MWAKA WA KWANZA

KITABU CHA KIADA

UTAngulizi WA BIBLIA

Uchunguzi  wa Jumla wa Biblia

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Utangulizi wa Biblia

Uchunguzi wa Jumla wa Biblia

 

 

 

 

Utangulizi 2.

Maelezo ya Kawaida ya Biblia .3

Umoja kamili wa Biblia 16

Uvuvio wa Biblia .20

 Kanoni za Biblia .29

 

 

 

 

Utangulizi

 

 

 

 

 

 

 

 

Utangulizi wa Biblia Takatifu na sababu zinazotufanya tuamini kwamba haina dosari, kosa, ni safi, na ni neno la Mungu lenye msukumo wake ambalo halina mgongano.

 

 

 

 

 

 

 

 

Asilimia kwa daraja la mwaka

 

 

Mungu hakuandika kitabu kingine zaidi ya Biblia. Hakuna ushahidi mwingine wowote wenye maelezo ya kina ya mapenzi ya Mungu na uwezo  wake zaidi ya Biblia. Ni kwa kusoma Biblia peke yake ndio tunaweza kuwa na majibu kuhusu maswali mengi yanayomhusu Mungu.

 

 

Katika Biblia Mungu ameandaa maelezo ya habari za mapenzi yake na kuonyesha upendo wake kwa binadamu. Ufunuo mwingine wowote unapaswa kuoana na kitabu hiki cha ajabu. Ni kiwango cha uhai wote—wa muda mfupi na wa milele!

 

(‘ya katikati’ kuu , kiongozi, dhamira ya msingi – mada, kama ya hotuba.)

 

 

Mwanzoni Agano la Kale liliandikwa kwa Kiebrania (na asilimia ndogo kwa Kiarabu.) Agano Jipya liliandikwa kwa lugha ya Kigiriki. Toleo la Kingereza la Mfalme Yakobo ni tafsiri inayotokana na lugha hizi asilia. ‘Kutafsiri’ maana yake ni kubadilisha kutoka lugha moja kwenda katika lugha nyingine.

 

Biblia ni kitabu kimoja, historia moja, na simulizi moja  HISTORIA YAKE [Historia ya Mungu]! Tunaiita Biblia TAKATIFU kwa sababu ni Neno la Mungu na siyo hadithi tu ya wanadamu. Neno TAKATIFU maana yake tukufu, safi, isiyo na lawama, au ya kidini, iliyotengwa. Biblia ni kitabu cha Kimungu ingawaje Mungu aliwatumia watu kuueleza ukweli wake Mtakatifu. Watu watakatifu (asili yake binadamu) waliandika kama walivyo himizwa na Roho Mtakatifu (Utukufu wa asili ya Mungu). Kwa kuwa ni Neno la Mungu hatuwezi tukatimiza wazo kwa kitabu au taarifa moja ya Biblia.

 

Biblia inavyo vitabu 66, 39 katika Agano la Kale na 27 katika Agano Jipya. Utukufu wa Kimungu umefunuliwa katika Biblia kwa utaratibu kuanzia kitabu cha Mwanzo hadi mwisho wake katika Kitabu cha Ufunuo. Mwanzo ni kitabu kinachoonyesha asili; Ufunuo ni kitahu kinachohusu mwishoni. Vitabu vya Biblia vya katikati ni maneno ya Mungu ya uamsho kutoka katika ulimwengu ulioharibika. Kila kitabu cha Biblia kinao ujumbe wake, hata hivyo kitabu kizima kinakuwa na ujumbe wa wokovu wa mwanadamu ambao unaonekana. Inaweza kusemwa pia kwamba Agano la Kale ni taarifa ya taifa ( Israeli ) na agano jipya ni taarifa za mwanadamu (Yesu)

 

 

 

 

 

 

 

 

Mwanzo 5:1- Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu.

 

Zaburi 40:7- Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (katika gombo la chuo nimeandikwa, (Ebr. 10:7)

 

Mathayo 1:1- Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, Mwana wa Ibrahimu.

 

Luka 4:17- Akapewa chuo cha Nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa.

 

 

 

II Wakorinto 3:14 – Ila fikra zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo.

 

II Wakorinto 3:6 – Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa Roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Ufunuo 13:8 – Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana -  Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.

 

Mpango wa Mungu toka mwanzo wa nyakati ni wa Yesu ambaye ni Kondoo wa Mungu kumwaga Damu Yake Takatifu kwa malipo ya ukombozi wetu.

 

 

 

 

Mathayo 5:17 – Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; laa, sikuja kutangua bali kutimiliza.

 

Kristo ndie mtu wa katikati katika Agano Jipya. Kristo ndiye mpatanishi wa Agano Jipya – Ebr. 12:24     

 

 

 

 

 

Yohana 20:31— Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake.

 

 

 Yohana 5:39—Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia.

 

 

Yohana 17:3—Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

 

Yohana 14:23—… mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda …

I Yohana 2:5—Lakini yeye alishikaye Neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika …

Yohana 10:27—Kondo wangu waisikie sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.

Yohana 12:26—Mtu akinitumikia, na anifuate

 

 

 

 Waefeso 5:27—Ili apate kujiletea kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

II Timotheo 3:1—Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

 

 

II Petro 1:19-21—Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi,  ambalo, mkiliangalia, kama taa ing’aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. 20. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. 21. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

 

 

 

I Wakorinto 3:11—Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani,  Yesu Kristo.

 

II Tim. 3:16—Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kuwaonya watu makosa yao, na kuwaongoza, na kuwaadibisha katika haki:

 

 

 

 

Ifuatayo ni orodha ya sehemu muhimu za Biblia na maelezo mafupi kuhusu kilichotokea katika kila sehemu mojawapo. Kujifunza kwa moyo sehemu hizi na kujua kilichotokea katika kila sehemu mojawapo kutakupatia picha nzuri ya Biblia yote.

 

 

 

MAHALI

MAELEZO

ANDIKO

Edeni

Mungu alimuumba mwanadamu na kumweka katika Bustani ya Edeni. Eneo la anguko la mwanadamu

Mwanzo. 2:8

Mlima Ararat

Mahali safina ya Nuhu ilipokuja kusimama baada ya ile gharika.

Mwanzo. 8:1-5

Babeli

Mnara uliojengwa kuifikia mbingu na Mungu akawafanya wanadamu waongee katika lugha tofauti.  Babeli maana yake mkanganyiko

Mwanzo. 10:10; 11:4

Uri wa Wakaldayo

Mahali abrahamu alipoambiwa mwanzoni aende Kanaani. Nchi ambayo baadaye ilikuja kuitwa Babeli.

Nehemia. 9:7

Kanani

Nchi ya ahadi ambayo walimoishi Abrahamu, Isaka na Yakobo. Yoshua aliiteka na kugawia kila kabila sehemu.

Mwanzo. 12:5

Misri

Nchi Yusufu alikouzwa kuwa mtumwa.  Israeli ikadumu utumwani miaka 400. Musa aliitoa Israeli kutoka Misri.

Mwanzo. 12:10

Mlima Sinai

Mahali Musa alipoona kichaka kinachowaka moto na baadaye akapokea sheria na agano.

Kutoka. 19:11

Nyikani

Watoto wa Israeli walihangaika jangwani kwa miaka 40 kwa kutoamini kwao.

Matendo 7:42

Syria

Mateka wa Israeli walipelekwa Syria.

2 Fal. 18:11

Babeli

Mateka wa Yuda walipelekwa Babeli. Danieli alikuwa mmoja wao

Danieli 1:1

 

 

MAHALI

MAELEZO

ANDIKO

Betlehemu

Mahali pa asili—Kuzaliwa Kristo katika hori.

Luka 2:7

Galilaya

Palistina iligawanywa katika mikoa mitatu, Yudea, Samaria, na Galilaya, ambayo ilijumuisha eneo lote la kaskazini la nchi (Mdo. 9:31), ambao ndio mkubwa zaidi.

Luka 4:14

Getsemane

Mahali pa Kristo pa sala na aliposalitiwa na Yuda.

Mat. 26:39

Golgota

Mahali Kristo aliposulubiwa. “Mahali pa fuvu la kichwa.”

Marko 15:22-28

Yerusalemu

Huitwa pia: Salemu, Arieli, Yebusi, "Mji wa Mungu,"  "mji mtakatifu;" wakati fulani "Mji wa Yuda" Mahali lilipozaliwa kanisa la Agano Jipya.

Mdo 1:8 (2:25,28)

Samaria

Samaria mkoa ulioko katikati ya Palestina lakini hauchukuliwi kama nchi takatifu. Umbali kati ya Samaria na Israeli ambayo ni mji mikuu ya falme mbili ni maili 35 tu katika mstari ulionyooka.

