kufanyia kazi yale tuliyo ya pokea, Mungu hutupa zaidi na mchakato wake endelevu katika haki ni njia ya mwenye HAKI. Ufunguo wa kudumisha uzoevu wetu na Mungu ni mchakato endelevu. Paulo anatangaza katika Waebr 6:1, “tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu.”
Paulo anajenga dhamira ya waraka kwenye msingi wa maandiko. “Kama ilivyo andikwa” iko kwenye rejea ya Habakuki 2:4 kutoka ambako taarifa hii imechukuliwa.
Wenye haki hurejelea kwa wale ambao wamewekwa katika uhusiano sahihi pamoja na Mungu kwa njia ya malipo yaliyotolewa na yesu Kristo. Wale waliokoka ni wenye haki au wamekwisha hesabiwa haki.
Mwenye haki hubakia kwa kulindwa na nguvu za Mungu. Katika ulimwengu huu wa dhambi, mkristo anahitaji kutunza nguvu ya Mungu ilikumlinda kwenye njia nyoofu ambayo humwoongoza kwwenda uzimani. Yesu alisema kwamba hakuna mtu anayeweza kumpokonya kondoo toka kwenye mkono wake (Yoh. 10:28). Hii haimanishi kwamba Mungu ataliondoa mbali chaguo la mtu. Wakristo lazima wachague kumtumikia Mungu, kuishi ni uzoevu wa kila siku (mkristo ataishi) hiyo hudai upokeaji endelevu wa nguvu ya Mungu kwa imani.
Nuru huwakilisha ukweli ambao humwongoza mkristo kwenye safari yake (Mith. 4:18; Zab. 119:105). Na zaidi tunatembea katika njia ambao ukweli zaidi hupokelewa. Mungu hufunua zaidi ukweli kadir tunavyo tii ukweli ambao tayari tulisha upokea. Maisha ya ukamilifu wa urithi wetu kama waamini.
Wagal. 2:20—Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.
Warumi 3:9—…Kwa maana tumekwisha kuwashitaki Wayahudi na Wayunani ya kwamba pia wamekuwa chini ya dhambi;
Mahitaji ya wanadamu wote ni kuhesabiwa haki kwanjia ya Yesu vinginevyo ghadhabu ya Mungu itafunulliwa dhidi ya hatia (1:18). Yesu ni ndio njia pekee ya wokovu na wale wasio chagua kukubali utoaji wa Kristo wamehukumiwa (Yoh. 3:18).
Hitimisho la sura hii linaendelezea watu hawa ambao wanahatia nakusitahili ghadhabu ya Mungu. Hawana udhuru.
Mungu alijidhihirisha mwenyewe kwao (mst. 19). Uumbaji wenyewe unatangaza matendo ya Mungu (mst. 20). Hiyo hata kwa wale wasio pokea sheria au kamwe hawajawahi kuisikia injili wamepewa ufunuo wa Mungu kwa njia ya asili kwa hiyo hawana udhuru. Kwa mara ya kwanza walimjua Mungu lakini hawakumtukuza kama Mungu (mst. 21). Picha za sanamu ni matokeo ya kuukataa ukweli na kutomtukuza Mungu.
Warumi sura ya pili inazungumzzia juu ya myahudi mwenye hatia au hatia ya mtu wa kidini. Myahudi aliyekataa nuru ya Ufunuo. Katika sura hii tunaona wayahudi wakiwalaumu wengine, kama mafarisayo walivyofanya. Vilevile sura hii inazungumzia kuhusu tohara ya moyo, ambayo ni ya muhimu sana.
Hukumu ya Mungu nikulinga na ukweli haina upendeleo, na ni halisi. Mwanadamu anaweza kujisikia kuridhika na kuwa na hakika na mahali pake kwa wakati anapo mhukumu mwingine, na bila shaka yeye yuko yuko bila kinga ya kutosamehewa wakati hukumu ya Mungu itakapokuja.
Haitoshi kuifahamu sheria, lazima KUITIMIZA. Ujinga wa sheria hautawaokoa watu wamataifa. Hii inarejea kwa watu wamataifa ambao hawakuipokea sheria ya Musa. Ingawa wao hawakuwa na sheria ya Musa, watu wote wamekwisha pewa habari kuhusu uumbaji na kuwa na sheria ya Mungu, iliofunuliwa na dhamiri ya mwanadamu, ilioandikwa katika moyo. Paulo ameshaonyesha kwamba watu wote wako chini ya hukumu kwa hiyo kuna hitaji la wokovu.
Wale ambao wamefanya dhambi katika sheria watahukumiwa kwa sheria. Yeye husimama mahali pa faraja kuu na haki yake kwa yeye ANAJUA sheria, lakini HAKUNA HAKI KWA KUIJUA SHERIA. Paulo anajiwakilisha kama mmataifa mwenye hatia kwasababu yeye hakuifanya sheria na sio kwamba yeye hakuwa na sheria, kama wayahudi wafanyavyo, na wayahudi pia hawakusamehewa kwasababu ya hatia yao walionao na sio sheria, na wao pia watahukumiwa kwa kutoifanya sheria. Ushuhda wao ni uovu, hujivuna kwakuijua sheria, lakini kutomheshimu Mungu ni KUVUNJA sheria.
Kuhesabiwa kwasasa inatolea kwa imani katika Kristo Yesu. Kristo ni utimilifu wa sheria. Chini ya agano la neema watu wanaweza kuhesabiwa haki kwa njia ya Yesu Kristo. Dhabihu za sheria zilitazama mbele kwenye ukombozi kwa njia ya damu ya Kristo. Na kuhesabiwa haki ambayo ni kwa njia ya imani. Kwa hiyo leo njia pekee ya mtu kuweza kumtii Mungu ni kukubali malipo ya Yesu Kristo (Gal. 3:24).
Je mstari 12 unamaniisha wamataifa hawawezi kuhesabiwa haki kwasababu yeye hakupewa sheria ambayo yeye anaweza kuitii kama wayahudi wafanyavyo? Hapana, kwakweli sio. Mmataifa kwa asili anaweza kufanya vitu vilivyoko katika torati pasipo kuwa na hiyo sheria kwasababu Mungu anampango na kila mtu, dhamiri vivyo hivyo kadiri watu wanavyoilinda na kuihifadhi inakuwa sheria ndani yao katika maana halisi na ukweli wa kifungu. Sheria hii imeandikwa katika MIOYO yao na dhamiri yao zinashuhudia.
Paulo anakabiliana na udhuru wa mwanadamu, kujibu swali: Jinsi gani Mungu anaweza kuhukumu mataifa ambao hawakuwa na sheria? Mungu atamhukumu mtu kulingana na ukweli ambao aliutoa kwake. Wamataifa wanaotenda dhambi watapotea, lakini sheria ya Musa haitatumika kama kiwango cha hukumu dhidi yao. Watu wote bado walikuwa na sheria ya dhamiri zao na ushuhuda wa uumbaji. Mtenda dhambi yuko chini ya hukumu hata kama bila sheria ya Musa.
Mungu alimuumba mtu akiwa na dhamiri ambayo ni uwezo wa asili wa mema na ubaya. Mungu tu ndio mwenye kiwango cha maadili. Hakuna sheria moja kwa ajili ya wayahudi na nyingine kwa ajili ya wamataifa.
Wayahudi walidai kusamehewa kutoka kwenye hukumu iliojikita kwenye urithi. Wakati Yesu anawalaumu wayahudi, wao walijibu: sisi ni wa uzao wa Ibrahimu; Yesu aliitikia:ikiwa ninyi wa uzao wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu (Yoh. 8:33-39). Wayahudi waliamini wao wangepokea uzima wa milele juu ya stahili ya kuwa myahudi na agano la tohara. Maandiko ya zamani ya kirabi huelezea kwamba mtu aliyetahiriwa hatapotea. Wayahudi walikuwa na mapokeo kwamba Ibrahimu alisimama kwenye malango ya kuzimu kuhakikisha kwamba hakuna mtu aliyetahiriwa ambaye ingia hapo.
Ujuzi wa sheria hauwezi kumuokoa Myahudi. Myahudi anayejivuna katika sheria huamini yeye ni kiongozi kwa kipofu, bali yeye mwenyewe ni kipofu. Kwamba yeye anaijua njia, kwamba hakuna mwingine ajuaye zaidi. Anasimama katika sehemu hii kwa ujasiri mkubwa wa binafsi kwasababu yeye ANAJUA sheria, lakini HAKUNA HAKI KATIKA KUJUA SHERIA. Paulo naongea mojo kwa moja kwa msisitizo kuelekea pointi yake, wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, mbona wewe waiba? Paulo kwa wazi anawakilisha kwamba eti mmataifa anahatia kwasababu hafanyi matakwa ya sheria bali si hivyo kwa kuwa yeye hana sheria, kama wayahudi wafanyavyo, vilevile wayahudi hawasamehewi hatia yao kwasababu wanao sheria na wanaijua, bali hatahivyo wanahukumiwa kwasababu hawatimizi. Ujasiri wao ni ujinga wa moyo kwakuwa wao ni vipofu na wanaongoza kipofu.
Tohara ilikuwa ni ishara ya kuondoa hali dhambi. Mmataifa asiyetahiriwa aliyetii sheria ya Mungu alipata faida zaidi kuliko myahudi aliye tahiriwa asiyetii sheria
Tohara ni ya moyo. Kwa swala la kuhesabiwa haki sio juu ya mtu aliyezali akiwa myahudi au mmataifa, wala aliyetahiriwa au la, au kama anasheria au la bali moyo wake unatohara? Ana ugumu wa moyo na dhambi imeondolewa toka moyoni mwake, Paulo kwa hitimisha anasema myahaudi wa kweli ana imani kwa ndani, ambaye moyo wake umeshabadilishwa, sio yule ambaye kwa inje anafuata sherehe kwa njia ya kimwili. Kila myahudi anahitaji kuongeza kwenye tohara yake ya kimwili, tohara ya moyo kwa njia ya toba na maisha yaliyo badilika.
Kuhesabiwi haki ni kwa imani pasipo matendo ya sheria. Sheria ni: faida kwao wanaoijua (mst. 1-2), kwa uhalisi katika asili yake (mst. 3-8), pasipo kupinda katika mamlaka yake (mst. 9-19), kuna kusudi tofauti (mst. 20-30), hakufaywa kwakkuepuka, bali zaidi huthibitishwa kwa imani yetu, (mst. 31).
Paulo anajitambulisha mwenyewe na shauku yake kutembelea kanisa huko Rumi na kisha kutambulisha somo lake la Injili ya Yesu Kristo. Katika hii Injili, haki ya Mungu imefunuliwa kutoka imani hadi imani na ghadhabu ya Mungu imefuliwa dhidi ya wale wanao kataa Injili.
Paulo anathibisha kwamba ujuzi wa sheria hauwezi kuokoa (sio wasikiaji bali watendaji ndio wanao hesabiwa haki) na kusalia au kujivuna katika kujua sheria ni ujinga. Wote wanahatia chini ya sheria; wale ambao wanasheria watahukumiwa kwa ile sheria na wale wasio kuwa nayo watapotea pasipo sheria.
Paulo anaweka wazi kwamba kuhesabiwa sio kwa wale wanao hifathi herufi ya sheria, bali kwa wale ambao ni wayahudi kwa ndani (2:29). Sheria ya tohara ambao inafaa ni utaratibu wa moyo na roho.
Paulo anaiweka sheria katika taswira yake ilio sahihi. Myahudi wa kidini anatoa sauti ya mgongano katika ujuzi wake wa sheria ya Musa kana kwamba ilikuwa kitu cha kuwahesabia haki mbele za Mungu. Wao walikuwa wamefunika taswira ya kile ambacho sheria hufanya. Yesu hakuitoa wala Paulo hakuitoa sheria kama kitu kisicho faa, bali anakiweka katika nafasi sahihi katika taswira iliotolewa na ufunuo wa msalaba. Katika uyahudi sheria ni mfalme, bali kulingana na Injili kuna haki na kuhesabiwa haki pasipo matendo ya sheria.
Ushawishi katika ukuu wa pili wa sheria ni kile ambacho kililisha upinzani wa wayahudi kwa Kristo. Roho mtakatifu alijuwa wayahudi walikuwa wanashikiliwa katika ukubwa wao na kjaribu kuhalalisha ukataaji wao kwa Injili. Katika War. 3, tunakuna na ukanushi wa udhuru wa wayahudi kwa kuendelea kuonyesha kwamba wako chini ya hukumu na wanamhitaji Yesu.
Neno “sheria” kwa ujumla humaanisha kanuni “maandishi ya maelekezo.” Ingawa ilikuwa imetolewa kwa wayahudi na Mungu kwa kupitia Musa, wote wayahudi na wamataifa walikuwa na sheria ya Mungu katika dhamiri zao (Iwe isiwe wanachagua kuipokea ilikuwa chaguo lao).
Kote katika Warumi, Paulo anaelezea udhaifu wa sheria iliotolea na Musa na bado kwa wakati huo huo anathibitisha thamani yake ya ukweli. Sheria iliotolewa kwa Musa kwakweli ni mapenzi ya Mungu, lakini haikuwa jumla ya maelekezo yake. Kosa la wayahudi lilikuwa kwamba walifanya zile kanuni pamoja na sherehe zake na kuambatanisha mapokeo kwenye jumla ya kusudi la Mungu mbele ya ubinadamu.
Ingawa tunaweza kupata neno lilelile “sheria” limetumika katika mistr 52 katika Warumi, Paulo mda wote hajadili kanuni zilezile au maelekezo.
Musa alikuwa ametumiwa kama mwaaguzi wa Mungu, lakini yeye hakuwa mjumbe pekee na wa mwisho kwa wajumbe wa Mungu. Hatimaye, yeye alikuwa tu sehemu ya alama ya neno la uzima! Sheria katika dhamiri zetu au sheria iliotolewa kupitia Musa zote ni dhana za sheria ya Mungu. Mungu ametoa kanuni zake za milele kwa Musa na Mungu anatamani mapenzi yake, sheria yake, na maandishi yake kuhifadhiwa ndani ya moyo wa kila mtu na kuelewweka katika maisha yao.
War. 3:28—Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Mtu anaweza kuhesabiwa haki mbele za macho ya Mungu pasipo matendo ya sheria ya Musa (mwizi msalabani). Mtu hawezi kamwe kuhesabiwa ikiwa anakinzana na mawazo ya Mungu.

War. 7:22—Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani,
Kuwa na sheria iliopokelewa mara kwanza, je wayahudi wana faida gani? (mst. 1-2)
Kuhesabiwa haki kwa imani ni fundisho la usawa wa watu wote ambao wayahudi walidharau kutokana na msisitizo wao wa kuwa na ukuu kwa mataifa. Wayahudi walitaka kuringia ukuu wao juu ya mataifa. Wayahudi wengi waliendelea kukataa injili na kushikilia ukuu wao na sehemu ya kujitukuza katika Yehova kirahisi kwa sababu msitari wao kwa Ibrahimu. Wayahudi wengi walitishwa na dhana ya mataifa kuwa sawa na wao kwa njia ya imani kwa njia ya Yesu.
“Ndio myahudi anafaida, lakini sio ile unayofikiri!” Uaguzi kihalisi humaanisha usemi na uliotumika hapa unarejea kama maneno ya usemi wa Mungu uliotangazwa kwa njia ya manabii na kuhifadhiwa katika Maandiko matakatifu. Wayahudi walikuwa wamepokea unabii wa masiha na kwa hiyo walikuwa na faida ya kuongeza ufunuo wa masiha ambawo mataifa hawakuwa nao. Faida waliokuwa nao wayahudi ilikuwa ni kitu ambacho kiliwahukumu kwa wengi ambawo waliendelea kumkataa Yesu kama masiha (Yoh. 1:11).
Faida ya kuijua sheria sio kile ambacho hutuhesabia sisi haki, bali ile kusikia kwetu neno la Mungu linalo funua furusa ya kupokea imani kutoka kwa Mungu. Tunaweza kkujua zaidi na kutamani kumpendeza Mungu.
2 Petro 2:21—Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
Swali: Je ni faida kutojua mapenzi ya Mungu?
Jibu: Hapana. Nibaraka kuwa na furusa ya kujua mapenzi ya Mungu. Petro anaelezea ukuu wa kiwango cha hukumu ya watu wanaorudi nyuma wamehukumiwa.
Kuhesabiwa haki ni kwa imani pasipo matendo ya sheria. Sheria ni: faida kwa wale ambao wanaijua (mst. 1-2), ni halisi katika asili yake (mst. 3-8), kutopindika katika, mamlaka yake (mst. 9-19), inakusudi dhahiri (mst. 20-30), haikufanywa kwa ajili ya kuepukwa bali zaidi imethibitishwa katika mioyo yetu (mst. 31).
MFANO: Madireva wawili wa malori walikuwa wanasafiri kwa pamoja kwa kuburuza matrela ya urefu wa 12 na 4 walipofika eneo la alama ya kupita kwenye forodha alama ya 11 na 3. Wakwanza alimuuliza mwenzake, je unafikije? wa pili aliangalia pembeni ilikuona polisi hakuona mtu, ndipo alipendekeza kwamba twende tujaribu.
Tumeshafanya udhahiri kati ya maagizo maalumu yaliyotolewa kwa njia ya Musa yaakijumuishwa na Kusudi la Mungu. Ni kosa kubwa kuifanya sheria ya Musa kuwa ni maagizo ya mwisho ya mapenzi ya Mungu. Ukamilifu wa mapenzi ya Mungu ni mkubwa sana kuliko sheria iliotolewa kwa njia ya Musa.
Iko katika Yesu, tunaona ukamilifu wa mapenzi ya Mungu. Bwana Yesu Kristo ni kiwango cha tarajio la Mungu (Waef. 4:11-16).
Kwa maana makusudi ya somo letu tumefafanua sheria ya Mungu kama:
Kiwango cha Mungu cha tarajio kwa ajili ya uumbaji wake.
Sheria ya Mungu inatawaliwa na asili yake. Kile kilicho ndani ya sheria ya Mungu kwasababu Mungu ndivyo alivyo. Mungu ni halisi na kwa hiyo sheria yake ni halisi–matarajio yake ya tabia ya mwanadamu ni halisi. (Muda mwingi, kujitawala kwa mwanadamu ni kitu chochote bali kiwe halisi.)
2 Samuel 22:31—Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia. (linganisha na Zab. 101)
Je wasio amini hufuta mpango wa Mungu? Angali II Tim. 2:13.
Kizuizi chao kilikuwa hata baadhi yao hawakuamini; hakuna kitu kinacho weza kubatilisha ahadi zetu halisi tumekwisha pewa kwa kupitia Abrahamu. Walikuwa katika tokeo la kusema hakuna haja zaidi kile tulivyo, sisi ni wa uzao wa Abrahamu na hiyo itatufikisha mbinguni.
Mst. 4—Hasha! Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo…
II Tim. 2:13—Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
Hii sio sababu, ya baadhi ya wayahudi ambayo hawakuwa waaminifu na ikahitajika imani katika kumwemini Yesu Kristo. Hii ni kwasababu ya ukamilifu wa mpango wa Mungu ambao muda wote uko katika Kristo.
Uf. 13:8—Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.
Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu (mst. 4).
Zaburi ya Daudi ilinakiliwa kuonyesha kuwa Mungu ni mwenye haki hata ijapokuwa Daudi alikuwa amehukumiwa kwa ajili ya dhambi yake. Kulingana na Zab. 51:4, Mungu ni mwenye haki anapozungumza na kuwa wazi wakati anapohukumu. Hii imetumika hapa kuonyesha kwamba Mungu anahaki ya kuhukumu wayahudi kwasababu wao walimkataa masiha ambaye alikuja kwa njia ya uzao wa Ibrahimu kulingana na ahadi. Hizi ahadi ambazo wao walizidai zingewahalalishia uhakika ulioleta hukumu kwa wayahudi kwasababu ya kumtaa kwao Yesu Kristo.
Sifu - ni kuwakilisha sitahili ya maandishi, kujali, au wema; kuongea kwa kupendelea; kutukuza neno la Kigiriki la Webster. Neno linabeba maana ya kutumia yote (kama tabia yenye kuonekana), au kutambulisha, au kusimama na, au kuja katika uwepo.
Lazima tutegemee kwenye mukitadha kutusaidia kufahamu maana ya swali hili. Hii imetolewa kama maswali mawili katika kifungu na kimerahisishwa kwa ajili ya kujifunza. Swali kwa halisi huuliza:kama kutokuwa haki kwetu kumetukuzwa au kulela usikivu kwenye haki ya Mungu na huruma; je Mungu atakuwa hana haki anapotuhukumu?
Hii bado iko upande wetu kufahamu. Kukumbuka kwamba Mungu anashughulika na vizuizi halisi vya wayahudi. Kizuizi ni sawa na vizuizi vya wengi leo. Tungeuliza kwa njia hii: Ikiwa Mungu ni mwenye haki kwanini anihukumu kwa ajili ya dhambi yangu na kunitupa jehanamu? (Hasahasa tukiwa watoto wa Ibrahimu.)
Jibu ni: kwa hakika sio. Kama kanuni hii imetumika kisha itakkuwaje Mungu kuipitia hukumu juu y a ulimwengu? Ulimwengu hapa unarelewa kama mataifa. Wayahudi walikuwa bado wanajaribu kujitolea udhuru kutoka kwenye hukumu. Ni kitu maalumu kwa Mungu mwenye haki kuhukumu wasio haki wenye dhambi haijalishi ni Wayahudi ama Wamataifa.
Ukweli ni, Mungu anaweza kuuhukumu ulimwengu kwasababu yeye ni mwenye haki.
Baadhi ya watu huharibu ukweli wa huruma ya Mungu na kujivuna kwamba hali yao ya dhambi huishi na kibali cha Mungu kisicho na mashariti, kinaielezea huruma kuu ya Mungu. Paulo hakuwa anahubiri mafundisho haya potofu, lakini alikuwa ameshitakiwa kwa kufanya hivyo pia.
Hili lilikuwa ni shambulio juu ya mahubiri ya Paulo ya kuhesabiwa haki kwa njia ya imani. Wayahudi walikuwa wanasema: wewe unatuambia Mungu anawahesabia haki watu waovu, kwanini wasiendelee kuwa waovu ili wema uweze kuja kutoka kwenye uovu?
Maelezo ya Paulo kwa hawa aliowahubiria yalikuwa ni: wale ambao hukumu ni haki yao. Kwakuwa shitaka halikuwa kweli Paulo hakwenda ndani zaidi kwenye jibu hili; yeye anathibitisha tu kwamba hukumu ya Mungu juu yao ni sahihi.
Kuhesabiwa haki ni kwa imani pasipo matendo ya sheria. Sheria ni: faida kwa wale ambao wanaijua (mst. 20-30), haijafanywa kama kitu cha kuepuka bali inathibitishwa kwa imani yetu. (mst. 31)
Dunia yote iko chini ya hukumu.
Mwenye dhambi ni nani? Tumeshathibitisha kuwa wote wayahudi na wamataifa wako chini ya dhambi kwahivyo wote wanahatia ya kuvunja sheria.
Shitaka rasmi ni shitaka lililoandikwa au shitaka la kawaida la mhalifu au mkosaji, hurejelewa kama baraza la wazee wa mahakama chini ya kiapo cha mahakama. —Webster
Hakimu mkuu haachi udhuru kwa ajili binadamu na Paulo ametumia neno lililoandikwa kuonyesha mshitakiwa.
Myahudi alitamka kwamba alikuwa na Maandiko; sasa Mungu anatumia Neno lile lile kufungua dhambi zao. Mungu anawafanya kuwajibika kwa Neno Lake.
Ulinzi wa mshitakiwa ni nini?
Mshitakiwa hana la kusema; kila kinywa kimefungwa.
Siku ya hukumu itakuwa ni siku ya kunyamaza kimya.
Sheria inarejea zaidi ya sheria ya Musa; vilevile pia kwenye sheria ya maadili na sheria ya dhamiri. Watu wamataifa hawakuimiliki sheria ya Musa, lakini kila mtu anasheria ya maadili ya Mungu ilioandikwa katika moyo wake na kuthibitishwa na dhamiri yake.
WARUMI 3: Kuhesabiwa ni kwa njia ya imani sio kwa matendo sheria. Sheria ni: faida kwa wale wanaoijua (mst. 1-2), ni halisi katika asili yake (mst. 3-8), haipindiki katika mamlaka yake (mst. 9-19), inayokusudi la pekee (mst. 20-30), sio kitu cha kuepuka bali zaidi imethibitishwa ndani ya mioyo yetu (mst. 31).
Sheria ni shitaka kwa asili dhidi ya wanadamu wote. Kusudi la kweli la sheria sio kumhesabia mtu haki, bali ni kuleta kuijua dhambi. Kipekee, sheria haiwezi kuzalisha wokovu au haki katika macho ya Mungu. Wokovu ni kwa neema kwa njia ya imani katika Yesu Kristo.
Mwenye mwili: ni mwili (ni kama kinyume cha nafsi (au roho)) ni ishara ya kile kitokacho inje, au asili ya mwanadamu pamoja na madhaifu yake (kimwili na kimaadili), hali ya kuwa na mwili.
Maana ya “kuhesabiwa” haki ni kutangazwa kuwa mwenye haki. Kuhesabiwa ni kuwekwa mahali penye uhusiano sahihi pamoja na Mungu. Paulo anaongea na watu jinsi gani wataweza kuhesabiwa haki au kutangazwa haki; kwa njia Yesu Kristo.
Kuhesabiwa haki: kurudisha (kuonyesha au kujali) mwenye haki au asiye na hatia: —uhuru, kuhesabiwa haki.
Umuhimu mkubwa, kuhesabiwa haki haimaanishi kwamba Mungu hutufanya haki, bali hututangaza kuwa wenye haki. Kuhesabiwa haki ni jambo la kisheria. Mungu huweka ya Kristo kwenye hesabu yetu ya wenye dhambi. —Wiersbe, W. W. (1996). The Bible Exposition Commentary
Bado, Wokkovu haujakamilika katika maelezo haya. Kwa kuwa katika tangazo la Mungu la kuhesabiwa haki, kwa kutupa haki yake ametufanya wenye haki.
War. 5:19—Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.
Kirahisi humaanisha kuwa haki ni kuwa kinyume cha ubaya. Dhambi ni ubaya na Mungu ni haki. Ilivyotumika kwa Mungu inarejea kuwa kamili au utakatifu wa asili yake; Mungu muda wote ni mwenye haki. Maneno haki na kuhesabiwa yako karibu sana na yametokana na neno lilelile la kigriki. Mzizi ni dika. Kuhesabiwa haki ni–dikaio, haki ni–dikaiosune.
Hii sio haki ya kuifanyia kazi au hata matendo ya haki. Kuhesabiwa haki ni haki ya Mungu kuwekwa kwenye hesabu ya mtu; Hiyo ni Mungu kumhesabia mtu haki kwa njia ya haki ya Kristo. Kifungu hiki humwonyesha mtu kuwa chanzo pekee cha haki ni kutoka kwa Mungu.
Mwenye dhambi hasitahili kupata haki. Mtu anasitahili kwa ajili ya dhambi. Mungu kwa uhuru huwahesabia haki wale ambao wanapokea utoaji ya Kristo kwa imani. Wokovu ni zawadi ya Mungu kwa wale wanao pokea utoaji wa Kristo kwa imani.
Ukombozi humaanisha kununuliwa, kuwekwa huru kwa malipo ya fidia. Yesu alilipa gharama kwa ajili ya wokovu wetu katika damu yake. Mtu anatangazwa kuwa haki kipekee kwenye stahili ya Yesu Kristo.
Kuhesabiwa haki sio tu Mungu kuonyesha huruma juu ya mwenye dhambi na kumwacha huru bila malipizi kulipwa. Neno uheri limetumika katika rejea kwa Kristo kukidhi matakwa ya sheria. Uheri sio sababu utekelezaji wa hukumu iliositahili. Huelezewa kwenye neno la kiebrania kumaanisha kiti ccha rehema ambacho kilikuwa kikiwekwa damu ya malipizi na kunyunyizwa ili kukidhi hukumu ya Mungu. Hii damu ya kunyunyiza ilifunika vibao vya sheria ikiwa nipamoja na sanduku la agano. Huu ni mfano wake yeye ambaye angekuja kumwaga damu ya kiungu kukidhi sheria. Damu ya Yesu ni sababu ya hukumu kutotekelezwa kuhusu mwenye kutubu.