Yoh. 4:1-5

 

Mungu— Biblia inatueleza kwamba Mungu ni roho (Yohana 4:24).  Mungu ni Roho nao wamuabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli (Strong) Mungu ni zaidi ya mtendaji katika Biblia; Mungu ni chimbuko la kila kiumbe.  Biblia inamfunua Mungu kwa mwanadamu.

Shetani—Neno shetani maana yake anayeshtaki. Yeye ndiye anayeshtaki kati ya wanaoamini. –  Ufunuo 12:10. Shetani huitwa pia muovu.  Mungu hakumuumba muovu.  Mungu alimuumba malaika Lusiferi ambaye alianguka kwa sababu ya dhambi akawa muovu. – Isaya. 14:12, Lk.10:18.

 Adamu— Mungu alimuumba Adamu, mwanadamu wa kwanza, akamuweka katika Bustani ya Edeni.  Ni yeye ndiye aliyeingiza dhambi katika jamii ya wanadamu. – Rum. 5:12

Eva—Mungu alimuumba Eva, mwanamke wa kwanza, kutokana na ubavu mmoja wa Adamu. – Mwanzo 2:21-22

Kaini— Mwanaye Adamu wa kwanza. Alikuwa mkulimaAlimuua nduguye Abeli na kuwa muuaji wa kwanza. – Mwa. 4;1

Abeli—mwanaye Adamu wa pili aliyeuawa na Kaini. Alikuwa mchungaji. Mwa. 4:2

Seti—Mwanae Adamu wa tatu. -  Mwa. 5:3

Nuhu—Alijenga safina kulinda uhai katika dunia. Mwa. 6:13-22

Abram—Mungu alimwita Abram aondoke nyumbani na kwenda katika nchi isiyojulikana ambako Mungu atamfanya baba wa taifa kubwa, ndio historia ya Wayahudi ikaanza. Mwa. 12:1-3 Mungu alibadili jina lake kutoka Abram Baba Mkubwa kuwa Abrahamu  Baba wa Umati. Mwa. 17:5

Isaka—Mwanaye Abrahamu wa agano aliyempata kwa ahadi uzeeni. Mwa. 17:19

Yakobo—Jina lake lilibadilishwa na Mungu likawa Israeli. Wanae 12 ndio waliounda makabila ya taifa la Israeli. Mwa. 32:28

Yusufu— Mwanaye Yakobo ambaye aliuzwa utumwani Misri.  Mungu alimpandisha cheo hadi nafasi ya pili katika ufalume na akamtumia kuilinda Misri na Israeli.  Yakobo na familia yake walihamia Gosheni wilaya iliyoko Misri. Mwa. 37:36,42:1-3.

Farao—Cheo cha mtawala wa Misri. Watoto wa Israeli walikuwa utumwani Misri kwa miaka 400. Mungu aliufanya moyo wa Farao aliyetawala wakati wa Kutoka kuwa mgumu na akawaondoa Waisraeli kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu. Kut. 1:11-14, 6:1

Musa— Mungu alimwinua Musa kwenda kuwatoa utumwani Misri wana wa Israeli.  Alipokea amri zake na agano katika mlima Sinai.  Aliwaongoza Waisraeli kwa miaka 40.  Kut. 3:10-12

Aroni—Ndugu yake Musa na Kuhani Mkuu kwa utaratibu wa Makuhani. Kut. 28:1-3

Kalebi—Mmojawapo wa wapelelezi aliowatuma Musa wakamletea taarifa nzuri. Nu. 13:30

Yoshua—Aliteuliwa na Mungu kuwa mrithi wa Musa.  Yoshua aliwaongoza Waisraeli wakaishinda Kanani. – Nu. 27:18-23

Waamuzi—Walikuwepo Waamuzi 15 waliotawala Israeli baada ya kifo cha Yoshua.  Hili ni jina la kitabu kimojawapo katika Agano la Kale

Ruthu—Wamoabi ambao walirudi Betlehemu pamoja na Naomi mume wake alifia Moabu kabla Naomi hajarudi Betlehemu.  Ruthu aliolewa na Boazi akawa mmoja katika uzao wa mstari wa Kristo.  

Samweli—Aliitwa akiwa kijana na akawa mmoja wa manabii wakuu wa Israeli. I Sam. 3:20

Saulo—Mfalume wa kwanza wa Israeli. I Sam. 15:1

Daudi—Kijana mchungaji aliyemuua Goliati. Mungu alimteua kuwa mfalume wa Israeli badala ya Saulo. II Sam. 5:3-12

Solomoni—Mwanae daudi na mrithi wa ufalme wake. Mungu alimruhusu achague chochote apendacho. Yeya aliomba moyo mnyoofu na Mungu alimfanya awe na busara kuliko binadamu yeyote.  Alijenga hekalu lililojulikana kama Hekalu la Solomoni. I Fal. 3:5-12

Eliya—Nabii shupavu wa Mungu. Aliilaani Israeli ikapigwa na ukame kwa sababu ya dhambi. Aliomba moto ushuke kutoka mbinguni katika mapambano yake na manabii wa baali katika mlima Karmeli. Alishinda kifo na alipanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli.

II Fal. 2:11

Elisha— Mtumishi wa Eliya.  Aliyechaguliwa na Mungu achukue nafasi yake kama nabii wa Israeli. I Fal. 19:16

Isaya—Alimuona Bwana ameketi katika kiti cha Enzi kilicho juu sana na kuinuliwa sana na pindo za vazi lake zikalijaza Hekalu. Nabii aliyeonya Taifa la Israeli kutubu vinginevyo hukumu ya Mungu italiangukia. – Isaya. 6:1

Yeremia—Aliitwa kuwa nabii wa Mungu akiwa tumboni kwa mama yake.  Alielezewa kama Nabii aliaye aliyeshinda dhambi za Israeli. – Yer.. 1:5

Ezekieli—Alitabiri kutekwa kwa Yerusalemu kwa sababu ya dhambi zao. –Eze. 3:4

Danieli—Alichukuliwa na Nebukadneza kama mmojawapo wa mateka ya Yerusalemu. Alitafsiri ndoto ya Nebukadneza na kuelezea kuzuka kwa Himaya nyingi. Alipokea maono ya siku za mwisho na alikuwa mashuhuri katika himaya za Babeli na Persia – Dan. 1:6

Ezra—Kuhani na Mwandishi aliyerudi Yerusalemu kulijenga tena Hekalu. – Ezra 7:6

Nehemia—Alikuwa mbeba kikombe aliyerudi Yerusalemu na kuwa kiongozi katika ujenzi mpya wa Hekalu. – Imeelezwa katika kitabu cha Nehemia.

Esta—Malikia wa Ahesueru ambaye alikuwa mfalme katika mkoa wa Persia.  Alitimiwa na Mungu kusimamisha njama za kuwaangamiza watu wake ambao ni Wayahudi. Imeelezwa katika kitabu cha Ester

 

 

Yohana Mbatizaji—Aliyemtangulia Kristo.  Alibatiza wale waliotubu dhambi zao katika mto Yordani. Mt. 3:5-6

 Yesu Kristo—Mwana pekee wa Mungu. Mhusika Mkuu katika Agano Jipya. Agano jipya lote kwa kipekee linaweka katikati kazi za Kristo duniani, lakini Biblia kwa ujumla wake inaonyesha kwamba inamhusu kwa njia moja au nyingine.

Wafuasi 12 – Waliitwa na kufundishwa na Yesu; Kwamba watakuwa viongozi wa kanisa katika Agano Jipya. 1) Petro, 2)Andrea ndugu yake Petro 3)Yakobo mwanaye Zebedayo 4)Yohana ndugu yake Yakobo 5)Filipo, 6)Bartolomeo 7)Tomaso 8)Matayo  aliyekuwa mtumishi 9)Yakobo mwanaye Alfayo 10)Tadei 11)Simoni wa Kanani, na 12)Yuda Iskarioti.

Stefano—Mmoja wapo wa wale Mashemasi saba wa Kanisa waliochaguliwa kwanza katika Yerusalemu na kutofautishwa kati yao kama "mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu."  Alipigwa mawe hadi kufa chini ya utawala wa Sanhedrin ambao Saulo wa Tarso alikuwa mwanachama wake. Kifo cha Stefano ilikuwa ni mwanzo wa mateso makali kwa juhudi zilizoongozwa na Saulo, ambazo zilisababisha kuenea zaidi kwa Neno la Mungu.

(Mdo. 8:1,4; 11:19-21)

Philipo—Shemasi na Mwinjilisti (Mdo. 6:5; 21:8; Efe. 4:11). Alikuwa na watoto wa kike wanne waliojaliwa kipaji cha unabii (Mdo. 2:17; 21:8-9).  Baada ya kifo cha Stefano alihubiri injili toka Samaria na kwa towashi Mhabeshi kwa mafaniko makubwa na kukawepo na miujiza mingi.