Kipatanisho kihalisi humaanisha kuonyesha uondoaji wa ghadhabu kwa utoaji zawadi. Katika Angano la kale huelezwa kwa tendo la kukausha samaki (MALIPO). Jambo la kipanisho huinuka kwa ukubwa wa jambo kutoka kwenye dhana nzima ya ghadhabu ya Mungu, ambao watetezi wa mtazamo huu huwakilisha jamii na msemo wa kale. Wanahisi watu wa sasa hawawezi kushikilia dhana hii. Lakini watu wa Agano wa la kale hawakuwa na makatazo kama hayo. Kwa wao Mungu hukasirishwa na uovu kila siku (Zab. 7:11). Wao hawakuwa na shaka kwamba dhambi kwa kutoepuka huamsha mwitikio wenye nguvu kutoka kwa Mungu. Yeye kwa ujasiri yuko kinyume uovu katika kila muonekano na mundo wakati yeye huo huo yeey anaweza kuwa mpole wa hasira. -Kamusi mpya ya Biblia
Katika kipindi cha Agano la kale, damu ya wanyama haikuweza kuondoa dhambi (Waebr. 10:4). Damu ya wanyama ni kivuli cha damu ya Yesu, ilikuwa ni kitu cha muda mfupi hadi pale Yesu alipokuwa amekuja na kujitoa mwenyewe kama dhabihu ya kiwango cha juu kwa ajili ya dhambi. Tafasiri halisi ya fungu hiki ni kwamba Mungu alizipitia juu dhambi ambazo zilitangulia kufanywa. Yeye akijua kwamba Yesu angekuja kulipa gharama yote hapo msalabani. Damu ya wanayama ilikuwa kama hati ya malipo hadi gharama yote iishe kulipwa. Hapakuwa na mtu aliyekuwa ameokolewa kwa wanyama Watu wote wanaokolewa kwa damu ya Yesu Agano la kale na jipya.
Imani na haki - nenda sawa kwa sawa ukimwona mtu mwenye haki, umeona mtu mwenye imani. Kumbuka imani mbali na haki sio ya kimaandiko. Haki kwa halisi inafaa haki (Marko 11:22). Haki: ni uwezo wa kufikiri na kutenda kama Mungu. Kuna haki za aina mbili: 1. ya kuwekewa - tendo la neema (Mungu anaweka katika hesabu yetu) 2. ya kugawiwa-neema ya kushirikisha au kutoa. 1:17 - “maana kuna haki ya Mungu iliofunuliwa toka imani hadi imani.” Hatua: I Wakr. 1:30 kuna viwango vya imani. Tunabadilishwa toka kuamini hadi kuamini, imani hadi imani, utukufu hadi utukufu. “Metron” - Kigiriki - kipimo cha imani, kiwango, sehemu. Kipimo cha imani imani iokoayo. Ikiwa wewe una imani wewe una imani katika moyo wako.
Kuhesabiwa haki ni kwa imani nasio matendo ya sheria. Sheria: ni faida kwao wanaoijua (mst. 1-2), uhalisi katika asili yake (mst. 3-8), haipindiki katika mamlaka yake (mst. 9-19), inakusudi la kipekee (mst. 20-30), haiepukiki bali imethibitishwa katika mioyo yetu (mst. 31).
Kuhesabiwa haki kwa imani huthibitisha sheria.
Kuhesabiwa haki sio kinyume cha sheria ya Musa. Wokovu kwa imani katika Kristo Yesu umekithi haja ya sheria ya Mungu. Yesu kwa ukamilifu amekamilisha au kuthibitisha uhitaji wa sheria. Kuna rejea pia hapa ya sheria ya maadili. Imani haipuki sheria ya maadili ya Mungu. Sheria ya sherehe imekamilishwa na Kristo. Hatuhitaji tena sadaka ya mbuzi na mafahalikumtolea Mungu, wala kushika sheria za sikukuu. Sheria ya maadili ya Mungu haibadiliki. Kuhesabiwa haki haikomeshi sheria ya maadili ya Mungu.
Sheria ya imani haifanyi sheria isitumike au kuepukika, bali huithibitisha. Imani haiondoi wala kuharibu sheria, bali kuiboresha.
Sheria huleta kuijuwa dhambi kwa mtu, na huyo mtu ambaye ameitambua hali yake awezekuhesabiwa haki kwa imani. Pasipo sheria mtu hangeweza kuijua dhambi, na kwa hiyo hangekuwa na hitaji kwa ajili ya kuhesabiwa haki, ukombozi au malipizi ya dhambi. Sheria ambayo kwa mara ya kwanza ilivunjwa imethibitishwa kwa njia ya imani katika kazi iliomalizika ya Kristo kwa maana kwa njia ya haki yake IMETOSHELEZA.
Kazi ya sheria katika kuhesabiwa haki ni ile inayoleta kuijua dhambi. Mtu haihesabiwa haki kwa njia ya matendo sheria. Kwasababu kuhesabiwa haki inachukua nafasi katika muumini “kwa neema kwa njia ya imani.” Kwa Neema zawadi ya uzima wa milele imetolewa bure kwa ulimwengu wote ni kwa njia ya imani ambayo zawadi hupokelewa. Mungu amefanya ya kwanza kuondoka kwenye ukombozi na kwa ajili ya ule mpango kuwa wamanufaa kwangu, lazima nichague kupokea zawadi kwa imani. (Neema ya Mungu husaidiana na asili ya mapenzi huru ya Mungu aliyoyatoa kwa mwanadamu.) Angalia pia Waefeso 2:8 na Warumi 4:16. Kuhesabiwa haki kwa njia ya imani imeonyeshwa katika maisha ya Ibrahimu.
War. 4:3—…Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa haki.
Kwa nini Paulo anaongelea kuhusu Ibrahimu? Paulo anaelezea swali la Wayahhudi. Wayahudi walihusiana na Ibrahimu kwa undani. Abrahamu alirejewa kama baba yetu katika mistri ya 1, 12, na 17. Abrahamu alikuwa baba yetu kama alivyofungamana katika mwili, baba wa tohara, baba wa imani yetu, baba wa mataifa (hii ilikuwa ni ahadi ya Mungu kwake).
Wayahudi walikuwa wameshikiliwa katika uhusiano wao na Abrahamu (“wana wa Abrahamu kimwili”) kama dhamana yao kwa uzima wa milele. Wayahudi waliweka faraja kubwa kwa Abrahimu baba wa taifa lao hii ni swali la kiyahudi, Paulo analielezea:
War sura ya 4 inashughulika na “haki ya Ibrahimu.” Ibrahimu ni mfano wa kuhesabiwa kwa neema kupitia ya imani. Paulo anatumia maisha ya Ibrahimu kama YALIVYOONYESHWA KATIKA MAANDIKO MATAKATIFU kuelezea fundisho la haki kwa njia ya imani. Katika sura sura zote mbili ya 3 na ya4 Paulo anautoa ukweli kwamba yeye hahubiri injili ya kushindanisha maandiko ya (Agano la kale), bali za ni injili ambayo mwendelezo wa kusudi la Mungu la milele.
Mwanzo 15:6—Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
Kabla ya torati kwa Musa na kwa mda mrefu hata kabla hata musa kuzaliwa, Ibrahimu alikuwa amekwisha hesabiwa haki kwa imani kama ilivyo kwa wakristo wa leo. Mungu alimpa Ibrahimu ahadi; yeye alimwamini Mungu ikahesabiwa kwake kuwa haki (War. 4:4).
Wale wasio zaliwa mara ya pili ni wenye dhambi na wapagani. Mwenye kutubu hutangazwa kuwa mwenye haki na Mungu kupitia damu ya Yesu. Wapagani hawana lolote la kufanya kwa ajili ya kuupata wokovu. Watahesabiwa haki kwa neema tu kwa njia ya imani.
KUMBUKA: Mungu anadai imani na haghairi neema ya Mungu. Mashariti ya kuhesabiwa haki kwa matendo iko katika ushindani pamoja na neema ya Mungu ambao ni wema wake ambao ulikusudiwa tu kwasababu ya wema wa Mungu. Sharti la kuhesabiwa haki ni itikio la imani. Imani kikwelii inahitajika na kuhesabiwa haki kwetu bado ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu kama yeye alivyotupa karama ya imani ambayo kwa hiyo twaweza kuitikia neema yake. Kuhesabiwa haki ni kwa neema na pia ni shariti: kwa neema kwa njia ya imani.
Paulo anatoa ushuhuda kutoka kwa Daudi unaosaidia ujumbe wa kuhesabiwa haki kwa imani. Daudi alienziwa na wayahudi kama mfalme wao mkuu. Nukuu hii kutoka Zaburi huthibitisha kwamba watu huhesabiwa haki kwa imani tu na sio kwa matendo (Zab. 32:1-2).
Daudi alikuwa anamshukuru Mungu kwamba dhambi zake zilikuwa zimesamehewa na hakuhesabiwa dhambi tena. Ikiwa dhambi haikuwa ndani yake na kusamehewa hii humaaniisha yeye akihifadhiwa katika uhusiano sahihi na Mungu.
Wayahudi walitazamia tohara na sheria kama chanzo cha haki yao. Ibrahimu alihesabiwa haki kabla ya agano la tohara. Alihesabiwa kuwa mwenye haki katika sura 15 na alikuwa na umri miaka 86 katika sura ya 16 wakati Ishimaili alipozaliwa. Mwanzo 17:24 inatoa habari ya kutahiriwa Ibrahimu akiwa umri wa miaka 99. Inaweka wazi kwamba yeyealihesabiwa kabla ya kutahiriwa. Kifungu hiki kinawaambia wayahudi kwamba Ibrahimu alihesabiwa haki kabla ya kupokea agano la tohara.
Tohara haikumhesabia Ibrahimu haki. Tohara ilikuwa imetolewa kama ishara ya ahadi. Ilikuwa imetolewa kama mhuri wa haki ya imani. Ni alama ya kuindoa sehemu ya mwili. Hakuna nguvu ya haki katika tendo la kimwili. Hii kwa uhalisi ni kazi ya Mungu mara nyingi katika njia hiyo hiyo ubatizo ni alama ya kazi kamili.
Sheria inaleta kuitambua dhambi (mst. 15). Inasema mahali ambapo hakuna sheria hakuna uasi inarejea kwenye ukweli kwamba ikiwa hakuna sheria basi hakuna kuivunja sheria. Hii pia lazima inarejea kwenye sheria ya maadili kama ilivyo kwa sheria Musa. Ibrahimu alikuwa amehesabiwa kwa imani kwa njia ya neema (mst. 16). Hakujipatia haki kwa uwezo wake mwenyewe;Itolewa pasipo kusitahili kwasababu ya imani yake.
Abrahamu alipewa ahadi ya Mungu. Mungu alimwahidi kuwa atakuwa na mwana. Pia Mesiha angekuwa mwana wa Ibrahimu. Yesu alitimiza unabii na aliziwa kulingana na ukoo wa mababu wa Abrahamu.
Mtu hupokea kuhesabiwa haki kutoka kwa Mungu kwa imani—“kama tunaamini…”
Abrahamu aliamini ahadi ya Mungu. Dhidi ya tumaini aliamini katika tumaini. Abrahamu aliamini ahadi ya Mungu bila kujali hali. Sara alikuwa na miaka karibia 90 na Ibrahimu alikuwa ni miaka zaidi ya 100. Hapakuwa na njia ya asili ya wao kujipatia mtoto. Abrahimu alikuwa hajakata tamaa kwa ahadi ya Mungu (mst. 20).
Kuhesabiwa haki ni kazi ya kimungu. Mtu hawezi kujihesabia haki mwenyewe zaidi ya kule Ibrahimu kupata mwana. Kuhesabiwa haki ni kazi ya Mungu inayotolewa kwa neema katika kuitikia kwa imani.
IKIWA TUTAMWAMINI
War. 4:24—bali na kwa ajili yetu sisi mtakaohesabiwa vivyo hivyo, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu katika wafu;
Zifuatazo ni hoja zilizo tolewa:
Mtu akifanikiwa kuifikia Neema ya Mungu na kuhesabiwa haki kwa imani kwa kupewa na Mungu. Nafasi muhimu sana kwa imani kupokea huu utoaji inawezekana kama matokeo ya upendo wa Mungu na neema iliyoonyeshwa katika kifo cha Kristo. Tulinyamazishwa na sheria kwa hukumu yake juu ya dhambi, lakini uwepo na na ufahamu mzuri wa Mungu, ulipatikana kwa imani katika Yesu Kristo. Katika sura hii Paulo anasisitiza jukumu la Bwana wetu Yesu Kristo kwa waamini kuhesabiwa haki na kupata upendeleo kwa Mungu au “neema.”
Hivyo ni nani atakayepata faida ya wokovuo? Yesu! Hakuwa mkuu bali kazi ya imani pekee ndiyo iliyompendeza Mungu, kwasababu hapakuwepo na nafasi kwa imani kufanya kazi hata ikawezekana bila Kristo. Alihusishwa kwa mpango wa Kristo ambaye Mungu alimpa kibali kwa mwanadamu ili kumwokoa kwa imani.
Wenye dhambi wako katika kifungo na hawezi kufurahia utimilifu wa Mungu uliotaka kuwabariki. Yeye aliyafanya kwa sababu ya dhambi. Ikiwa mtu ana nafasi yake katika Kristo na kwa kuawa kwake ni kwasababu ya dhanbi zao, yule mtu atapata mambo ya ajabu mengi kupitia hazina ya Yesu ambayo itamwezesha yeye kupata Neema ya Mungu kwa wingi. Yafuatayo ni baadhi ya Maandiko juu ya wingi: Mithali 28:20; Warumi 5:20; 15:13; II Korintho 8:7; 9:8; Wafilipi 1:9; 4:17; I Wathesalonike 3:12; 4:1; II Petro 1:5-8. Soma Warumi 5:1-5.
Kupitia Yesu:
Pia angalia II Kor. 1:22; Gal.4:4-7; Efes 1:13-14.
Baraka zote zilizotangulia (kuhesabiwa haki, amani, upatikanaji, n.k.) yaliwezekana kwasababu, “Hatukuwa na nguvu bado, mpaka wakati wa kufa kwake Kristo kwa ajili ya wenye dhambi.” Ni damu ya Yesu Kristo iliyoishinda sheria na msukumo wa upendo wa matendo yake.
“Upendo” wa mtu humhusu yeye mwenyewe na una kikomo. Kwa wale ambao hufanya ya kidini na unaweza kumpata mtu kufa kwa ajili ya vitu vizuri na kwa wale wema na wakarimu, wanaweza kutapa mtu yeyote kwa urahisi zaidi kufa, lakini Yesu hakufa kwa wale waliokuwepo kupata thamani na utajiri, bali alikufa kwa ajili ya wahalifu, wavamizi. Yeye alikufa kwa wenye dhambi.
Kristo Alikufa kwa wenye DHAMBI, wale wakosaji na waliomkataa Mungu. Upendo wa Mumgu ulionyeshwa kwa wale wasio haki wala wema.
Tuliuwa wa ajabu kwa Mungu. Tulikuwa:
Yesu alisukumwa na upendo, na alituokoa kutoka kwenye laana na akatupa kuhesababiwa haki kupitia damu yake.
Upatanisho maana yake “huja kwa maneno; makubaliano.” Nilipopatanishwa kwa Mungu, alirekebisha maneno na kunibadilisha. Soma II Wakorintho 5:17 na Isaya 1:18-20
Upatanisho ni lazima kufanyika kwa mahusiano ya mtu na Mungu. Tunatakiwa kupokea huduma ya upatanisho (II Wak. 5:16-21). Mungu humbadilisha mtu vizuri kupitia upatanisho, na haya mabadiliko ni kazi ya Mungu. “Vitu vipya” huumbwa na Mungu, kama vile katika uumbaji Mungu alisema na iwepo dunia. Dunia katika chanzo chake. Wokovu ni Mungu aliupatanisha ulimwengu Mwenyewe.
Tumekuwa mabalozi wa ofisi ya upatanisho (War. 5:19-20). Dhambi ya mtu humtenga yeye kutoka kwa Mungu, lakini hutufanya sisi tukubali maneno ya upatanisho (War. 5:21).
Ukweli ni kwamba Mungu ni pendo na Kristo atabaki mwenye Haki haitoshi peke yake kumhesababia mtu haki. Gharima lazima ilipwe kwa ajili ya dhambi na Kristo ndio aliyolipa hiyo gharama kwa damu yake mwenyewe (upatanisho). Katiak msitari wa 11 hadi 18, Paulo aliandika tofauti ya Utawala wa Dhambi na utawala wa Neema.
Kama vile dhambi ilivyo tawala mpaka kifo, neema imetawala kupitia haki mpaka uzima wa milele. Kama vile sheria ilivyokuwa na mamlaka juu ya wale waliovunja sheria, Hivyo neema ina nguvu na mamlaka juu ya haki. Kama vile muumini alivyo na nguvu na mamlaka kutawala katika uzima, watakuwa na nguvu na mamlaka kutawala katika umilele. Dhambi ya Adam iliendelea kwa hukumu ya sheria na kumtawala mpaka kifo. Utawala wa neema ya Mungu uliongezeka kwa kuendeleza haki kwa Yesu Kristo Bwana Wetu mpaka uzima.
Neema ni upendo, kama inavyoonekana katika kifo cha Kristo kwa wasio mcha Mungu na katika maisha ya Yesu alivyoyatoa kwa wale ambao Yeye aliwaokoa kwa njia ya kifo chake. Hukumu ni utumwa kupelekea mauti kupitia Adamu. Kuhesabiwa haki ni kutawala katika uzima kwa njia ya Yesu Kristo. Kwa Kristo watu wote watafanywa hai.
Paulo aliandika tofauti yenye nguvu sana ya utawala wa dhambi na utawala wa neema:
| Tofauti katika Warumi sura ya tano | |
|---|---|
| Dhambi | Haki |
| Kifo | Uzima |
| Sheria | Neema |
| Maadui | Upatanisho |
| Kutotii | Utii |
| Kuhesababiwa | Haki |
| Hukumu: Kuwahukumu watu ni utumwa wa kifo kwa Adam. | Kuhesabiwa haki ya Uzima: Kuwahesabia watu haki ilitawala katika uzima kwa Kristo. |
| Hasira | Amani |
| Wenye dhambi | Walio okolewa |
| Utawala wa dhambi | Neema imeongezeka |
Katika surta ya sita, Paulo alianza kwa kuweka wazi mahusiano ambayo waumini waliokuwa na dhambi na kuhitimisha kwamba dhambi haitaendelea kutawala juu ya waumini na wale waumini wasiendelee katika dhambi. Paulo alijibu swali “Tufanye dhambi?” kwa kuwaliza na alitoa majibi mawili ya kufanana lakini maswali tofauti:
Paulo alithibitisha hilo kwa kuwa hakuna sababu nzuri ya kufanya dhambi. Hakuna sababu sahihi ya kufanya dhambi au ya kunufaisha.
Paulo alifundisha kuwa kuishi katika dhambi lakini kama tutafia dhambini isiwezekane. Ama ufe katika dhambi au uwe hai katika dhambi. Wakati umeokoa hundi ya timu kwa faida, moyo wa mwathirika unaweza kusukuma damu au moyo wake unaweweza kutulia. Kama tutasulubiwa katika Kristo, Mungu hatainua tena ule utu wa kale, bali Mungu atatuinulia juu upya wa uzima kale.
Paulo aliwaeleza waumini mahusiano ya kufanya dhambi kama “kifo” kwao.
Wokovu ni dawa kamili kwa mwanadamu (mwili, nafsi, na roho). Mpango wa Mungu wa Wokovu hauwezi kuzuiliwa katika kuhesabiwa haki (kurekebisha mahusiano ya waumini katika sheria), bali kuendelea katika utakaso (kumrejesha mwanadamu kutembea na Mungu), ambaye ni kilele katika utimilifu (Wokovu umekamilishwa). Wokovu katika Biblia ni neno ambalo linajumuisha matendo yote ya ukombozi na ni umiliki wa Mungu: Kupitishwa, kuhesabiwa haki, ukombozi, kuzaliwa mara ya pili, neema, upatanisho, mkazo, kugawa, msamaha, utakaso, utukufu na ukamilifu. Soma Warumi 8:29-30.
Agano Jipya linaeleza Wokovu katika nyakati tatu: uliopo, uliopita, na ujao:
| Uliopita | Uliopo | Ujao |
|---|---|---|
| Tumeokolewa: alimaliza kwa wakati uliopita | Tunaokolewa: kitendo kinachoendelea | Tutaokolewa: itakamilika kwa wakati ujao |
| Tumeokolewa kutoka kwenye adhabu ya dhambi na hatia: Kuhesabiwa haki, msamaha, kuokolewa | Kutoka nguvu ya dhambi: endelevu -> kutakaswa, kusafishwa | Kuokolewa mbali na dhambi kwa wakati uliopo: Alitukuzwa, imekamilika |
| Nafsi, mwili, roho | Uzima, mazungumzo, mwenendo | Kukamilishwa, fanikishwa, kumaliza |
| II Tim. 1:9; Tit.3:5; Efes. 2:8-9; Luk.7:50; Yoh.5:24; 6:47; | I Kor. 1:18 (“Tumeokolewa”), Filp. 2:12 II Kor. 2:15; II Kor. 15:2; Efes. 2:5, 8; Rum. 6:14; Gal. 2:19—20; IIKor. 3:18 | Rum. 5:9; 8:23, 24; 13:11; Mat. 10:22 (24:13; Mark. 13:13); Yoh. 10:9; Rum. 10:13; IKor. 3:15, 5:15; Efes. 1:13, 14; I Thes. 5:8; Ebr. 10:36; I Tim. 2:4; I Petr. 1:5, 4:18; I Yoh. 3:2—3; Mat. 25:46; Mark. 10:30; Tit. 1:2—3. |
Tunaweza kupata maelezo ya muhtasari katika II Wakorintho 1:10:
II Wakorintho 1:10—Aliyetuokoa sisi [WAKATI ULIOPITA] katika mauti kuu namna ile [WAKATI ULIOPO]: ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa [WAKATI UJAO];
Tume batizwa kupitia kifo cha Kristo, tumesulubiwa pamoja na Kristo, na kuifia dhambi (mst. 1-6).
Muumini ni “aliyeifia dhambi” (Rum. 6:2, 11, 7:4, 7:6; Gal. 2:19; Col. 2:20, 3:3).
Ina maanisha nini kuifia dhambi? Au ni nini matokeo ya kuifia dhambi? Paulo ametutambulisha kwetu picha ya kifo na kuandika usawa kati ya kifo cha Kristo na Ufufuo na kfo cha kiroho na ufufuo wa muumini. Hebu tuufikirie huu usawa wa kiroho na kifo cha kimwili:
| Tumetambuliwa na Kristo kwa njia ya kifo chake | |
|---|---|
| Alikufa kifo cha asili | Tulikufa kifo cha kiroho |
| Alikufa kwa ajili ya dhambi ya ulimwengu wote | Tunakufa kwenye dhambi |
| Alikufa kwa njia ya uhamisho, mateso, kukamilisha Utukufu wa Mungu | Tunakufa kwa njia ya aibu ya asili ya miili, kuua mwili, kusulubisha maisha binafsi. |
Baadhi ya watu wanasema “Mimi nimekufa kwa dhambi,” lakini wakati mgumu ukiwajilia miili yao itapiga kelele. Kama tutakuwa wafu ndipo hatutasikia kitu chochote katika majaribu ya dhambi, na hatuta ungua kwa moto kwa hali ya shinikizo. Wafu hawasikii na wala hawana hisia yeyote.
Mtu aliyekufa hana haja na nyama au mboga. Hivi ni vyanzo vya vyakula, na mtu aliyekufa hana uhai wa kuendelea. Mtu aliye hai anakula kwa kusudi la kuendeleza uhai. Kama tutausulubisha mwili, kwanini tubakie katika wakati mmoja wa kupigania kuendelea kuwa hai? fisha ile asili ya kale, na lisha mtu wa rohoni.
Mtu anaweza kuishi maisha yote yakiwa yamejaa ulevi na na aina zote za ubinafsi na dhambi, lakini ajapo kufa, roho yake huacha mwili na ule mwili hauwezi kubeba uhai. Watapumzika katiak mikono ile sawa na wale walioshinda vita, miguu ile ile kwa walio kimbia haraka uovu, bali sasa wajapo kufa na roho zao zitaenda katika sehemu pa mwanga penye ushahidi wa maisha yote—mazuri au mabaya.
Kifo hiki kina mwisho kwa waumini wake wa asili ya dhambi. “Utu wa kale” hautafufuliwa tena, bali “utu upya” utafufuliwa katika sehemu yake. Kumbuka, watu wanajiuliza katika sehemu hii, “Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuongezeka?” Kufahamu lugha ya “kifo” na “uzima” Paulo alitumia, ni lazima tufikiri kile “kinachofunga mahusiano” ni nini. Umri wetu wa kuishi, ni vigumu kuhitimisha kwamba kifo lazima kichukue nafasi ili mwisho wa mahusiano uwepo. Chochote tunachokichagua kukifanya kwa akili zetu na miili, kuna sheria za rohoni ambazo zinaongoza haijalishi mtazamo wetu wa nje. “Vifungo viwili vya mahusiano” katika Maandiko ni:
Kifo hiki ni mwisho wa waumini wenye mahusiano na dhambi (utu wa kale). Kabala hatujasulibishwa pamoja na Kristo tulikuwa watumishi (watumwa) wa dhambi (Mith. 13:15) na mlikuwa wafu katika dhambi (Efes. 2:1).
Hatufanani (Gal. 6:14). Tume:
Kwasababu tulikufa kwa ajili ya dhambi, tumekuwa huru mbali na dhambi (mst. 7). Kwasababu tulikufa pamoja na Kristo, tutaishi pamoja naye!
Tulikufa katika dhambi, bali tu hai kwa Mungu. Dhambi ilitisha na kushindana na Kristo.
Chukua mamlaka juu ya akili yako katika jina la Yesu. Mstari wa 12 unasema, “Basi, dhambi isitawale….” Kuna nguvu katika Mungu (Neema yake) ile inayomwezesha mtu kuwa mfu wa dhambi na kuishi kwa haki. Muumini afanyie mazoezi imani yake kwa uthabiti wa maono ya Mungu ambayo muumini hatakuwa chini ya utawala wa dhambi. “kujitawala mwenyewe” ni muhumu kwa watakatifu ili kubaki chini ya neema na kutoka chini ya laana ya sheria. Zingatia maneno yanayotegemea matendo ya watakatifu katika mistari hii: “jifikirie ninyi wenyewe…,” “Kwahiyo usiache dhambi itawale katika mwili wa mauti…,” na “Wala ninyi msizalishe vyombo visivyo vya haki katika dhambi: bali vuneni yaliyo kwa Mungu…” Tunaishinda dhambi kwa Neno la Mungu—kwa kufanya kile anachokisema. Kujizalisha wenyewe kwa Mungu maana yake ni kwamba kujitafutia sababu ya mizizi yenu na kuing’oa kutoka katika maisha yenu.
Mtakatifu amewekwa huru kutoka kwa bwana wae wa zamani aliposulibishwa pamoja na Kristo, lakini alipata bwana mpya. Ubwana wa maisha ya muumini yamemilikiwa na Kristo. Tuko huru mbali na dhambi, lakini hii pia maana yake tumefungwa kwenye haki. Dhambi ni mtego wa utumwa wa Shetani, bali haki ni huduma ya Kristo. Basi mkifanya dhambi ninyi ni watumishi wa Shetani, na sio watumishi wa Mungu. Huwezi kutumikia dhambi na pia kuwa mtumishi wa Mungu.
Neema ya Mungu ni udhihirisho katika kutupatia upatanisho, kwa kuifunika dhambi (damu ya Yesu) (Efes.1:7). Neema itatawala kwa njia ya haki (War. 5:21). Neema ya Mungu haiwezi kutusaidia sisi kutumikia dhambi, bali inatuwezesha kumtumikia Mungu. Watumishi wa Mungu wajitakase" wajitenge mbali na dhambi na wajitenge kwa Mungu. Neema ya Mungu ni ushawishi wa Mungu juu ya moyo na fikra zake katika maisha (Luk. 2:40; Yoh. 1:14; 1:17; Mdo. 4:33).
Maisha ya Mkristo ni ya hiyari, lakini tuwe wazalishaji wa hiyari sisi wenyewe kwa Mungu, tutakuwa watumishi na hivyo wajibu kama watumishi uko kwa bwana wao.
“Tabia ya zamani ni ngumu kufa.” Kitu kinachobadilisha utumishi wetu kutoka kwenye dhambi ni wewe mwenyewe kwa Mungu, tunatakiwa tuwe na tahadhari katika jitihada zetu za kumtumikia Bwana wetu kwa uaminifu. Tunaelekezwa kufanya baadhi ya mambo:
Matunda gani mtakayoyapata? Faida gani ya hudumu yako? Ni mshahara wa kazi yako. Mkristo lazima atahayarishwe kwa utu wa zamani na kutumikia dhambi kwasababu dhambi humfanya mshtuko kwa kila mmoja (Efes.5:12).
| Mtumwa wa dhambi | Mtumwa wa Haki |
|---|---|
| Huru toka haki | Huru toka dhambi |
| Tunda la aibu | Tunda la kumuadhimisha Mungu, utakatifu |
| Kifo | Uzima wa milele |
| Mshahara wa dhambi ni mauti | Karama ya Mungu ni uzima wa milele kupotia: Yesu Kristo BWANA Wetu. |
Sheria kwa amri zake za hukumu zilitawala juu ya mtu yule anayeishi ndani ya dhambi. Maisha ya haki hayawezekani kwa kupitia kazi ya sheria kama wenye dhambi walivyofungwa dhambi zao. Hii sura inahusu umwili na mahusiano ya dhambi (kama waishivyo) kwenye dhambi na mauti. Sura hii pia inasisitiza kwamba sheria ya Mungu ni utakatifu. Kuna vitu vitatu katika sura hii:
Afanyaye dhambi yuko katika kifungo cha mahusiano ya dhambi yake, kama vile mke aliyefungwa na mme wake. Kama wataendelea kuwa hai wote wawili, mme na mke wamefungana kila mmoja chini ya Mungu.