Paulo—Aliinuliwa kuwa Mtume wa Mataifa. Alikuwa chombo cha kibinadamu kilichofikisha sehemu kubwa ya Agano Jipya kwa mataifa.  Mdo. 9:15

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Waraka ni barua. Hizi ni barua zenye pumzi ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya Kanisa.

 

 

 

Umoja Kamili wa Biblia

Mwanadamu amekombolewa kwa damu ya Yesu Kristo. Yesu ameshalipa kikamilifu  kwa damu yake iliyomwagwa msalabani bei ya ukombozi wa mwanadamu.  Wokovu kwa Damu ya Yesu ndio dhamira kuu ya Biblia. Dhamira hii inapatikana tangu kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo. Ahadi ya kwanza ya ukombozi imetolewa katika Mwa. 3:15. Nami nitaweka uadui kati yao na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huu utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

Huu ni utabiri kwamba Yule Masiha ambaye atakuja kutokana na uzao wa mwanamke siku moja atakiponda kichwa cha nyoka. Mada hii inaendelea mpaka kitabu cha Ufunuo.

 

Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukatukomboa kwenda kwa Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa; - Ufunuo 5:9  Andiko hili linahusu kufufuka kwa Kristo aliyetukomboa kwa Damu Yake.

Sadaka za kumwaga damu katika Agano la Kale zilikuwa ni aina inayofanana na Yesu ambaye ni Mwanakondoo aliyechinjwa kabla ya misingi ya ulimwengu. Wakisema kwa sauti kuu, Anastahili Mwana – Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka. (Ufu. 5:12)  Agano la Kale huangalia mbele kwa imani katika msalaba wa Kristo. Injili hii inamuonesha Kristo na Kifo chake juu ya msalaba. Agano Jipya huangalia nyuma katika kazi iliyomaliziwa katika msalaba.  Kristo hujidhihirisha mwenyewe katika Agano la Kale kwa nyakati tofauti na kwa njia mbalimbali.Kristo ameelezwa kwa namna ya kinabii kuwa ni Masiha ajaye.

Tangu Adamu hadi Abrahamu tunaona ______________ mwanzo wa jamii ya mwanadamu. Mwanzo 1:26, 27,  4:1,  5:1-5 ,32;  6:9, 10 ;  7:17-23; 9:1; 11:10, 27.

Kizazi_____ taarifa ya historia ya ukoo wa mtu somo la mtiririko wa familia

 

Tangu Abraham mpaka Kristo tunaona____________ mwanzo wa kabila teule. Taifa la waebrania .

Mwanzo 12:1,2;  22:15-18;   32:9-12;  Yoshua 1:1-3;  Mathayo 1:1, 2, 16 [Taifa hili lilianzishwa na kulelewa na mungu ili kumleta mwanadamu ulimwenguni.]

 

Tangu Kristo na kuendelea tunaona _________ Mwanzo wa kanisa. Mathayo 16:18; matendo 2:47;  11:26

 

Tunapata mwonekano wake katika kila ukurasa, katika maandishi matakatifu yaliyochirwa kwa Nuru, Mkombozi, Nabii, Kuhani.

 

 

II Biblia Haipingani.

 

 

 

 

 

Uwatakase kwa ile kweli; Neno lako ndiyo kweli. - Yohana 17:17

 

 

 

 

 

           

Jipya liko katika la Kale ndani yake; la Kale limeelezewa katika Jipya;

 Jipya liko katika la Kale linefichwa; la Kale ni katika Jipya limeoneshwa;

Jipya liko katika la Kale limetangulia kuoneshwa; la Kale liko katika Jipya limekomaa.

         “Huu mtungamano wote wa Biblia katika maelezo na mchoro, kwa uelewano wake utulivu na uthibitisho unaoelewana ungekuwa kunaonekana wazi kama ingekuwa umekamilishwa na kikundi cha wasomi waliofanya kazi pamoja wakiwa na mawasiliano ya kudumu ya habari na mawazo. Hata katika hali ya namna hioyo ambapo kila mwandishi angegawiwa sehemu iliyohaririwa na bingwa wa mawazo na ikapitishwa na kikundi kipana umoja uliounganishwa wa maandiko hayo ungekuwa ni mafanikio ya ajabu.  LAKINI, Biblia haikuandikwa kwa njia hiyo!  Iliandaliwa na waandishi 40 au zaidi ambao waliishi katika kipindi kinachozidi miaka 1600 katika nchi 13 tofauti ndani ya mabara 3 ambao waliandika kutoka katika maeneo na ujuzi usiofanana kabisa. Walikuwa wachunga kondoo, wafalme, wanajeshi, wana wa wafalme, makuhani, wavuvi, wasomi, wanahistoria, watalaam na vibarua wa kawaida. Kazi yao ilifanyikia maporini, majangwani, mapangoni, makasri, magerezani, kwenye meli na nyumbani. Waliandika kuhusu mada nyingi kwa mbinu tofauti katika angalao lugha tatu. Hata hivyo pamoja na tofauti za namna hiyo na matatizo yaliyotokana na kazi zao mbalimbali walichofanya kinaoana kwa hakika na ni sare, inayoonekana kuandaliwa moja kwa ajili ya nyingine.”

 

Kristo katika Vitabu 66 vya Biblia

 

Katika Mwanzo, Yeye ni uzao wa mwanamke 3:15

Katika Kutoka, Yeye ni Mwanakondoo  wa Pasaka 12:1-28

Katika Mambo ya Walawi, Yeye ni Sadaka ya upatanisho 1:14

Katika Hesabu, Yeye ni Mwamba, na yule Nyoka wa Shaba 20:8-11; 21:8,9

Katika Kumbukumbu, Yeye ni Nabii ambaye Atakuja 18:15,18,19

Katika Yoshua, Yeye ni Amiri wa jeshi la Bwana 5:13-15

Katika Waamuzi, Yeye ndiye aliyewakomboa watu wa Mungu 2:16,18

Katika Ruthu, Yeye ni  Mkombozi wa jamii 4:1-10

Katika I Samweli, Yeye ni Mpakwa mafuta 16:10-17

Katika II Samweli, Yeye ni Mfalme Aliyetawazwa 5:3-5

Katika I Wafalme, Yeye ni utukufu unaolijaza hekalu 8:10,11

Katika II Wafalme, Yeye ni uzao wa  kifalme aliyeokolewa kutoka kwa mchinjaji 11:1-3

Katika I Mambo ya Nyakati, Yeye ni Mfalme Mtukufu 11:2,3; 14:17

Katika II Mambo ya Nyakati, Yeye ni Bwana aliyemtokea Sulemani 7:12

Katika Ezra, Yeye ni Mtawanyaji Mkuu wa wanadamu ch.10

Katika Nehemia, Yeye ni Mrejezi mpya wa Taifa la Israeli 2:5

Katika Esta, Yeye ni Wakili wa watu wake 7:2-4

Katika Ayubu, Yeye ni Mtetezi aliye hai na sauti katika upepo wa kisulisuli 19:25; 38:1

Katika Zaburi, Yeye ni Mchungaji, ni Mwana, ni Mfalme wa Amani,

ni Mungu wa Majeshi, ni Mwenyezi Mungu       23:1; 2:12; 24

Katika Mithali, Yeye ni Hekima na ni rafiki akaaye karibu kuliko ndugu Mt.8,9; 18:24