Paulo alitangaza kifo! ni kifo cha binafsi. Kama mke atakuwa huru kutoka kwenye torati ya mme wake ni kwa kifo, hivyo wenye dhambi watakuwa huru kutoka kwenye sheria ya dhambi kwa njia ya kushiriki kifo cha Kristo. Kifo hiki ni kuusulibisha utu wa zamani pamoja na Kristo (Mdo. 13:38-39; War. 3:25; 5:21; 6:6; 7:4; II Kor. 5:15; Gal. 1:4; 2:20; 5:24; 6:14; Efes. 4:22; 5:2; Col. 2:11; 3:5, 9; Tit. 2:14; Ebr. 9:15; I Petr. 1:21; 4:2; I Yoh. 2:2; 4:10). Basi alimfufua katika ufufuo, tunashiriki katika maisha ya Kristo ambayo kwa nguvu za Mungu tunaweza kuwa mwanandoa wa ndoa nyingine. Katika ndoa hii ya pili, Tumeungana pamoja na Kristo.
Kadiri mtu anavyo ishi katika dhambi yuko chini ya sheria, na njia pekee ya kuepuka ni kuifia dhambi zake. Atendaye dhambni hana chaguo bali kuwa chuni ya sheria. Kifo huvunja wajibu wa sheria ya wa ndoa. Mtenda dhambi anaweza kuwa huru kutoka kwenye nguvu ya dhambi na adhabu ya kuvunja torati (7:4; 6:14).
Paulo alirudia maneno “hamjui” mara tatu wakati akizungumzia hili somo:
Kutokana na umoja huu wa Kristo utumishi wa Kristo utakuwa wetu (mst. 6).
Umoja wetu pamoja na dhambi huzalisha mauti (7:5; 1:32; 6:21; 7:5; Gal. 5:19-21), bali umoja pamoja na Kristo unatuwezesha sisi kuzaa matunda ya haki katiak utakatifu (1:13; 5:3-5; 6:22; Yoh. 15:2, 4, 5, 8, 16; I Kor. 1:6; Gal. 5:22-23; Efes. 5:9; Filp. 1:11; 4:17; Kol. 1:6, 10; Tit. 3:14; Ebr. 12:11; 13:15; Yak. 3:18; 5:7; II Pet. 1:3-9).
Katika Warumi 7:7-13, Paulo alianza na uzuri wa sheria ya Mungu na udhaifu wa dhambi. Paulo aliwaandikia Wayahudi, wale ambayo waliifahamu sheria (mst. 1), na kujua kujenga vizuri kusudi na asili la sheria. Idhini la barua ya sheria haiwezi kumfanya hata mmoja kuwa na haki, bali katika usahihi wa kuamsha watenda dhambi katika hitaji lao la Kristo.
Kwanini Paulo aliuliza sawli hili? Paulo aliandika katika mstari wa sita kuwa sheria ilikuwa kitu kinachopelekea kitu fulani. Hii ilionekana kushawishi kuwa sheria ni “mbaya.”
Dhamira kuu ya sura ya saba ni mahusiano ya muumini kwenye sheria. Muumini aungane na Kristo, ambaye ni “mme mpya.” Tulipozaliwa tulifungwa kwenye sheria kama ndoa. Tuliuwa huru mbali na sheria, kwasababu sheria haitakufa kamwe au sisi kubadilika lazima tufe. Tumekuwa wafu kwenye sheria kwa njia ya mwili wa Kristo, ambao ulituruhusu sisi kuoana na Kristo, alifufuka kutoka wafu.
Kutumikia waraka wa zamani wa sheria haukumfanya Paulo kuwa mwenye haki, bali badala yake ilifunua wazi uovu. Sheria haikuwa sababu ya dhambi zake, bali ilikuwa kama kiongozi mkuu wa shule na ilimfundisha yeye dhambi ilikuwa nini. Kwa kawaida ya jamii, Paulo hakuwa na kosa isipokuwa yeye alifuata matamanio yake, bali sheria ilihusisha kiwango cha Mungu ambaye kwa matokeo wazi ya uharibifu wa moyo wake.
Sheria yake ni mapenzi yake. Ilishauri kile ambacho ni rahisi, na sahihi, na jema na kukataza kile ambacho hakifai, jeuri, na kuumiza.
—Adam Clarke
Sheria ilifunua ukweli wa dhambi (Kol. 3:5; I Thes. 4:5). Matokeo ya ulimwengu yangekuaje bila sheria? Sheria ilikuwa muwakilishi wa agizo (amri) usalama, utulivu, uaminifu, sare, usawa. Kutokuwepo kwa sheria kulizua machafuko, kwa watumishi wabaya. Kama nguvu ya sheria ilizuiliwa matokeo yake yangekuaje? Mwisho wa dunia.
Paulo alizungumzia dhambi kwa kutolea mwanadamu mfano na kwa kufanya hivyo aliweza kueleza dhambi kutoka kwa mtu. Upanga wa rohoni hukata migawanyo ya hukumu ili kwamba tuweze kuona tunaweza kuwa huru mbali na dhambi. Kama dhambi ina sifa ya kumsubiri adui kudaka na kuchukua faida ya mtu mwingine, ndipo yule mwingine aweze kumpa mwingine kwa njia ya haki, kanusha ile dhambi. Mauaji yapo miongoni mwa mtenda dhambi. Lakini, kama dhambi pekee ina atahari ya asili ya moja kwa moja, hukumu inaweza kufanyika vipi kwa haki?
Nini ilikuwa hoja ya faida kwa dhambi? Sheria inaeleza mtenda dhambi ni kama mfu katika dhambi yake. Kuwa mfu, dhambi ilichukua faida ya uasi na kufanya vifo zaidi.
Sheria ni kama msitari wa tamaa: Inaonyesha wapi na nini iko katika macho ya Mungu. Ilikuisudia kuamsha watenda dhambi kwa hitaji lake kwa Kristo. Ndipo sheria ilikuja kuwa mwelekezaji kwa Kristo ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
Chini yua sheria, mwanadamu alihukumiwa kifonkwasababu ya dhambi. Warumi 7:5 inaeleza hali ya Wayahudi kimwili wakiitumikia dhambi ambaye waliichukulia wako chini ya sheria. Ilionyesha kuwa ilikuwa laana (Walawi. 27:26; 28:15; Zab. 119:21; Yer. 11:3; Gal. 3:10).
Matokeo ya mwisho kwa Paulo aliyefuata sheria kwa nguvu na kuitunza kwa bidii, alikuwa amekufa katika dhambi! Dini zake zote zilifanya kazi kwa pasipo haki—katika nuru ya msalaba, amri zote za Mungu zilikuwa hukumu ya kifo.
Dhambi ilichukua faida yetu na ilitudanganya. Sheria ya Mungu ikaja kujulikana kwa njia tofauti: Sheria za sikukuu, sheria za kijamii, sheria za asili, sheria za madili, na sheria za afya. Wayahudi waliamini ukitunza sheria hizi zote utakuwa mtakatifu. Kwa wakati wa Paulo kufanya huduma, Marabi walikuwa na jumla ya sheria 613 katika amri za Agano la Kale. Haikuwa rahisi kuzitunza hizo zote, hasa hasa tangu zilipoharibiwa mbele ya kusudi la Mungu.
Sheria ilifunua madhara ya dhambi. Madhara ya dhambi zote ni kifo cha kiroho. Madhara ya kufa kimwili pasipo kutubu dhambi ni utengano wa milele kutoka kwa Mungu. Kwa kutoweza kutekeleza sheria mkosaji akawa anahukumiwa kifo chini ya sheria. Amri haiwezi kukupa uzima, bali inaweza kukutuhumu kwenye dhambi kwa kupitia hukumu ya kifo na inakusababibsha wewe kutubu na kutafuta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
Sheria ni takatifu, ya pekee na nzuri, ya kawaida, ni mstari wa kina, amri inatuonyesha wapi na tuko katika upande gani wa Mungu; dhambi inatuonyesha kwa nini “waovu wanaendelea.” Mbali sana na alama ya ile ya Mungu aliyetuwekea sisi kwa ajili ya Kristo. Ni kusudi lake kutuhumu wafungwa wa dhambi na njia pekee ni kupitia kwa Kristo pekee kutafuta toba. Ina laana, shutuma, huzuia, na kuongoza kuamsha wakosaji kwa Kristo (3:19, 13; 7:8-11; 8:3; Gal. 3:19-24). Dhambi inaweza kufichwa katika jamii ya watu ikilinganishwa kwa mtu mmoja na mwingine au pia kwa kuhukumiwa tu kwa amri ya moyo wake mwenyewe, lakini katika nuru ya utakatifu kamili, dhambi itakuwa “inazidi sana.”
Katika Warumi 7:14-25, Paulo anatuleta katika mzizi wa mapambano; kusudi letu la kushindana kwetu daima ni miili yetu wenyewe, “mwili wa mauti” (mst. 24).
Kila muumini amependelewa, amewezeshwa na awajibike kuishi maisha matakatifu. Kwa kupumzika katika sheria tumehesabiwa haki, ni muhimu kuwashawishi wale wote waliokosea. Sheria haitoshi kwa haya bali neema kupitia Yesu Kristo ndiyo iwezayo. Wayahudi wanaamini kujitoa katika kujitoa kwao kwenye ibada za sikukuu za kisheria, na kwa uhuru ukaja chini ya injili ya Mungu kwa kupitia Yesu Kristo Bwana Wetu na Mwokozi (mst. 1-4).
Ufunguo wa maana wa sehemu hii ni msingi katika kurudia rudia kwa Paulo kujirejelea mwenyewe (“mimi”, “yangu”). Angalau, mara 48 katika sura hii, Paulo alionyesha mapungufu wake mwenyewe bila kutaja hata mara moja Roho Mtakatifu. KUMBUKA: Katika sura ya 7 sheria imetajwa zaidi ya mara 20 na katika sura ya 8 Roho Mtakatifu ametajwa zaidi ya mara 20.
Sauti hii ilichukuliwa katika sehemu hii ni katika sehemu kesi ya Paulo akitumia diplomasia (utaalam). Badala ya kutoa maneno ya dini yake na bidii ya wasomaji kwasababu ya kujilinda, Paulo alifika kwa ndugu zake na alijiamini mwenyewe na kushuhudia kwa uzoefu chini ya sheria:
Msisitizo wa kina juu yake mwenyewe akionyesha hali ya udhaifu wa mwili. Paulo katika uzoefu wake wa kutushirikisha kuwa chini ya sheria alishuhudia kile alichopigania kukifanya, na vitu vya kina alivyo vishindwa kuvifanya kwa nguvu zake mwenyewe.
Maneno 2 katika kiyunani (kigriki) kwa mwili. Moja ina maana kwamba ambaye ni kifaa sahihi, na nyingine ina maana kwamba ni ya maadili. Ya kwanza ina sema asili ya mwanadamu ni udhaifu, na ya pili inasema sifa ya mwanadamu ni mwenye dhambi.
Hapa tunaona Paulo akieleza mapigano. Kwa kuwa yeye alikuwa mtu mwenye mwili, haliokai lilo jema kwa sababu ya ushawishi wa dhambi.
Yeye alifahamu daima maadili tunaambukizana na chuki ndani yetu yetu. Alikuwa na shauku ya kufanya mema na bado mabaya mara zote yapo.
Katika mkono mmoja utu a ndani ni furaha katika sheria ya Mungu. Katika mkono mwingine aliona sheria tofauti katika washirika wake waliosimama kinyume cha sheria ya akili yake na kumleta katika kifungo cha kiroho. KUMBUKA: “mtu wa ndani” hata baki kama akivyokuwa “utu upya,” wala akili itatumika milele kwa kuhuisha ile asili. Haitaiweza sehemu ya mwili.
Mstari wa 24 unalia kwa uchungu na mashindano:
Ole wangu mimi! ni nani atakaye niokoa na mwili huu wa mauti?
Mwili wa kifo hiki ukiwa na hofu! hauja kombolewa, hauja badilishwa, na uko chini ya sheria ya dhambi. Kukaa bila kufunguliwa kwa jinsi ya mwili ni kutafuta “mauti ya mwili.”
Warumi 3:9—Ni nini basi? tu bora kuliko wengine? La! hata kidogo: Kwa maana tumekwisha kuwashtaki Wayahudi pamoja na Wayunani, ya kwambna wamekuwa chini ya dhambi;
Warumi 6:14—Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi: Kwa maana hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema.
Naweza kuepuka uovu? Ndio! Njia tumepewa kwa dhambi kutokaa (Efes. 6:13; II Petr. 2:20; I Yoh. 2:13; Col. 3:1-3). Akili zetu haziwezi kuwa mateka kwa dhambi (Warumi 12:2). Mstari wa 25 unasema, “Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana Wetu.” Kwa kifupi, Paulo alijua:
Warumi sura ya nane inazungumzia ushawishi wa “Sheria ya Roho wa Uzima” juu ya Mwamini. Matokeo ya mwisho ya wokovu kupitia Yesu Kristo ni ukombozi wa maisha ambayo zamani yalikuwa yamehukumiwa na Mungu kwa maisha yaliyotukuzwa na Mungu. Kusudi la Mungu kwa Mkristo ni kuwatukuza pamoja na Kristo. Roho Mtakatifu anafanya kazi katika maisha ya mwamini akizalisha matokeo ya Mungu. Wale walio ndani ya Kristo hawalaaniwi tena, lakini wako kwenye njia na mchakato wa utukufu wa Mungu.
Ina maana gani kuwa ndani yua Kristo?
Kuwepo kwa Kristo ni kushirikishwa katika Mzabibu wa keli. Maisha yake aliyaweka kwetu na kile kilicho chake kimekuwa chetu. Mungu Baba ametuonyesha vile vilivyoko kwa Mwanawe wa pekee ambaye tumekuwa warithi wa Mungu. Kwa Kristo, hatushindani na mwili bali dhambi pekee, na wala hatupati ondoleo la dhambi pekee, bali tumempokea Kristo Mwenyewe. Waumini wako kwa Kristo na Kristo yuko kwa waumini (11:16-18).
Paulo alipiga kelele juu ya ukombozi katika 7:24 na kutangaza katika 8:1. Ubora wa maisha mbele ya vizazi vya kidini ni baadhi ya vitu vya kutisha, bali mtu mpya katika Kristo ana uzoefu mkubwa wa uhuru. Hakuna hukumu tena ya kifo kama mtu aliyefungwa kwa maiti, Kwa maana hiyo sasa hakuna hukumu kwao kwa wale walio kwa Kristo Yesu. Dhambi huleta kifungo, bali sheria ya Roho ya uzima katika Kristo Yesu ilikuwa kazi kubwa ya uhuru! Nafasi yetu kwa Kristo ikiwemo uhuru kutoka kwenye hukumu.
Matendo mema ya sheria yamekamilishwa kwetu kupitia kumfuata Kristo kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu. Kuna njia mbili kutembelea njia ya uzima: 1) Kwa kuufuata mwili 2) Kwa kumfuata Roho wa Mungu. Mapenzi yangu mara zote yanafanya kinyume cha mapenzi ya Mungu, lakini ukiutanguliza mwili juu ya mapenzi ya Roho wa Mungu utashindwa kabisa. Akili ya kimwili au akili ambayo inaongozwa na ile iliyo ya mwilini ni ufafanuzi mkubwa wa uasi juu ya Mungu (mst. 7). Kutembea katika matendo ya mwilini sio kumtumaini Kristo kama Mwokozi na sio kumfuata Yeye kama Bwana wa wote. Kutembea kimwili mtindo wa maisha anayeuzingatia mtu mwenyewe. Kutembea katika Roho, kwa kuongozwa. Hii unaweza kujikana mwenyewe kwa mahitaji binafsi na kujihusisha katika hatua za kukua (kukomaa). Katika Wagalatia 5:16-26, “tunda la Roho” linalinganishwa na “kazi ya mwili.”
Huleta kuhesabia haki pale katika sheria ya zamani ilipokua inatufunga. Sheria hii inafanya kazi njema kwa muumini, bali sheria ya zamani inaweza kutambua tu uovu. Uzima huu ni somo la shreia ya Mungu, ambapo mwili hautaweza na hauwezi kuwa adui wa Mungu.
Ilitimilizwa kati ya mmoja ambaye alitembea si kwa mwili, bali kwa Roho. Kama Roho wa Mungu akikaa ndani yako ndipo uzima wake utakamilika kwako. Usijaribu kumtumikia Mungu katika hali ya mwilini, bali unaye Roho wa Kristo atakye kuvuvia na kuhakikishia uzima. Huu uzima si wako mwenyewe, bali ni uzima wa Kristo (Gal.2:20). Huu uzima haudaiwi kwenye mwili, bali kwa kumtumikia Mungu na kumtii Yeye (mst. 12). Huu uzima ulitimilika kwa kupoteza matendo ya mwili (mst. 13).
Walio katika Kristo wanafanya vitu vya tofauti vyotye viwili kutenda na kufikiri. Tutembee kwa kufuata Roho wa Mungu. Roho wa Mungu atatuongoza kwenye uzima, bali mwili utatuongoza kwenye kifo na uharibifu.
Tunaweza kuona kazi muhimu ya matendo mema katika mstari wa 10 hadi wa 13.
Kwa sababu ya dhambi, miili yenu inahesabiwa kufa, bali kwa sababu ya haki roho yako inahesabiwa uzima!
Roho Mtakatifu alimfufua Yesu kutoka wafu. Mwili wa kufa unayo hesabiwa kufa utafanywa hai kwa Roho Mtakatifu.
Je, sisi sote ni watoto wa Mungu? Watu wote ni viumbe wa Mungu, bali wale tu waliozaliwa mara ya pili ndio watoto wa Mungu. (Yoh. 1:12, 13; Gal. 3:26; Col. 1:16).
Muumini ana vitu vikuu vya kuangalia mbele kwa Mungu. Mungu amefanya mambo makuu na atafanya kwa waumini na bado ametupa ukombozi tulio usubiri kwa uvumilivu katika tumaini au imani! Kitu gani muumini anaweza kukiangalia mbele?
Muumini atapokea marupurupu na urithi wa mwana kwa sababu atashirikishwa katika uhusiano pamoja na Baba.
Majaribu huhakikisha sifa ya kweli ya Mkristo. Ingawa kuteswa sio kutukuzwa, Paulo ameleta uangalifu wa kutukuzwa kwetu. Mkristo ana tumaini katika mateso, kwa kuteswa, pia tutatawala. Kristo ni mfano wetu wa mateso (I Petr. 2:21; Waebr. 2:10; 5:8-9; I Petr. 4:1; Yak. 5:10).
Mungu ana mpango mkubwa na Tumaini lililo liweka mbele kwa uumaji. Ni utumwa kwasababu dhambi iko ulimwenguni, bali kule tutakuwa tumefunguliwa!
Roho Mtakatifu ni msaidizi wetu wa Kiungu.
Waeb. 7:25; I Yoh. 2:1; I Tim. 2:5
Mungu huangalia utoaji wa huduma kwa watu wake (walioitwa). Hawa “walioitwa” sio tu kama wamealikwa, bali wameteuliwa. Hapa “kuitwa” ni alama ya kuchagua neema ya Mungu. Kama Mungu alivyo na uhuru, kama Mungu alivyo na kusud, atakuja kutuchukua. Kufanana kwa sura ya Mwana wake ni kusudi kubwa katika maisha ya Mkristo (mst. 29).
Mwisho wa sura unahusu tumaini la Mkristo, ambaye ni “Mungu akiwa upande wetu ni nani atakayesimama ketu.” Pia inahusiana na wazo sisi ni zaidi ya kushinda na hayo yote yanafanya kazi pamoja kwa wema. Tunaenda kuteswa kwa njia ya kutufundisha azimio.
Vifungu viwili ya vya siri ya maisha ya Mkristo yanaelezwa kwa misemo miwili katika mstari wa 1 na mstari wa 10: “Kwa Yesu Kristo” na “kama Kristo akiwa ndani yako.” Mapenzi ya Kristo ni kuishi ndani ya Kristo na maisha ya kumpendeza Mungu. Roho Mtakatifu hukaa ndani yetu, akituongeza nguvu za kuishi kama vile uzima.
Kumbuka muundo wa Warumi?
Warumi 9 mwanzoni mwa mgawanyo wa pili kati ya migawanyo mitatu ya kitabu cha Warumi. Sura ya 8 imehitimishwa na Mgawanyo wa kwanza ambao ni kimsingi wa kimafundisho na sura ya tisa imeanza na mgawanyo wa pili ambao ni mpango ukweli mkubwa.
Kwa ujumla, Mpango ukweli ni njia ya kuamuru vitu—utawala, muundo na usimamizi. Katika elimu juu ya Mungu mpango ukweli ni utawala wa kimungu wa kipindi cha wakati. Mpango ukweli ni njia ya Mungu kuchagua kushughulika na ubinadamu (au sehemu yake) kwa ajili ya kipindi cha wakati.
Dhamira ya mgawanyo wa huu wa pili ni wakimpango ukweli kuhusiana na waisraeli hasahasa jinsi Mungu alivyoshughulika na atashughulika na wa iraeli. Utawala na haki ya Mungu imeonyeshwa katika mistari hii pamoja na shughuli zake na waisrael na hasahasa na jamii ya wanadamu kwa ujumla.
Warumi sura ya tisa inaongelea kuhusu masikitiko ya Paulo kwa ajili ya wayahudi. Tunapatakuwa sio wazao wote wa Ibrahimu walikuwa wana wa ahadi.
Masikitiko yake kwa waliopotea ilikuwa unyofu na uvuvio wa Kimungu.
Paulo aliubeba mzigo! Masikitiko yake yalikuwa mkazo - uzito mkubwa wa kuendelea, kujitoa dhabihu - binafisi.
Paulo alipotia uzito mkubwa kwa kuisikitikia hali ya Waisrael kwa ujumla. Paulo akajikuta mahali ambapo angekuwa na hiari ya kushitakiwa kwa ajili ya Kristo kwamba ndugu zake wange patikana katika Kristo. Hili ni tangazo dogo la kibinafsi, bali tamko hatahivyo halikuwezekana. Nuru ya wenye dhambi katika giza lao ni kuhesabiwa haki, waliotakaswa, maisha matakatifu ya waamini kwamba wanatembea kwa kudumu katika Kristo na wokovu wao wenyewe uko katika Kristo tu. Tamko la Paulo ni nukuu ya Musa katika Kut. 32:32, 33.
Paulo anamasikitiko makuu kwa ajili ya kutokuamini kwa Israel. Kutokuamini hasahasa kutokuwa na moyo kama walivyokumbushwa katika kutokuamini kwao na kutharau urithi wao mkuu. Paulo anatoa urithi wa Wayahudi kama kuwa na sehemu ya nane. Kwa mafungamana ya wayahudi:
Kristo ni mwamba wa kujikwaa kwa Wayahudi (Gal. 5:6; Yoh. 14:15; 1 Pet. 2:7-8)
Paulo anaweka wazi kwamba lengo lake na shauku yake nikwamba Waisrael waokolewe (War. 9:1-5; 11:26; 10:1). Shauku ya Mungu ni kwamba wenye dhambi wote waokolewe (1 Tim. 2:4; 2 Pet. 3:9; Ezekiel 18:23; Mat. 23:37). Paulo ni mwenye haki katika shauku yake na sio kwamba anapingana ufahamu na mapenzi ya Mungu.
Wengi wa waisrael wamekosea lengo. Kristo ni ukamilifu wa sheria, lakini waisrael wamejikwa kwake kama kwenye jiwe na kjishikisha kwe sheria na dini. Wanadhani wao ni wana wa Mungu kwasababu wao ni wana wa Ibrahimu na Isaka na kwamba wao ndio sheria ilifunuliwa kwa ajili yao.
Sababu ambayo wayahudi kama taifa walimkataa masiha (Kristo) inaibua swali kwamba “je neno la Mungu lilishindwa?” “Je Mungu alishindwa kutimiza ahadi zake?” ni jinsi gani Paulo anajibu maswali haya? Katika fungu la misitari hii Paulo anaujasiri kwamba kukataa injili kwa waisrael sio kitu Mungu anaweza kupandikiza tena!
Mwiisraeli wa kweli ni mteule, sio kwa mbegu ya asili. Tunaona mpango wa Mungu ambao haujafungwa. Sio kila mtu ambaye hajazaliwa katika taifa la Israel ametengwa na Israel ya kiroho. Wana waisraeli ni wale tu wa kimwili, bali wana wa ahadi ni wana wa Mungu. (Yoh. 3:6 “walio zaliwa kwa Roho”). Kanisa la Agano jipya lina rejelewa kama israeli wa Mungu (Gal. 6:16) kwasababu ya imani yao kwa Mungu na mwanae, Yesu kristo na sio kwasababu ya ukoo wao (10:1-4).
Uteuzi umetajwa katika mistari kumi na moja. Uteuzi na nadharia sio tendo lisilo la haki la Mungu anaweza kumhesabia haki yeye atakaye na kumuhukumu atakaye. Matendo yote mema haya wezi kuwafanya wao kuwa watoto wa ahadi, bali hayo mashariti yanategemea Mungu kuonyesha huruma.
Ni muhimu kufahamu kutoka maandiko jinsi gani nadharia au uteuzi unavyo fanya kazi. Nadharia na uteuzi yana msingi juu ya ukiri wa Mungu. Yeye hujua mwisho kutokea mwanzo hujua nani atapokea na nani atakataa kabla hata ya wao kuzaliwa (8:29). Baadhi wamepewa miaka 100 na wengine michache tu. Hii ni jukumu la mwanadamu kuitikia wakati wa huruma ya Mungu kumgeukia haiwezi kutokea kwa muonekano wa haraka wa mtu, bali ni lazima avutwe na Baba (Yoh. 6:44).
Utawala wa Mungu umeelezwaje? Mungu ni mtawala na kwahiyo ni Mungu wa haki.
Kumbuka neno tangu zamani. Kwa mchakato mzima wa wokovu imetazamwa kutoka siku iliobarikiwa tutakapoiingia, kwa njia ya huruma ya Mungu, kwenye huo utukufu ambao Mungu aliuelekeza kwetu. Ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ila na watu wa Mataifa pia? (2 Tim. 2:20-21; 1 Pet. 5:8; Mat. 25:1-10; Gal. 5:4)
Katika mstari ya 25 Paulo, anachukua kutoka nabii Hosea (2:23) kifungu ambacho hasahasa kiliongelea Waisrael, bali hakupatta utimilifu kwa waisrael bali zaidi ya hapo inaonekana kutimilizwa kwa mataifa kupokea injli. Sentensi katika sehemu ya mwisho ya msitari huu ni za mkato sana, na zinajieleza kwa kuendelea; zikiacha yale maneno yaliyotumiwa na Watafasiri: nitasema kwa watu ambao HAWAKUWA WATU WANGU, NINYI NI WATU WANGU na wao watasema, MUNGU WETU (1 Pet. 2:9-10).
Katika mstari ya 26, tunaona watu wa mataifa. Neema ya kwanza ya Mungu imewapata wale ambao mara ya kwanza waliitwa “mbwa” (Mat. 15:26) na kuwapa wao wito “waliitwa kuwa wana Mungu aliye hai.”
Katika mstari ya 27 mtume ananukuu na nabii mwingine, Isaiah, kuhusiana na mabaki (Isa. 10:22).
Njia za Mungu sio zetu. Yeye husubiri - na huchukuliana - na yeye ni mkimya - kisha kwa ghafula huweka kusudi lililo kusudiwa la milele.
Mstari 29 umenukuliwa toka Isaya 1:9 unaonyesha kuwa kama Mungu asingalifupisha kwa neema yake, wote wangekuwa kama Sodoma na Gomora (2 Wath 2:7).
Mataifa hawafuati haki (haki kwa sheria), hupatikana kwa imani. Imani imetofautishwa katika kifungu kwa njia hii: Kutafuta haki kwa shika sheria dhidi ya kutafuta haki kwa njia imani katika Kristo Yesu.
Israeli alifuatasheria ya haki, lakini hakujipatia (hangeweza kuitunza sheria). Israeli anafuata sheria, lakini alijikwa njiani.
Israeli hakutafuta kwa imani.
Walijikwaa kwenye mwamba uchukizao. Walijikwaa kwa Yesu. KUMBUKA: Njia pekee ya kuwa na Yesu katika maisha yako ni kumwamini. Vinginevyo yeye ni “mwamba uchukizao.” Alichukiza viongozi wa Israeli kwa kukemea dhambi.