Katika Mhubiri, Yeye ni Msingi wa Uhai Mhu.12

Katika Wimbo ulio Bora, Yeye ni Bwana Harusi Mtukufu

Katika Isaya, Yeye ni Imanueli, Mshauri wa Ajabu, Mwenye Nguvu,

Baba wa Milele, Mfalme wa Amani, na Bwana wa Mateso

alichubuliwa kwa maovu yetu 9:6; 53:3-6

Katika Yeremia, Yeye ni mfinyanzi wa Kimungu, Chipukizi la Haki, na

BWANA ambaye ni haki yetu 18:1-6; 23:5; 23:6

Katika Maombolezo, Yeye ni Yehova anayesikitika ambaye huwalea watu wake 1:1-6

Katika Ezekieli, Yeye ni Utukufu wa Bwana na ni yule

  Mfalme atakaye kuja 10:4,18;11:23; 44:4 21:26,27; 37:24

Katika Danieli, Yeye ni Jiwe Lililokatwa bila kazi ya mikono, ndiye Mtu

wa nne katika lile tanuru la moto, katika siku za zamani 2:34; 3:25; 7:22

Katika Hosea, Yeye ni mtoto aliyeitwa toka Misri 11:1

Katika Yoeli, Yeye ni Simba aungurumaye kutoka Sayuni 3:16

Katika Amosi, Yeye ni Hakimu wa Mataifa 9:8

Katika Obadia, Yeye ni Mfalme wa Ufalme utakaokuja 1:21

Katika Yona, Yeye ni mjumbe wa Bwana kwa Mataifa 1:1,2; 3:3-5

Katika Mika, Yeye ni Mtoto wa Betlehemu mtawala wa Israeli 5:2

Katika Nahumu, Yeye ni Ngome katika siku za tabu 1:7

Katika Habakuki, Yeye ni Bwana wa hekalu Lake takatifu 2:20

Katika Sefania, Yeye ni Mfalme wa Israeli 3:15-17

Katika Hagai, Yeye ni Bwana wa majeshi, ni Tamanio la mataifa 2:7

Katika Zekaria, Yeye ni Mfalme aliyepanda mwana punda na

ni Mchungaji Aliyepigwa   9:9; 13:7

Katika Malaki, Yeye ni Mjumbe wa Mungu, na Jua la Uchamungu

linalochomoza kwa uponyaji katika mbawa Zake 3:1; 4:2

katika zile Injili Nne, Yeye ni Mungu – Mtu akifundisha, akiponya, akihubiri,

akifa, na akifufuka tena Yoh.1:14; Mt.9:35; Lk.23:44-46;Mk.16:5,6

Katika Matendo, Yeye ni Bwana Aliyeshuka akiwa kazini ulimwenguni kwa

Roho Yake 1:8,9

Katika Nyaraka, Yeye ni Kristo katika mkono wa kuume wa Baba Mpatanishi

wetu, Kol.3:1; I Tim.2:5; Ebr.7:25; I Yh..2:1

Katika Ufunuo, Yeye ni Mshindi wa dhambi na kifo anayerudi katika utukufu 19:11-16

 

 

Uvuvio  wa  Biblia

 

 

 

2 Tim. 3:16—Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, la faa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadabisha katika haki.

 

Maneno katika taarifa ya kuwa na pumzi ya Mungu ni tafsiri kutoka katika neno moja la Kiyunani: theopneustos, ambalo limetolewa katika neno  Theos  - Mungu na  pneuma – Roho Mtakatifu.  Pneuma limetolewa kutoka neno lenye maana ya pumzi. Tafsiri halisi ya maneno haya (iliyotolewa kwa pumzi ya Mungu) ni: ILIYO PUMULIWA NA MUNGU  

 

 

II Petro 1:21—Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

 

Unabii katika maandiko haya yanahusiana na aya ya 20 inayosema: Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Aya hizi zinahusu unabii ulioko katika Maandiko. Maandiko hayakuletwa kwetu na mwanadamu.  Wale wanadamu walisukumwa na Roho Mtakatifu. Kitendo hiki Kitukufu cha Mungu.  

Je tumeshapata Neno lenye pumzi ya Mungu? Ndiyo, tumeshapata!  Haitoshi kujibu ndiyo peke yake swali kama hili, kila muamini anapaswa kufahamu bila shaka yeyote kwamba Biblia siyo kitu kingine zaidi ya pumzi ya Mwenyezi Mungu.  

 

 

Wazo hili la uwongo hushikilia kwamba Biblia ni tunda la mtu mmoja mwerevu wa hali ya juu, ila siyo mwenye nguvu za ajabu au za Utukufu. Hii ni aina ya msukumo ambao umeoneshwa katika maandishi ya Milton, Shakespeare au Confusius. Hakuna binadamu mwenye kipaji hata kiwe cha namna gani, ambaye akisoma alichoandika Shakespeare kisha akaisoma Biblia atashindwa kuona tofauti kati ya mambo haya mawili kuwa ni kubwa sana. Kitabu kinaweza kuwa na uvuvio bila kuwa na pumzi. Biblia inavipita kwa mbali vitabu vya wanadamu.

 

Wazo hili la uongo hudai kwamba Mungu alitumia ngazi mbalimbali za udhibiti kwa vipindi tofauti katika mchakato wa msukumo. Wazo hili linatetewa zaidi kwamba Mungu alitumia utukufu wake na wakati mwingine, alitoa tu mapendekezo au alianzisha jambo kwa maagizo. Hii ni kinyume kabisa na msukumo wa kweli wa Biblia.

 

Wale wanaoshabikia wazo hili la uongo wanasema kwamba mapendekezo au mawazo hayo yalipewa uvuvio. Msimamo huu unawapa wanadamu nafasi ya kutumia maneno yao katika taarifa hizo kutoka akili mwao. Hii ni kinyume na maana halisi ya uvuvio wa kweli wa Biblia.  

 

Haya ni mafundisho ya uongo ambayo ni hatari kuzungumzia sehemu tu kuwa na pumzi. Msimamo huu unatamka kwamba Biblia inalo Neno la Mungu lakini siyo maandiko yote yamepumuliwa. Ni nani basi wa kuamua nini ndiyo na kipi hakijapumuliwa? Nadharia ya namna hiyo inamuacha mwanadamu katika hali tata na hatari ya kutokuwa na uhakika.

 

 

 

 

 

 

II Tim. 3:16—Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu ……

 

Wazo kwamba Biblia katika ukamilifu wake inayo pumzi ya Mungu huitwa uvuvio kwa mamlaka. Mamlaka maana yake kamili au timia. Biblia kamili huanzia mwanzo mpaka ufunuo ni Neno la Mungu lenye uvuvio. Maandiko yote yamepumliwa sawasawa.

Kwa kuwa imepumuliwa na Mungu Biblia haiwezi kuwa na kosa. Haiwezi kuwa na kosa maana yake imetenganishwa kabisa na uwezekano wa kukosewa. Maneno hayo huhusishwa na Mungu ambaye hawezi kufanya kosa au kughafilika. Katika matumizi yake kuihusu Biblia kutokuwa na kosa kunahusu Utukufu wa Mwandishi wa Maandiko. Muandishi huyu Mtukufu hafanyi makosa na kwa hiyo Neno lake haliwezi kuwa na kosa.

 

Mara kwa mara tena tunaweza kupata maelezo yafuatayo katika Agano la Kale:

 

“Neno la Bwana”         “Mungu akaamuru” “Mungu akasema /akaonge

“Bwana akasema”   “Mungu akatokea”    “Asema Bwana”

 

Maelezo kama haya yanadhibitisha uvuvio wa Agano la Kale. Uthibitisho wa madai haya uko wazi kutokana na umakini wa kila neno la taarifa na majina, nyakati na mahali ambako watendaji walikamilisha ujumbe wao na, ukamilifu wa kutimia kwa unabii wao.

 

Matendo 28:25—Na walipokuwa hawapatani wao kwa wao, wakaenda zao, Paulo alipokwisha kusema neno hili moja, ya kwamba, Roho Mtakatifu alinena vyema na baba zetu, kwa kinywa cha nabii Isaya,

 

2 Petro 1:21—Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

 

Waebrania 1:1—Mungu ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi.

 

Kumb.18:18-22—v. 22 Atakaponena nabii kwa jina la Bwana, lisifuate jambo lile wala kutimia hilo ndilo neno asilonena Bwana; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimuogope.

 

Waandishi wa Agano Jipya wanadai kuwa uvuvio kwa waandishi wa Agano la Kale  unawahusu wao pia:

Matendo 1:16—…ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi kwa habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu....,

Maandiko yanatamka kwamba watu watakatifu wa Mungu waliongea kama walivyosukumwa na Roho Mtakatifu. – 2 Petro 1:Mungu aliwavuvia Neno lake watu ambao walikuwa ni vyombo vya kibinadamu kuandika Biblia. Kauli za Manabii kutoka kwa Mungu zilitumiwa na Mungu kuwasiliana na watu Wake. Bwana aliwaagiza wengi wa watu hao kuandika Maneno Yake. Watu hao walivuviwa na kuagizwa na Mungu kuwapatia watu wake Neno lake.

 

E. Yale Maneno Yalivuviwa

 

Yuda 17—Bali ninyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo;

2 Petro 3:2—Mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mokozi iliyoletwa na mitume wenu.

Yohana 12:48—Yeye anikataaye mimi,asiye yakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.

 

Zile herufi za maneno ya Biblia zimevuviwa kwa Utukufu wa Mungu. Kwa mfano, hebu tuangalie mafundisho ya “punje moja na siyo nyingi” kwa njia ya Kristo ambao ilidhibitishwa kwa matumizi ya herufi: ‘u.’

 

Wagalatia 3:16—Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu kwa mzao wake. Hasemi, kwa wazao kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni  mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo. (linganisha na Mwanzo. 22:16-18)

 

Herufi ‘u’ katika aya hii inaweka tofauti KUBWA.  Herufi ‘u’ inaweka tofauti kati ya umoja na wingi na muhimu zaidi tofauti ya kutamka kwamba kuna msuluhishi mmoja au kutamka kwamba wapo wasuluhishi wengi. Iwapo Mungu angesema wazao’ badala ya uzao’ ahadi hizo zingeweza kutolewa kupitia Confucius, Buddha, Mohammed, Papa au mwingine yeyote ambaye amechagua kujitwalia umaarufu huu. Kwa kutumia umoja, Mungu ameufunga mlango kwa manabii wa uongo na kumnyanyua Kristo kama njia PEKEE ya kwenda kwa Mungu. Punje ya Ahadi inaweza kuwa Kristo tu, na siyo Kristo na Buddha au Kristo na Muhammed. Yesu Kristo peke yake alikuwa ndiye punje ya ahadi.

 

Mathayo 5:18—Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka Mbingu na Nchi zitakapoondoka yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.

 

Yodi inaweza kulinganishwa na apostrofi (‘) na nukta kulinganishwa na kistari ungio (-).

 

“Biblia siyo kitu kingine isipokuwa ni sauti Yake yule akaaye katika kiti cha enzi. Kila kitabu chake, kila mlango, kila aya, kila neno, kila silabi, kila herufi, ni tamshi lake Yule Aliye Juu ya Yote.”—Dan Burgon

 

 

 

 

 

II Kor. 5:17—Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Jedwali lifuatalo ni orodha ya watu wa Mungu ambao waligeuka kupitia sehemu mbalimbali za maandiko. Maandiko haya yalikuwa na matokeo katika maisha ya watu hawa wa Mungu.

John Calvin

Isaya 53:5

C.H. Spurgeon

Isaya 45:22

Henry Moorhouse

Mathayo 1:21

John Williams

Marko 8:36

Sir James Simpson

Yohana 3:14,15

W.P. Lockhart

Yohana 19:30

David Livingston

Matendo 16:31

William Cowper

Warumi 3:25

Sir  George Williams

I Wakorinto 15:1-4

Martin Luther

Wagalatia 3:11

Lord Shaftesbury

I Petro 3:18

Hedley Vicars

I Yohana 1:7

James Chalmers

Ufunuo 22:17

Robert Moffat

Yohana 3:16

Duncan Mathieson

Yohana 3:16

Richard Weaver

Yohana 3:16

Hakuna yeyote aliyewahi kusikia mtu aliyefanywa “kiumbe kipya” kupitia Homer, Shakespeare, Scott, Dickens, Macauley, Huxley, Carlyle, Eliot, Kipling, Wells, au mtu mwingine yeyote? Mamilioni ya watu wamefanywa wapya kwa kusoma na kuiamini Biblia ambayo ni Neno la Mungu.

 

Biblia huzalisha ukuaji wa Kiroho katika maisha ya Watakatifu wa Mungu. Biblia ni chakula cha roho ya Mkristo na inapaswa kusomwa kila siku ili kupata nguvu na kukua Kikristo.

Yeremia 15:16—Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ya furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu maana nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA, Mungu wa Majeshi.

1 Petro 2:2—Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa,ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu:

Biblia inaweza kuyasafisha maisha ya wanaume na wanawake. Roho Mtakatifu atawahukumu wanadamu kwa Neno. Biblia itaonesha wanadamu kitu kinachopaswa kubadilishwa katika maisha yao. Maji yaliyopo katika Hema ya kukutania ni alama ya Neno la Mungu. Makuhani walipaswa kunawa katika maji hayo kila wakati waendapo kufanya ibada ya Bwana.

Yohana 15:3—Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu lile neno nililowaambia. (Eph. 5:26)

Zaburi 119:9—Jinsi kijana aisafisha njia yake? Kwa kutii akilifuata Neno lako.

 

Kunakuwepo na nguvu na kuwa na moyo katika neno la Mungu. Neno la Mungu litakujenga na kukuweka imara katika wakati mgumu. Wakristo wanaweza kusimama katika mwamba huu imara.

Warumi 16:25—Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara sawasawa na Injili yangu…

Waefeso 2:20 -22—Mmejengwa  juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe Hekalu Takatifu katika Bwana. Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.

Upo ushahidi ulio wazi wa kudhibitisha uvuvio wa Biblia. Zaidi ya matamko yaliyomo katika maandishi yenyewe, taarifa nyingi za ukweli wa Biblia zinaonyesha kwamba maandiko yalivuviwa kwa utukufu.

Biblia inavyo vitabu 66 vilivyoandikwa kwa lugha 4 na watu 40 ambao walikuwa wakiishi umbali wa zaidi ya maili 1500 katika kipindi cha miaka 1600.  Watu waliotumiwa walitoka katika ngazi mbalimbali za maisha; Baadhi yao walikuwa wafalme, madaktari, manabii, wachungaji, wafanya kazi, wavuvi, na mmoja alikuwa mtoza ushuru.  Pamoja na ukweli huo mtiririko wake haukuvunjika na inao utimilifu ulio na umoja katika Biblia nzima. Hii inaweza kuwa kazi ya Mungu peke yake.  

 Biblia husema mapema kuhusu matukio ya miaka au karne nyingi zijazo kabla hayajatokea. Wakati wa kuandikwa kwa unabii ulioko katika Agano la Kale unaweza kuelezwa kwa historia kwa sababu taarifa sahihi za historia kati ya maagano yote mawili imeendelea kuwepo.  Taarifa hii ya kihistoria inathibitisha tarehe ya kuisha kwa Agano la Kale kwa kuweka kipindi cha miaka 400 ambacho Biblia imekuwa kimya kati ya utabiri wa mwisho wa Agano la Kale na ukamilishaji wake kuanza katika Agano Jipya.

Tarehe ambazo vitabu vya Biblia zimeandikwa zinaweza kupatikana katika historia. Uwepo wa Septuaginti, yaani ile tafsiri ya Kiyunani ya Agano la Kale unaweza kuwekwa kwa usahihi katika miaka 250 kabla ya Kristo. Kwa kuwa Septuaginti ilitafsiriwa kutoka katika maandishi ya Kiebrania ni lazima kulikuwepo na Agano la Kale la Kiebrania angalau miaka 250 kabla ya kuwepo kwa Agano Jipya. Uthibitisho huu ni wa kihistoria kwamba unabii huo uliandikwa miaka 100 kadhaa kabla ya kutokea utimilifu wake katika Agano Jipya. Hakuna uwezekano wa mwanadamu kuweza kutabiri kwa uhakika wa namna hiyo. Huu ni uthibitisho usiokuwa na ubishi ya kwamba Maandiko ya Injili yamevuviwa.

MIFANO YA UNABII ULIOKAMILISHWA KWA UHAKIKA:

Mdo. 3:18—Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Kristo alitimiza unabii wote katika Agano la Kale kumhusu yeye pamoja na mashaka yote. Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kuchagua ukoo wake kabla ya kuzaliwa ingawa Yesu alizaliwa katika ukoo kama ilivyokuwa imetabiriwa na manabii. Walikuwepo watu wengine waliohusika katika ukamilisho wa unabii huo kama askari wa Kirumi ambao waligawana mavazi ya Yesu kati yao na kuipigia kanzu yake kura.  Hata lile giza lililotokea Kristo alipofariki linaweza kuthibitishwa kwa taarifa za historia na nyingine zilizoandikwa.  Nabii Amosi alitabiri giza lile miaka mia 700 hivi iliyopita kabla ya kutokea kwake.  Hakuna mwanadamu anayeweza kuelezea kwa usahihi kutimia kwa utabiri huu wa Kimasiha.  Huu ni uthibitisho ulio wazi wa uvuvio wa Biblia!

 

Ezekieli 36:24—Maana nitawatwaa kati ya mataifa nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe.

 

Mungu alisema atamleta Mfalme wa Babeli kuwapinga. Aya ya 7.  Utabiri huu unasema kwamba yale mawe, mbao na udongo vitatupwa katika maji. Aya ya 12.  Nebukadneza, Mfalme wa Babeli, aliuzingira mji wa Tiro kwa miaka 13.  Aleksanda Mkuu aliuteka mji wa Tiro katika kile kisiwa mwaka 332 Kabla ya Kristo kwa kujenga daraja toka nchi kavu hadi kisiwani. Walitumia mawe, mbao kutoka kwenye majengo yaliyoharibiwa na udongo wakaujaza kutengeneza kinachoitwa bomazuizi (daraja la udongo) katika maji. Wale Askari waliweka mawe, mbao, na udongo majini kama ilivyotabiriwa na manabii. Jambo hili la hakika lililotabiriwa na likatokea siyo kubahatisha kwa binadamu peke yake.  Biblia ni Neno lililovuviwa la Mwenyezi Mungu. Lile Bomazuizi la Aleksanda Mkuu bado liko mahali pale hadi leo.   