Ni ujumbe gani wa injili uliofunuliwa kwa wote? “Na yeyote aminiye hata aibika.” Huruma Mungu imeonyeshwa kwa kazi zake kwa wayahudi na wamataifa. Unyenyekevu na uchaji ni misimamo maalum kwa ajili yao wote ambao wanaipokea huruma na wema wa Mungu. Iwe mtu ni myahudi au wamataifa, wokovu wake hutegemea zaidi au kidogo kuliko vile anavyofikiri na kufanya pamoja na Yesu. Kujishusha chini ya njia ya Mungu kwaq ukiri binafsi wa Yesu kama Bwana mfufuka, na kumleta mwanadamu katika “haki na kusimama pamoja na Mungu.”
Injili ni kwa ajili ya Wayahudi (War. 1:16; 2:9-10. Wayahudi wengi walikataa Injili (Mdo. 2:22-23). Mateso ya kwanza ya wakristo yaliandaliwa na serikali ya kirumi chini ya utawala Nero mnamo 64 AD baada ya moto mkuu wa Rumi. Kwa hiyo mateso ya kwanza ya wakristo kwa ukubwa yalitokea kwa Wayahudi (Mdo. 9:1-2).
Mafarisayo: Maagizo madogomadogo yaliongezwa katika sheria (Mdo. 23:6; 26:5; Fil. 3:5-6). Paulo hadharau juhudi zao. Anashuhudia kwenye ari yao “kwa Mungu.”
Walikuwa na ari ya Mungu, lakini walipoteza ukweli wa muhimu: Haki ya Mungu ambayo ni kwa imani. Na lengo la imani hii ni Yesu Kristo mwana pekee wa Mungu ni mwisho wa sheria kwa njia ya Imani. Imani hii huja kwa neno la Mungu haihitaji mpaka ufike mbinguni au jehanamu kwanza, bali ni sasa hivi.
Soma Isaya 65:1-10. Mungu atuma mhubiri -> mhubiri ahubiri -> wasikiaji wanasikia -> wasikiaji wanaamini -> muumini analiita jina la Bwana -> Bwana ana mwokoa. KUTOKUUNGANIKA kuko wapi? “Hawaja itii injili au kuisikiliza.”
Wasikiaji walikataa kuamini. TUNAJUKUMU KATIKA MPANGO WA MUNGU KWA AJILI YA UKOMBOZI. Mungu anawatumia wa mataifa kuwaachokoza Wayahudi kwenye wivu (10:19).
Ukataaji ni KUTOKUAMINI kwa wayahudi (Mdo. 14:2; Ufu. 21:8).
“Kwa kukataa injili, na kwa hasira yao katika kuhubiriwa injili kwa mataifa, wayahudi walipata kuwa maadui wa Mungu.
—Matthew Henry
Rehema ya Mungu (Zab. 13:5; 89:2; Yak. 5:11).
Dini inayostahili kuabudiwa kwa hekima, furaha, na haki ya Mungu.
—Matthew Henry
Warumi sura ya 12-16 kamilisha mwisho wa sehemu ya kitabu hiki. Hii sehemu ni ya vitendo zaidi katika maelezo yake. Tunaona Haki ya Mungu inatumika katika maisha ya kila siku ya Muumini.
Warumi sura ya kumi na mbili inahusiana na majukumu ya wakristo, ambapo mwishowe inapelekea maisha ya kushindwa. Kanisa linafananishwa na mwili wa binadamu. Lazima kuwepo na umoja kwenye mwili, kama hakuna umoja, mwili hautafanya kazi vizuri. Sura hii inahusiana na majukumu mbali mbali ya kanisa. Hii sura inahitimisha na roho ya mkristo. Hatupaswi kushinda kwa mabaya bali kushinda kwa mema.
Maneno yaliyotumika mara nyingi hupoteza thamani yake kwetu kwa kutumika mara nyingi. Hebu tuangalie kwa karibu kwenye misamiati ya mistari miwili ya mwanzo ambapo tunaweza kupata uelewa zaidi:
Hii ni ombi kuu la Paulo kwa ajili ya utakaso binafsi kwa Mungu. Paulo anafundisha kwamba kila muumini anapaswa kutamani mapenzi makamilifu ya Mungu. Maelekezo yanatolewa kwaajili muumini kuyafuata.
Katika mstari wa 1 anatuambia kutoa miili yenu, “hii inamaanisha kutoa sio nafsi tu,” bali na miili yetu vile vile. Ni sadaka ya hiari, na kutakugharimu kitu fulani. Ni dhabihu iliohai. Tunapswa kujipeleka wenyewe kwa Mungu tukiwa hai!
Mungu ametoa sana kwa watu wake. ametoa neema, yeye ametoa kwa kila mtu kipimo cha imani, amefanya mwili moja katika Kristo, naye ametoa karama za unabii, huduma na ufundishaji.
Watu wa Mungu wanapaswa kutenda kwa usahihi tunapaswa kufikiri kwa busara, kutoa kwa urahisi, kutawala kwa akili, kuonyesha huruma na uchangamfu, upendo usio na mfarakano, chuki ambayo ni uovu, kuambatana na lililojema, kuwa mwema kwa upendo, kuonyesha upendo wa kidugu, kupendana, sio wa kujipachika katika shughuli nyingi, kuwa mwenye juhudi katika Roho, mtumikie bwana, furahahi katika tumaini, kuwa mvumilivu katika dhiki, kuendelea katika maombi, kugawia mahitaji ya lazima kwa watakatifu, kutoa kwa ukarimu, kuwabariki wale wanao kutesa, kufurahi na wanao furahi kulia na wanao lia, kuwa na nia inayo fanana.
Muumini na mtindo wake wa maisha lazima yawe tofauti zaidi kuliko ulimwengu. Ulimwengu unatumia kanuni za Mungu kwa ajili ya mafanikio yao katika kujipatia mapato. Tuzitumie kanuni za Mungu kwa ajili ya mafanikio sio kwa ajili yetu bali kwa ajili yake na ufalme wake. Kwanini nataka kuwa mkristo mwenye mafaniko?mafanikio ni kujifunza jinsi ya kuongoza wengine kwa Kristo. Maisha yetu yawe mfano wa Kristo.
Kazi ya Roho mtakatifu kwanza anza na ufahamu, unaobebwa kwenye mapenzi, upendo na mazungumzo, hadi kuwa na badiliko la mtu mzima kwenda kuwa mfano wa Mungu, katika ujuzi, haki, na utakatifu wa kweli. Kwa wale wamchao Mungu tunapaswa kujitoa kwa Mungu.
—Maoni ya Matayo Henery
Kufanywa upya kwa ufahamu hutokea kwa Neno la Mungu (Zab. 119:9, 105). Ni kazi ya Roho. Ufahamau mzima lazima uje chini ya uongozi wa Roho (Waefeso 5:17-20—17). Ufahamu uliofanywa upya ni ufahamu wa Kristo. Sio kwamba ni ufahamu tofauti au mwingine, bali ni kazi ya Mungu ndani inayo zalisha ufahamu wa Kristo (Waflp. 2:5; 1 Cor. 2:14-16; Luka 19:10; 2 Tim. 1:7; Yohn 8:50).
Tu mwili mmoja katika Kristo, wenye karama mbali mbali. Kila moja ni kiungo cha mwenzake. Mtu anapo miliki karama atapaswa kuitumiaje? Karama mbali mbali hutolewa na Roho. Kazi za karama ni unabii, huduma, kufundisha na kutia moyo, nk. Umiliki wa karama sio bila matumizi. Ni mazoezi mazima ya karama, wakati imetolewa na kusihiwa na mitume. Karama zimetolewa moja kwa moja na Roho. Imani ni ya lazima kwa kupokea na kutumia hizi karama.
Kutokuiga humaanisha “kutochukua wazo la mtu, hisia, au tabia; kujifanya.” Upendo usioshindwa umeshuhudiwa kwa wema (2 Wakor 6:6).
Zaburi 34:14—Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.
“Uovu” ni kile kinacho umiza, kuzuia uzalianaji katika asili, ya shetani, anasa au ubaya. Tunahitaji kukimbia uovu na kukimbilia mema. Hii sio hofu ya uovu kama ilivyo kwa ushirikina,lakini ni utakaso au mgawanyiko wa mwenendo wetu na maisha ya mawazo kutoka kwa vitu hivyo ambavyo ni kinyume na utakatifu wa Mungu. Je, tunawezaje "kuchukia" na "kuachana" na uovu? (Zab. 37:27; Is. 1:16)
Kuwa mkristo inajumuisha kila eneo la maisha ya mtu. Nia na mwili hutolewa kwa Mungu kwa kujikabithi kimaadili kama sadaka ya kiroho. Kwa msimamo wake na matendo mbele ya Wakristo wengine yeye ni wakuonyesha ukweli kwamba yeye ni mfuasi na wengine katika mwili wa Kristo. Katika uhusiano wake na mwenye dhambi, yeye hufanya katika upendo na kumwachia Mungu ulipizaji kisasi kwa ajili ya uovu.
Warumi sura ya 13 inaelezea kazi yetu katika amri na sheria, vilevile kazi za kiraia. Ndani yake tunaona kwamba upendo ni utimilifu wa sheria na kwamba hatuhitaji utoaji wowote kwa ajili ya mwili (mst.14).
Kwa kuwa sisi tunapokea ahadi ilioko kwenye Zaburi 47:3 (yeye atawashusha watu chini yetu na mataifa chini ya miguu yetu.) sasa tunaenda kujiunza kwenda kuwa watiifu sisi wenyewe kwa Mungu kwenye mamlaka yake. Hebu tuchunguze “utii wa Mkristo” (utii kwa watawala kama walivyo agizwa na Mungu) katika War sura ya kumi na tatu.
Sura ya 12 husisitiza hitaji letu la kukabithi miili yetu kama dhabihu iliohai, na sura ya 13 inafundisha juu ya umuhimu wa utii kwa wenye mamlaka.
Sehemu ya pili ya mstari wa 2 hutuambia kwamba mamlaka yote hutoka kwa Mungu. Mamlaka yote ni ya Mungu (Zab. 62:10–11; 29:10; Mat. 19:26). Mamlaka ya kidunia lazima yapokee msukumo toka kwa Mungu mtawala (Kol. 1:16–17; Dan. 2:21). Tunainamishwa na Mungu kuwa katika utii wa mamlaka. Amri hii hutoka kwa Mungu.
Kwa kuwa mamlaka yote ni ya Mungu, wakati tunapojitiisha wenyewe kwa watu, kwa uhallisi tunajitiisha wenyewe kwa Mungu. Kuwa kinyume cha Mungu ni kuwa kinyume chetu wenyewe. Hatumuumizi Mungu kadiri tunavyokuwwa sio watii kwa Mungu tunajiumiza wenyewe.
Uasi unagharama kubwa. Hukumu ndio ile ambayo Paulo anaiwasilisha kama gharama ya uasi. Hakuna hofu kwa jambo la watawala wanaoagizwa na Mungu kama wenye hofu kwa ajili ya kazi njema bali kwa maovu. Kuepuka ghadhabu ya upanga wao (War. 12:18; Waebr. 12:2).
Mungu anaagiza mamlaka kwa ajili ya kusudi la kulinda wema na kuadilisha uovu. Mamlaka yamebuniwa kwa ajili ya wema wetu na ulinzi. Pasipo uongozi hapatakuwa na utaratibu na machafuko yaweza kutokea.
Tunapaswa kuwa wa watiifu sio kwa sababu ya kuepuka adhabu, bali pia kwa kuhifadhi dhamiri zetu safi. Kwa Wakristo Mungu anatuagiza kuwa katika unyenyekevu.
Mathayo 22:21—Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
Kanuni inayohusiana na maandiko matakatiu ni ndefu kiasi kwamba “Kaisari” haihitaji zaidi ya kile ambacho Mungu anataka sisi kubakia katika utiifu. Kwa kadiri iwezekanavyo, tunapaswa kuishi kwa amani. Labda miaka kama 4 au 5 kabula paulo hajaandika barua hii kwa Warumi, kulikuwa na amri iliotolewa na serikali ya Kirumi ambayo ilikuwa inazuia wayahudi (kwa kuongezeka, Wakristo) kubakia katika mji wa Rumi. Na haki kwa ajili ya amri hii iliozuia mnongono ulioenea wa Wayahudi waliokuwa waleta matatizo. Paulo haelezei “haki za kiraia” za wayahudi na wakristo katika sura hii, badala yake anasisitiza majukumu yao wenyewe.
Katika mistari ya 6 na 7 tunaona mifano ya utii kwa mamlaka ya kiraia:
Upendo hutimiza sheria. Kujihusisha na upendo ni kuitimiza sheria. Katika Yohana 14:15 Yesu anasema, “Mkinipenda, mtazishika amri zangu.” Muumini yuko katika “uumbaji mpya,” na kuenenda katika madarka ya “juu ya maisha” (Wagal. 6:15–16) sio kwa sheria. Katika kupenda yeye ametimiza sheia ya kiwango cha chini.
Bwana anaahidi kurudi, lakini wakati wakurudi ataikuta imani duniani? (Luk. 18:8)
Kila mwanafunzi wa kikristo, lazima awe na kusudi, au maono, vinginevyo tutashindwa. Hili ni jambo ambalo Kristo atatupa.
Hii sio kazi yetu. Kazi yetu ni kuyafanya mapenzi yake yeye aliye tuita. Ni kuifanya kazi yake (Yoh. 4:34). Ikiwa tumeitwa, tuna kusudi lililo funuliwa katika maisha yetu. Ufunuo huu wa kusudi la Mungu kwa ajili ya maisha yetu hupokelewa kwa maombi.
Kama wahudumu mnahitajiwa kuwaleta wengine kwenye kumjua Kristo; Iliwalitafute neno la Mungu wao wenyewe (mwanamke kisimani aliamini kwa sababu ya kile ambacho neno linasema).
furusa ni haki iliopatikana popote ulipo. Unapokuwa mtiifu na kuwa na hiari kwenye mapenzi ya Mungu, tunakuwa vifaa katika mikono ya Bwana.
Amri za sura hii huelekezwa kwetu leo kama zilivyoelekezwa katika siku za Paulo. Mkristo anapaswa kuchukuliana na kila hali kulingana na Mungu alivyo na kile Mungu afanyacho. Matazamio ya mkristo yameelekezwa kwa mtazamo wa Mungu wa dunia na kusudi la Mungu katika dunia.
Warumi sura ya kumi na nne inaongelea kuhusu jinsi ya kumtendea ndugu mdhaifu. Tunapaswa kuwasaidia wale ambao ni wadhaifu katika imani yao. Tunaona hitaji la kuwa na upendo. Tunapaswa kumishia Mungu, na yote tunayohitaji kwa Mungu. Hatupaswi kuhukumiana, kwa kuwa siku moja kila mmoja atatoa hesabu ya maisha yake mwenyewe.
Kunatofauti katika afya za imani zetu vile vile kunatofauti za maoni (madhaifu na yenye nguvu). Kunamaelekezo yaliyo wazi yaliyotolewa katika maandiko matakatifu:
Lakini pia kuna maoni mengi na ufasiri na matumizi ambayo hujazwa kati ya mistari. Wakristo wengi hugawanyika juu ya mambo kama vile:
Mara nyingi maoni huvuviwa na maandiko matakatifu, lakini tunafanya kujaza sehemu ya kijivu (isio elezwa) maeneo ya maandiko kwa maoni yetu. Tofauti za maoni zisingekuwa sababu za migawanyiko au kisngizio kwa ungomvi.
Kila mtu angekuwa kama mimi?
Uthafu Paulo ameutaja hapa unabeba dhana ya ugonjwa na hali ya kushindwa kuzaa hanithi. Wale walio wadhaifu katika imani wanafanana na kilema anayehitaji kujikokota, kipofu anayehitaji kuongozwa, au mwenye kupooza anayehitaji msaada kwenye mambo ya lazima katika maisha ya kila siku. Magonjwa hukatisha maisha na kuyaondoa kama hayatatibiwa. Huu udhaifu wa imani ni sawa na ugonjwa ambao ni lazima ufahamike na kushughulikiwa kwa neema, lakini pia uwe ni uponyaji ulio hudumiwa. Wadhaifu lazima wasiachwe wapweke, lakini watiwe nguvu (Yak. 5:16).
Katika Wakor wa kwanza sura ya 8 Paulo alipaswa kushughulika na swala lile lile na Kanisa la Wakoritho. Hili linaweza kusikika kama kitu kisicho na maana na sio cha kidini na mabishano kwa mkristo wa sasa, lakini Biblia ya maoni ya Layman inatupatia mwanga kwenye ubishi huu:
Ilikuwa ni aina tofauti ya swali la kidini katika utawala wa kirumi. Uhakika ni katika soko la kirumi ungeweza kwa ugumu kupata nyama nzuri au ya kuokwa au aina yeyote ya nyama ambayo haikutokana na wanyama waliochinjwa ndani hekalu. Mnyama angeweza kuchinjwa kwa ajili ya sadaka ya kutekezwa;kisha kuhani (amabo walikuwa hawana idadi ingawa walikuwepo lakini haingwezekana kula wanyama wote walioletwa kama sadaka) wangeweza kuwauza kwa reja reja kwenye vituo. Hii ilikuwa chanzo kikuu cha nyama katika masoko, Mkristo mnunuzi angekumbana na shida: katika kununua na kuila nyama hii, nifanye au nisitoe msaada kwa ibada ya kipagani?
Roho ya sheria haiulizi “uliikumbuka siku?” bali huuliza kwamba je ulifanya kama kwa Bwana?" waliabudu kwa siku kadhaa, na walikuwa wanaweka umuhimu juu ya siku na sio kwa Kristo.
Msitari wa sita kwa wazi unaelezea pande zote mbili za hoja ya kumjua Bwana.
Ni nini tunayodhani kuwafanyia wengine:
Ni baraka zaidi kuwa na uhuru mbele ya Mungu ambayo hatutumii udhaifu wa ndugu, zaidi ya kusisitiza uhuru, ingawa umetolewa kwa utofauti.
Waamini ni wakukaribishana wao kwa wao, kama Kristo alivyo wapokea mataifa—kwa utukufu wa Mungu. Sehemu ya kwanza ya sura hii inaelezea mahusiano ya Kikristo, Kristo akiwa kama mfano wao mkamilifu. Ujumbe binafsi wa Paulo kwa Warumi unaanza na katika msitari wa 14. Huduma ya Paulo ilikuwa kwa wote kwa wale waliokuwa ndani (wayahudi ambao makuu ya Mungu yalifanyika kwao na kwa wale ambao haikufanyika (wa mataifa). Kazi ya umoja kataika mwili wa Kristo ni kazi ya MUngu.
Kuna tofauti nyingi za kidini na kimila kati ya wayahudi na wamataifa kwa kufunguliwa injili kwa mataifa kulikuwa na ugumu mwingi wa kushinda. Paulo anaonya kwa ushupavu, tunatakiwa kufanya kazi ili kuwapokea wamataifa kama Mungu alivyo wapokea. Kiwango cha juu na kutawala kwa kile ambacho tabia zetu hupimwa “kama kristo alivyo tupokea sisi kwenye utukufu wa Mungu” (mst. 7).
Kuwa myahudi kwa shaka, makanisa ya kwanza yange jisikia “kuwa ya kiyahudi”(michanganyiko ya mila na ushawishi). Kulikuwa na ufukuzwaji kwa mara ya kwanza kutoka Roma kwa wayahudi wote na ni mageuzi ya kiasili na kimila yaliyo tokea katika makanisa ya kirumi. Mwishowe, Wayahudi walirudi katika mji wa Roma kupata vitu tofauti zaidi ya walivyokuwa wameacha. Ilikuepuka mgawanyiko, Kanisa la kwanza lilikuwa linafanya kazi kwa pamoja ilikushinda tofauti zao za kimila kwa kujifunza vile vitu ambavyo “vinahitaji sana” (Matendo 15:28; Waefeso 4:3, 13).
Warumi sura ya kumi tano inaongelea kuishi maisha yasiyo ya kichoyo. Wenye nguvu wanapaswa kuwasaidia wadhaifu. Tunapaswa kuishi sio kujipendeza wenyewe bali kumpendeza Mungu, kuwatanguliza wengine mbele yetu. Sura hii inaishia na safari za Paulo.
Sura ya kumi na tano ya Warumi inahisia nzito ya hitimisho. Kama ulivyo mtindo wa Paulo katika kitabu hiki, anarudia mawazo ambayo aliyawasilisha lakini ni kwa mwelekeo zaidi na kibinafsi. Anatoa maelezo ya maelekezo maelezo yaliyo fuata kwa wasomaji wake:
Kwa nini mkristo ni lazima kuhusika na wengine badala yake mwenyewe? Tunapaswa kumtumia Kristo kama mfano wetu, “hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, kuhusika kwake ilikuwa ni kwa wengine alijionyesha kwa upendo, mafundisho yake na uponyaji wake.”
Tunaweza kuwa na faraja wakati mahitaji kwa kuyasoma maandiko. Tunaweza pia kuendelea mbele kwa tumaini.
Tunaswa kuunganika katika nia moja na kwa roho inayomtukuza Mungu ambaye ni lengo letu la maisha.
Maoni ya Paulo yalikuwa nini kuhusu wakristo wa Rumi?
Ijapokuwa Paulo hakuwahi kuwa Rumi, alijuwa na kufarijika kwa imani yao (1:8).
Kuna vitu vingi vya kutia moyo Paulo anaweza kusema na ameshasema (1:8), lakini wote tunakitu cha kufanya.
Katika hatari inaonekana ya kutotambuliwa kwa mfano wao na imani, Paulo kama mhudumu mwaminifu wa changamoto za injili ujasir wa kanisa na vitu vya lazima.
Je, Paulo anajirejea mwenyewe kama nini? Kama, mhudumu wa Yesu Kristo kwa mataifa. Akihubiri neno katika nguvu za Roho. Kwa ishara na maajabu kama uthibitisho. Utambulisho wa Paulo ulifunika wito wake. Paulo aliweka kipau mbele kwa wito wake na kuchelewesha matakwa na malengo binafsi. Sio kwamba kile anafanya hakina mzigo kwa ndugu zake, bali kile alichonacho ni wito ulikuwa unatangulia.
Kadiri Paulo alivyokuwa na ujasiri anaongea, haogopi kusema lakini kwa kile ambacho Kristo amemwezesha:
Kifungu “hizi nyakati nyingi” inaonyesha jinsi ani wakisto wa Roma kwa kuendelea walivyokuwa katika moyo wake na shauku zake. Kifungu “muda mrefu unaokuja” inaonyesha kwamba yeye alikuwa shauku kubwa ya kuwatembelea watu.
Paulo anaelezea tena shauku yake na kusudi lake la kutelea kanisa la Roma na ratiba yake. Alikuwa lazima kwanza aende Sipania na kukusanya sadaka kwa ajili ya watakatifu wa Yerusalemu. Yeye angeweza kuzileta Yerusalemu baada kile alichokusudia kutembelea Roma. Kwa jinsi gani wakristo wa Makedonia na Akaya walivyohusika na maskini miongoni wa wakristo walioko Yerusalemu? Walichangia kwa ajili ya maskini. Paulo mwenyewe pamoja na ndugu wengine walichukua hizi sadaka na kuzipeleka Yerusalemu, kupokea kwa mtu kile ambacho ni kanuni ya kiroho Paulo anawafundisha warumi kwa kuhusianisha hizi habari? Lilikuwa ni tendo la upendo juu ya sehemu ya watakatifu wa mataifa. Ilikuwa ni utimilizo wa maneno ya Bwana katika Yoh. 13:17, 35.
Katika mstari wa 30 kwa mara ya kwanza tunaona utatu:
“Mungu wa amani awe nanyi nyote,” inaonyesha kwa jinsi gani moyo wa mtume ulikuwa umejawa na amani na kujawa mapensi ya Mungu! Inaonyesha pia upendo unaofurika kwa ajili ya watakatifu (mara mbili katika sura hii Paulo anaomba kwa ajili ya kanisa la Rumi. Angalia misitari ya 13 na 33). Kusudi na nguvu ilio nyuma ya umoja wa wakristo ni mfano wa upendo wa Kristo na huduma na dhabihu. Kuwa na msisimko kama huo miongoni mwa wakristo, tunahitaji kuomba kama Paulo alivyofanya uwezeshaji wa Bwana. Maana ya Paulo ya agizo kuu haikumfanya kuwa wakutegemewa na wakristo wenzake.
Inavutia kukumbuka kwamba kuna kiasi cha utata juu ya kitabu hiki cha Warumi 15:14–16:27. Swali ni kwamba “wapi warumi waliishia kiasili? je ni kwenye 15:13 kwa asili ni katika mstari wa mwisho wa Warumi?” Maandishi mengi ya zamani hayaingizi kifungu (15:14–16:27), na kwa wakati huo huo kuna mengine yanaingiza kwa njia moja au kwa njia nyingine. Baadhi huweka yaliyoko kwenye sura hii ya kumi na nne mwishoni lakini mengine huweka yote mwishoni mwa sura na mengine huweka mwisho wa kitabu. Hii haichukui msukumo wa kuafikiana na heshima ya kifungu, bali imefafanulilwa kwa mtiririko mzuri. Mtu ana nakili barua na kuwa na shauku ya kuipeleka miongoni mwa makanisa mbalimbali isinge acha nafsi ya mtu yeyote huko katika kanisa la Roma.
Warumi sura ya kumi na sita inatunyesha upande binafsi wa Paulo kama anavyotuma salamu kwa waamini wanoishi Rumi. Anaongea kama mtu anayeongea na marafiki zake na sio kama kiongozi au mchungaji. Hii sura ya kumi sita mara nyingi huupuziwa na wengi. Ni kwa wale walio mbali zaidi, kwa siri, na umaaalumu wa barua ya Paulo yenye salamu (na ya pili ni Wakolosai 4). Hakuna atakaye athubutu kupoteza umwagikaji waajabu wa moyo wa mitume wetu kwa, watakatifu ambao aliwapenda sana, ambao ni kanisa la Mungu.
Roho ya kifungu hiki ni ya kipekee na maalumu unapofikiria kwamba Paulo hakukuta kanisa huko Rumi na hata alikuwa bado hajawahi kutembelea huko (barua hii inafanana na ile ya Wakolosai)! Licha ya kwamba Paulo anawataja kwa majina watu 26 katika kanisa hilo. Kila jina limeorodheshwa katika alama za Paulo za kufunga bila shaka alikuwa na historia yao ya kutia moyo, upendo na ibada kwa Bwana Yesu Kristo. Wengine zaidi ya majina yao, Paulo anawatambua hawa watu kama:
[KUMBUKA: nukuu kadhaa katika sehemu zimechukuliwa kutoka fafanuzi za Alexander Maclaren ya maandiko matakatifu“. Alexander MacClaren (February 11, 1826 - May 5, 1910) alikuwa mvuka salama na mhudumu wa injili kwa takribani miaka 65 aliyefanya kazi bila kuchoka katika kuhubiri na kuandika kuhusiana na maandiko matakatifu. Fafanuzi za MacClaren za maandiko matakatifu ni mkusanytiko wa zaidi ya hotuba 1,500]
Lakini kama tutahesabu kutokuwa na maadili kwingi kuliko jificha kwa wakrinto, tutadhani labda ilikuwa hapa kulikuwa mji, wenye maji mengi, ilikuwa kama bandari nyingi, udongo ambamo wema kwa ulipandwa ilikukuwa, na kanisa lilikuwa na upinzani mwingi ambao walipaswa kupambana. Kuwa mkristo katika Cenchrea inawezekana haikuwa kazi rahisi. —MacClaren
Jina lake kwa wazi alikuwa mwabudu sanamu, na linamwelezea kama Mgriki, na kwa kuzaliwa labda alikuwa mwabudu wa Apolo.
—MacClaren
Hapa ni Paulo myahudi, Fibi mgiriki, na wasomaji wa kirumi wa barua, wote waliungana kwa pamoja katika upendo wa kimungu ambao uliyeyusha mioyo yao, na imani ya kawaida ambayo iliounganisha maisha yao. Orodha ya majina katika sura hii, yanajumuishwa kama wanaume na wanawake wenye uraia mbalimbali, na baadhi ni watumwa kama watu huru.
—MacClaren
Wagalatia 3:28—Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
Kwa ulimwengu ambao Paulo alikuwa anaishi ulikuwa ni wa kigeni, wazo jipya ambalo wanawake wangeshirikisha kwa wanaume katika msisimko yake ya kifahari. Kihistoria udhaifu wa nusu ya wanadamu ni matokeo ya moja kwa moja ya kanuni ya kikristo ambayo wote ni wamoja katika Kristo Yesu. —MacClaren
Paulo anayasalimia makundi 16 ya watu huko Rumi:
Paulo anafuatana na baadhi miongozo ya kichungaji na maelekezo. Anasema na kuyatia “alama.” Hili neno alama humaanisha “kuchukua lengo, kuwa mwangalifu.” Ni neno lile lile lililotumika katika Wafilippo 3:17.
Paulo anamalizia na HALELUYA!