 

4. Unabii wa Siku za mwisho

 

2 Timotheo 3:1-9—msitari 1 Mambo haya mfahamu pia, kwamba katika zile siku za mwisho…

 

Yako maelezo mengi ambayo ni sahihi kuhusu siku za mwisho yanayopatikana katika Maandiko. Haya ni baadhi tu ya mambo yaliyotabiriwa ambayo yanaeleza hali ya siku zetu:

Fikiria kuhusu vitu vyote vipya vilivyogunduliwa katika kipindi cha miaka 100.  Wale ndugu wawili wajulikanao kama Wright waliruka kwa ndege kwa mara ya kwanza 1903 na leo usafiri wa anga ni njia ya kawaida ya usafirishaji. Kumekuwa na maendeleo makubwa ya Teknologia katika muda mfupi sana.

(walikunywa, wakauza, wakanunua, wakapanda na wakajenga. Hali hii inasikika sana kama ilivyo kwa watu wa leo. Kuna ongezeko pia la dhambi ya ushoga leo kuliko ilivyokuwa siku za Lutu.)

 

Akiolojia ni kuhusu mafunzo mambo ya kale kwa kutafuta vitu vilivyotumiwa na watu wa zamani. Vitu hivi vya zamani vinatupatia habari kuwahusu watu ambao walivitumia. Kumesha gunduliwa vitu vingi kudhihirisha usahihi wa kihistoria wa Biblia. Kwa kweli, hakuna chochote cha akiolojia kilichopatikana kinachopinga Biblia.  Wakosoaji wamebisha kwamba Biblia si sahihi kwa historia lakini akiolojia inaendelea kudhihirisha kwamba Biblia ni ya kweli.  

Makitaba ya Wahiti iligunduliwa huko Uturuki 1906 ikidhibitisha usahihi wa Taarifa ya Biblia kuhusu jamii ya Wahiti.

Kumekuwep na vionzi vya mfupa vilivyopatikana vya majitu makubwa kudhibitisha maelezo ya majitu iliyoko katika Biblia.

Masalia ya mtu aliye uawa kwa kusulubiwa yalipatikana Yerusalemu mwaka 1968. Masalia hayo yalikuwa na tundu la msumari katika miguu yake lililopita katika nyayo zote mbili na tundu moja la msumari katika viganja vya mikono. Mtu huyo aliaminika kwamba aliuawa na Warumi wakati wa uasi wa Wayahudi mwaka wa  70 baada ya Kristo.  Hii inathibitisha kwamba kusulubu msalabani ilikuwa ni njia ya kutekeleza hukumu ya kifo iliyotumiwa na Warumi kama ilivyoelezwa katika taarifa za Biblia kuhusu kusulubiwa kwa Yesu.

Kitabu cha Matendo kimethibitishwa kihistoria kuwa sahihi.

Michoro imegunduliwa yenye majina ya watu walioelezwa katika Biblia katika maeneo ambamo Biblia imewaweka.

Zimekuwepo taarifa za kupatikana kwa vifaa vya akiolojia vinavyoendelea kudhibitisha usahihi kihistoria wa Biblia. Huu ni ushahidi zaidi ambao unathibitisha uvuvio wa Neno la Mungu.

 

 

Biblia iko sahihi kisayansi.  Yapo mambo kadhaa katika Biblia ambayo wanadamu walioyaandika hawakuwa na uelewa wa kuweza kuyajua.  Mungu ndiye mwandishi wa Maandiko Matakatifu na anafahamu mambo yote.

Maelezo yaliyoka katika Biblia ni ya kweli na yako sahihi kisayansi.

Vipimo vya safina ya Nuhu alivyopewa na Mungu vinalingana na meli inayofaa kabisa kwa usafirishaji baharini.  Meli za kisasa zimeundwa kwa uelewa mkubwa wa fizikia na matumizi ya teknologia ya kompyuta na zinatumia vipimo kama alivyotumia Nuhu.  Isingewezekana Nuhu apate elimu hiyo kwa wakati wake.  Ni jambo la busara katika hali kama hiyo kuamini kwamba taarifa kuhusu vipimo vya safina katika Biblia ambavyo Mungu alimpatia Nuhu ni sahihi.

 

Katika kitabu cha Ayubu kuna taarifa kuhusu kugawanywa kwa mwanga. Ayubu 38:24 Mwanga unaweza kugawanywa katika vipande kwa kutumia mche wa kioo. Hakuna uwezekano wa Ayubu katika kitabu chake ambacho ni cha zamani zaidi kuliko vyote katika Biblia aweze kufahamu kwamba mwanga unaweza kugawanywa.  

Kitabu cha Mhubiri kinazungumzia mizunguko ya upepo. Kuna mizunguko ya upepo na maumbo yake ambayo imegundulika katika sayansi hivi karibuni kwa matumizi ya setelaiti na kompyuta. Watu katika zama za Agano la Kale wasingeweza kuwa na habari kama hizo japo kwa mara nyingine Biblia inayo taarifa sahihi kuhusu mizunguko ya upepo.

Mwandishi wa kitabu cha maombolezo angewezaje kujua kwamba mito ilimwagikia baharini. –Mhubiri. 1:7

Nabii Isaya alizungumza kuhusu Mungu akiwa ameketi katika duara ya dunia.  Isaya. 40:22.  Dunia haikuthibitishwa kuwa duara mpaka Magellani alipoizunguka kwa merikebu miaka ya 1500. Isaya hakuwa na uwezo wa kupata habari hizo. Ili kwa mara nyingine tena ni jambo linalothibitisha uvuvio wa Maandiko.

 

 

Warumi 1:16—Kwa maana siionei haua Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao Wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.

 

Biblia ni zaidi ya kitabu. Biblia ni neno la Mungu.  Wale ambao wanaisoma Biblia kwa umakini katika imani wanaweza kubadilishwa kwa nguvu ya Mungu. Mungu anaweza kuitumia Biblia kubadilisha maisha ya wanadamu. Maisha ya watu wengi yameshabadilika kwa nguvu za Mungu kwa kuisoma tu Biblia na kuiamini.

Biblia inanguvu za kuwaokoa watu katika hali zote za maisha: walevi, wabuya unga, malaya, wezi, wauaji, watenda dhambi wote. Wote wanaweza kuokolewa kwa njia ya Yesu Kristo. Tunaweza kupata muongozo katika Neno la Mungu kwa kila tukio la maisha yetu, kwa ushauri usiokuwa na ubaguzi wowote. Biblia inasimama imara juu ya kitabu chochote kile kilichoandikwa bila ushindani wala kupingana. Kwa usahihi Biblia ndio kitabu pekee alichoandika Mungu.

 

Kuorodheshwa kwa vitabu vya  Biblia

 

Mchakato wa ukusanyaji wa vitabu vya Biblia katika mfumo wake wa sasa ndio kunakoitwa: kuorodheshwa kwa vitabu vya Biblia. Jambo hii halikufanyika kwa siku moja.  Ikumbukwe kwamba kila kitabu kimoja ilibidi kiandikwe kwa mkono na kwa umakini mkubwa.  Vitabu hivyo vilitumiwa na kusambazwa na viongozi wa dini wa siku hizo.  Kulikuwepo pia vitabu vingine vilivyodai kuwa na uvuvio ambavyo havikuingizwa katika Biblia. Kulikuwepo na vitabu vya dini na historia ambavyo vilikuwa vinasambazwa wakati wa kuamua ni vitabu gani viingizwe katika Orodha hiyo. Mchakato huu wa kutambua vitabu vyenye uvuvio na vipi havina ndio jambo tutakaloangalia katika somo la sehemu hii.  Tutajaribu pia kulijibu swali: Biblia iliwezaje kufikia katika hali iliyo nayo sasa?

 

 

 

 

 

 

Ni Kigezo gani kilitumika kuamua vitabu gani viingizwe katika Biblia na vitabu vipi visiingizwe katika orodha ya Maandiko Matakatifu?  Hili ni swali muhimu ambalo inabidi lipatiwe majibu na mwanafunzi makini wa Biblia.  Uanapaswa kufahamu bila shaka yeyote kwamba  Biblia katika mfumo wake wa sasa ndio NENO LA MUNGU LENYE UVUVIO

 

 

 

 

Mabaraza ya dini hayakuamua vitabu vya kuorodheshwa katika Biblia.  Mabaraza ya wanadamu hayawezi kufanya kitabu kuwa Andiko Takatifu ambacho katika asili yake siyo maandiko matakatifu.

 

 

 

 

Hali hii ndio inayosemekana kwamba ni sababu pekee ya umoja na uelewano wa Maandiko Matakatifu. Ubishi ni kwamba wanadamu waliondoa vitabu ambavyo havikukubaliana na maoni yao na kuingiza vile ambavyo vilikubaliana na maoni yao.  Maoni haya ya yongo humuweka mwanadamu katika nafasi ya uamuzi wa orodha ya kanoni.

 

 

Mungu alimpatia mwanadamu vitabu ambavyo alitaka viingizwe katika Biblia.  Mungu alilinda na kuhifadhi vile vitabu alivyovivuvia na kuvitunza hadi wakati wa kuviweka katika orodha ya Biblia.

 

 

Kitabu kiliweza kuingizwa katika Kanoni  kwa sababu ya kutambuliwa kwake kuwa na Uvuvio wa Wakiungu wa Neno la Mungu. Kitabu ambacho kilionekana kutokuwa na Mamlaka ya Kiungu hakikuingizwa katika Biblia kama sehemu ya  kanoni ya Maandiko Matakatifu.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Kumbukumbu 31:24-26—Basi ikawa hapo Musa alipomaliza kuandika maneno ya Torati hii katika Chuo, hata yakaisha, 25 ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la Agano la BWANA akawaambia, 26 Twaeni chuo hiki cha Torati, mkiweke kando la agano la BWANA, Mungu wenu, ili kiwepo kama shahidi juu yako.

Sheria iliwekwa kama muongozo kwa Makuhani ili kuitunza pamoja na lile Agano. Makuhani hao waliagizwa kuisoma Sheria kila miaka saba.

 

 

 

 

Mathayo 5:18—Kwa maana Amini, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya Torati haitaondoka, hata yote yatimie.

 

 

  Waandishi wa Kiyahudi walinakili kwa uangalifu mkubwa na kuhifadhi maandishi ya Agano la Kale.  Augustino alisema, waandishi wa Kiyahudi walikuwa ni Wakutubi wa kanisa la Kikristo. Waandishi wa mwanzo kabisa kati ya hawa waliitwa Tannaim (walimu) walinakili maandishi ya Agano la Kale kwa usahihi mkubwa. Watannaim walifuatwa kwa hadhi na kikundi cha waandishi walioitwa Amoraim (wafichuaji). Hawa walikuwa ni wasomi waliofanya kazi siyo kama wa kunakili tu, bali walizalisha pia ile Talmud ambayo ni kitabu kinachoweka hadharani sheria na mila za Wayahudi.

 

 

 

 

Walimu (Rabi) wa Kiyahudi waliziweka nakala za Maandiko Matakatifu katika heshima ya hadhi ya juu.  Wakati andiko lolote lilipo zeeka au kuchujika na kuonekana halifai kwa matumizi lilipumzishwa kwa heshima kuu.  Iliaminika kwamba ni bora zaidi kuzizika kwa heshima kuliko kuthubutu kuziacha ziangukue mikono isiyofaa au kudharauriwa. Hii ndio sababu ya kuwepo nakala nyingi za Agano la Kale zilizoandikwa.

 

 

 

 

 

Yapo majaribio yaliyotumiwa na viongozi wa Wayahudi ili kuamua kanoni ya kitabu misingi hii ilizingatia walichotaka waandishi wa historia ya Biblia na kanisa.  Ulikuwepo mfumo maalumu wa kuangalia utambuzi wa kanoni ya kitabu.  Sehemu hii inataja waandishi wa kanoni za vitabu vya Biblia. Maelekezo haya ni kuhusu ukweli kwamba walikuwa ni vyombo vya kibinadamu  vya mwandishi wa kiungu.

 

Uandishi wa Musa wa kitabu ulichukuliwa kama jaribio halali la uvuvio na Wayahudi tangu zamani. Musa anatajwa kama nabii mkuu wa Wayahudi. Vitabu ambavyo viliandikwa na Musa vinachukuliwa kama vyenye asili ya Mungu kutoka mwanzoni kabisa mwa taarifa za historia ya Wayahudi.  Ushahidi wa akiolojia wa Palestina unaimarisha sana mtazamo huu wa kitamaduni.  Yesu alithibitisha kwamba Musa ndiye chombo cha kibinadamu kilichopokea ile Sheria. Musa hakuwapa torati? – Yoh. 7:19. Kama tunavyofahamu taarifa iliyoandikwa katika Biblia inaonesha kukubalika mara moja kwa vitabu vya sheria kama vilivyotolewa na Mungu.

 

Iwapo kitabu hicho kiliandikwa na nabii wa Mungu anayejulikana ambaye alifikiriwa kama mwaguzi wa Mungu; kitabu hicho kiliaminiwa kuwa ni Neno la Mungu.

 

Mwandishi alichukuliwa kuwa mtu wa Mungu iwapo alionesha ushahidi wa nguvu za Mungu katika maisha yake.  Kama mwandishi alichukuliwa kama mtu wa Mungu na maandishi yake pia yaliaminika kwamba yametoka kwa Mungu. Watoto wa manabii walitambua mamlaka ya Elisha walipomuona amechukua nafasi ya Eliya na kuutenganisha mtu Yordani. – II Fal 2:15.

 

Ni lazima kuwepo umoja kamili wa Maandiko.  Kanuni katika sehemu moja ya Maandiko ni lazima ielewane na ukweli ulioko katika sehemu nyingine za Maandiko. Kama ilivyokwisha tamkwa wengine watabisha kwamba vitabu vilivyochaguliwa ni vile vinavyopatana na maoni ya viongozi ambao walivichagua.  Hata hivyo kitabu kisingeweza kuhesabika kama cha Kanoni iwapo isingekuwa kinakubaliana na Maandiko mengine yaliyopokelewa.  Kitabu kilitambuliwa kuwa cha Kanoni kwa sababu ya kuwa na uvuvio.  Jambo hili kama tunavyoweza kuona siyo jaribio pekee la kuthibitisha kanoni ya kitabu.  Ni wazi kwamba Kitabu chenye asili ya Mungu hakitapingana na kitabu kingine chenye asili ya Mungu.

   

Ni lazima kitabu kiwe sahihi katika maelezo yake kumhusu Mungu na kuhusu vitu vya Mungu.  Kitabu hicho kitakaliwa kwa kutokuwa na uvuvio iwapo kutakuwa na makosa kuhusu teolojia.

 

Baadhi ya vitabu vilikubaliwa na viongozi wa Wayahudi kama vya kanoni na vingine vilikataliwa.  Huu ni ushahidi kwamba viongozi wa Kiyahudi walitambua vitabu hivyo ambavyo viliingizwa katika Kanoni kama Maandiko yenye mamlaka.

 

 

 

Luka 24:44—… ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na

katika Manabii na Zaburi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 “hatupaswi kulionyesha kama ni chimbuko la Erasmo la ‘maandishi yaliyopokelewa’ bali kama muendelezo wa kutoka kwenye maandishi ya mkono iliyozooeleka jinsi ilivyopokelewa kwenda kwenye mfumo wa kuchapisha, ambao uliendelea kuwepo kwa karne tatu.” – Kenneth W. Clark, msomi wa Maandishi ya Kiyunani  (msisitizo umeongezwa)

 

 

Mathayo 24:35—Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

 I Petro 1:23—Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili si kwa mbegu iharibikayo bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima lidumulo hata milele.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Yalikuwepo majaribio ambayo yalitumiwa na kanisa la mwanzo kuamua kuwepo kwa kanoni katika kitabu. Walikuwepo viongozi wa kanisa waliohusika kwa wakati mbalimbali ambao waliamua ni vitabu gani vyenye uvuvio na visivyokuwa nao.  Ifuatayo ni miongozo mnne iliyotumiwa na viongozi hawa katika ugunduzi wao wa kanoni ya Agano Jipya.

 

 

Tunaelewa kwamba Mungu ndiye mwandishi wa Agano Jipya.  wale Mitume walikuwa ni baadhi ya watu watakatifu wa Mungu ambao kwa Utukufu wake Mwandishi aliongea kuwapitia wao.  Kama kitabu kiliweza kuthibitishwa kuandikwa na mmoja wa wale mitume wa mwanzo wa Yesu kilichukuliwa kama chenye asili ya Mungu.  Uzito mkubwa uliwekwa katika ufundishaji na maagizo ya mitume wale wa mwanzo. Maandiko yaliyowahusu wao yalisambazwa kati ya jamii za Kikristo za kwanza kabisa.

 

Iliaminika kwamba wale mitume wa kwanza walifahamu zaidi ni vitabu vipi vyenye uvuvio na ni vipi visivyokuwa nao. Kitabu ambacho hakikuandikwa na mtume ambacho kilikuwa na idhini ya Kitume kilichukuliwa kuwa na asili ya Mungu.  

 

Vipo vitabu fulani ambavyo vilikubaliwa haraka na kanisa la mwanzo kuwa Maandiko yenye Utukufu wa Mungu.  Vitabu hivi viliingizwa mara moja katika Kanuni. Kulikuwepo na vitabu vingine ambavyo vilichukua muda kukubaliwa na kanisa kuwekwa katika orodha ya kanoni.

 

 

Tunayo taarifa ya kihistoria kutoka kwa viongozi wa mwanzo wa kanisa zinazoonesha kwamba ni vitabu gani vilisomwa katika makusanyiko ya kanisa.  Vitabu hivi vilitumiwa na kanisa kwa sababu vilichukuliwa kama vyenye uvuvio.

 

 

Kama ilivyokwisha tamkwa kuhusu kukubaliwa kwa Maandiko ya Agano la Kale kwamba ni lazima kitabu kioane vizuri na vitabu vingine vyenye kanoni iliyokwisha kubalika. Pamoja na hayo, vitabu vya Agano Jipya ambavyo vilipokelewa vinapaswa kuwa na uwiano na kanoni ya Agano la Kale na kanoni ya Agani Jipya ya Maandiko Matakatifu.    

 

Vitabu 20 kati ya 27 vya Agano Jipya vilikubalika mara moja na vikapokelewa ulimwenguni pote kuwa asilia na kuitwa Homologoumena.  Vitabu hivi  20  ni zile Injili nne, Matendo, Nyaraka za Paulo (isipokuwa Waebrania), na nyaraka za kwanza za Yohana na Petro.

 

Vitabu vile saba vya Waebrania, II Yohana na III, II petro, Yuda, Yakobo, Ufunuo vilipingwa kwa kipindi fulani na kuitwa Antilegomena.  Yalikuwepo maswali kadhaa kuhusu vitabu vilivyoitwa Antilegomena.  Moja ya maswali hayo ni lile la kwamba viliandikwa kweli na wale watu wanaoitwa waandishi wake. Waebrania kilikuwa hakina jina la mwandishi wake na kilitofautiana na mwelekeo wa nyaraka za Paulo uliofahamika; II Petro ilikuwa na tofauti na I Petro; Yakobo na Yuda walijiita watumishi; na siyo mitume; mwandishi wa II Yohana na III Yohana alijiita mzee na siyo mtume. Uandishi wa kitume ulichukuliwa kama kigezo muhimu katika kutambua kanoni ya kitabu. Yalikuwepo maigizo mengi yaliyodai mamlaka ya kitume, kwa hiyo vitabu hivi vilichunguzwa kwa makini kabla ya kuingizwa katika kanoni.

Swali lingine ni kwamba Yuda aliandika taarifa ambazo hazijatajwa mahali pengine katika Maandiko na anamtaja Henoko jambo ambalo lilihusishwa na Apokrifa.  Kitabu cha Ufunuo hakikueleweka kwa viongozi wengi wa kanisa kwa hiyo kikazua maulizo katika akili zao. Vitabu hivi havikukubalika mara moja na kuwekwa mahali pake katika kanoni. Baada ya kuchunguzwa kwa makusudi mwishoni vilipokelewa kama halisi, na ucheleweshaji wake ukathibitisha uchunguzi ambao ulitumika katika mchakato wa kuviweka kanoni. Mwanzoni mwa karne ya nne vilipokelewa katika makanisa mengi na mwishoni mwa karne hiyo vikapokelewa na makanisa yote.

 

 

 

 

 

 

Kanuni ya Kiyahudi inaundwa na vitabu 39 vya Agano la Kale.

 

 

 

Marisiyo ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kutengeneza orodha ya baadhi ya vitabu vya Agano Jipya. Marisiyo alilikataa Agano la kale lote na akamuona Mungu wa Agano la Kale kuwa ni mdogo kwa Yesu.  Kanoni ya Marsiyo iliundwa na vitabu 10 tu ambavyo ni nyaraka za Paulo (ukiondoa ambazo za kichungaji) na injili ya Luka. Vitabu  hivi alivifanyia masahihisho ili vielewane na ufundishaji wake uliokengeuka.

Ingawaje alikuwa muongo kuibuka kwa mafundisho ya uongo kulilifanya kanisa ligundue umuhinu wa kufafanua kanoni ya kweli ya Maandiko.

 

 

Mtawanyiko wa Kanuni Muratoriano unaorodhesha kanoni ya vitabu vya Agano Jipya. Mtawanyiko wa Muratoriano ambao ni maandishi ya kale sana katika miaka ya 200 Baada ya Kristo inayo orodha ya Kanoni kwa vitabu vya Agano Jipya.  Haisomeki yote kwa hiyo inaelezewa kama iliyotawanyika. Inavitambua vitabu vyote isipokuwa Waebrania, Yakobo, II Petro, na III Yohana.  

Lipo pia suala la I Petro ilivyotajwa au hapana. Imejumuisha pia kitabu kimoja kiitwacho Apokalipse cha Petro ambacho kilikataliwa baadaye kwa kutokuwa na Kanuni.

 

Tertuliano (160-221 Baada ya Kristo) anavyo vitabu 22 katika kanoni yake ya Agano Jipya inayohusu Injili nne, Matendo, nyaraka 13 za Paulo, I Petro, I Yohana, Yuda na Ufunuo. Hakukiona kitabu cha Waebrania kama chenye kanoni.

 

Origeni (185-254 Baada ya Kristo) alikiri Injili nne zenye kanuni, matendo, Nyaraka za Mtume Paulo na Waebrania, I Petro, I Yohana na Ufunuo kama vitabu visivyokuwa na upinzani.  Origeni alikiri kwamba Waebrania,  II Petro, II na III Yohana, Yakobo na Yuda ni vitabu visivyokuwa na upinzani.

 

 

Eusebio (260-340 Baada ya Kristo) anachukuliwa kama mwanahistoria wa kanisa.  Anatupatia taarifa kamili yenye maelezo ya nafasi ya kanisa kwa upana. Anaonesha tofauti muhimu kati ya homologoumena (vitabu vilivyokubaliwa) na antilegomena (vitabu vilivyopingwa).  Vitabu vilivyo kubaliwa ni zile Injili, Matrndo, Nyaraka za Paulo pamoja na Waebrania, I Petro, I Yohana, na Ufunuo.  Amevigawanya vitabu vilivyopingwa katika mafungu mawili madogo: (1) vile vinavyoelekea kufaa kuingizwa katika Kanoni - Yakobo, Yuda, II Petro, II na III Yohana (2) vile visivyoelekea kufaa kuingizwa katika kanoni — Matendo ya Paulo, Mchungaji wa Herimesi, Apokalipse ya Petro, Didisi, Barnaba.  Alihoji kuingizwa kwa ufunuo kutokana na wasiwasi wa kuhusika Mtume katika Uandishi wake.  Ukiacha kusita huku kwenye Ufunuo kwa Eusebio yeye katika Agano Jipya anafanana na la wakati wetu.

 

 

Atanasio (298-373 Baada ya Kristo), Atanasio amaorodhesha vitabu 27 vya Agano Jipya la wakati wetu.

 

Kanisa Katoliki la Roma linaingiza ndani vitabu 66 vya Biblia yetu na kukubali pia vitabu vya Apokraifa kama sehemu ya kanoni yao ya Maandiko. Hii ni kanoni ile ile ya Yerome aliyetengeneza Vulgeti ya Kilatini ambayo ni msingi wa Biblia ya Katoliki ya Roma.

 

 

Kanoni ya kweli imeundwa kwa vitabu 39 vya Agano la Kale na vitabu 27 vya Agano Jipya la Biblia.

 

 

Martini Lutheri aliorodhesha vitabu 27 vya Agano Jipya kama lilivyo isipokuwa vitabu vinne alivyoviona kama vyenye utata.  Aliweka Waebrania, Yakobo, Yuda na Ufunuo kwa utenganisho mwishoni mwa Agano Jipya.

Vipindi Saba Maalum katika Maandiko Matakatifu

I

II

III

IV

V

VI

VII

MWANZONI

VIONGOZI

WAKUU

WAFALME

WATAWALA WAGENI

 

UJIO WA KWANZA WA KRISTO

KANISA

UJIO WA PILI WA KRISTO

KUTOKA: Uumbaji

KUTOKA: Musa

KUTOKA: Saulo

KUTOKA: Kutekwa

KUTOKA: Uzalio wa Bikra

KUTOKA: Pentekoste

KUTOKA: Millenia

HADI: Musa

HADI: Paulo

HADI: Kutekwa

HADI: Kristo

HADI: Kupaa

HADI: Mateso

HADI:
Mbingu mpya & Dunia Mpya

VITABU: Mwanzo, Kutoka

VITABU: Kutoka, Walawi, Hesabu, Kumbukumbu, Yoshua, Waamuzi, Ruthu,

I Samweli

VITABU: I & II Samweli,

I & II Wafalme,

I & II Nyakati, Vitabu vya Manabii

VITABU: Ezra, Nehemia, Esta, Danieli, Ezekieli

VITABU: Mathayo, Marko, Luka, Yohana

VITABU:
Matendo Nyaraka

VITABU: Ufunuo