Sura ya 1: Maelezo ya Kawaida ya Biblia

Maelezo ya Msingi ya Biblia

BIBLIA  NI   NINI?

  • Biblia ni Ufunuo wa Mapenzi ya Mungu kwa wanadamu.
  •  

    Mungu hakuandika kitabu kingine zaidi ya Biblia. Hakuna ushahidi mwingine wowote wenye maelezo ya kina ya mapenzi ya Mungu na uwezo  wake zaidi ya Biblia. Ni kwa kusoma Biblia peke yake ndio tunaweza kuwa na majibu kuhusu maswali mengi yanayomhusu Mungu.

     

     

    Katika Biblia Mungu ameandaa maelezo ya habari za mapenzi yake na kuonyesha upendo wake kwa binadamu. Ufunuo mwingine wowote unapaswa kuoana na kitabu hiki cha ajabu. Ni kiwango cha uhai wote—wa muda mfupi na wa milele!

     

    (‘ya katikati’ kuu , kiongozi, dhamira ya msingi – mada, kama ya hotuba.)

     

     

    Mwanzoni Agano la Kale liliandikwa kwa Kiebrania (na asilimia ndogo kwa Kiarabu.) Agano Jipya liliandikwa kwa lugha ya Kigiriki. Toleo la Kingereza la Mfalme Yakobo ni tafsiri inayotokana na lugha hizi asilia. ‘Kutafsiri’ maana yake ni kubadilisha kutoka lugha moja kwenda katika lugha nyingine.

     

    Biblia ni kitabu kimoja, historia moja, na simulizi moja  HISTORIA YAKE [Historia ya Mungu]! Tunaiita Biblia TAKATIFU kwa sababu ni Neno la Mungu na siyo hadithi tu ya wanadamu. Neno TAKATIFU maana yake tukufu, safi, isiyo na lawama, au ya kidini, iliyotengwa. Biblia ni kitabu cha Kimungu ingawaje Mungu aliwatumia watu kuueleza ukweli wake Mtakatifu. Watu watakatifu (asili yake binadamu) waliandika kama walivyo himizwa na Roho Mtakatifu (Utukufu wa asili ya Mungu). Kwa kuwa ni Neno la Mungu hatuwezi tukatimiza wazo kwa kitabu au taarifa moja ya Biblia.

     

    Biblia inavyo vitabu 66, 39 katika Agano la Kale na 27 katika Agano Jipya. Utukufu wa Kimungu umefunuliwa katika Biblia kwa utaratibu kuanzia kitabu cha Mwanzo hadi mwisho wake katika Kitabu cha Ufunuo. Mwanzo ni kitabu kinachoonyesha asili; Ufunuo ni kitahu kinachohusu mwishoni. Vitabu vya Biblia vya katikati ni maneno ya Mungu ya uamsho kutoka katika ulimwengu ulioharibika. Kila kitabu cha Biblia kinao ujumbe wake, hata hivyo kitabu kizima kinakuwa na ujumbe wa wokovu wa mwanadamu ambao unaonekana. Inaweza kusemwa pia kwamba Agano la Kale ni taarifa ya taifa ( Israeli ) na agano jipya ni taarifa za mwanadamu (Yesu)

     

     

     

     

     

     

     

     

    Mwanzo 5:1- Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu.

     

    Zaburi 40:7- Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (katika gombo la chuo nimeandikwa, (Ebr. 10:7)

     

    Mathayo 1:1- Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, Mwana wa Ibrahimu.

     

    Luka 4:17- Akapewa chuo cha Nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa.

     

     

     

    II Wakorinto 3:14 – Ila fikra zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo.

     

    II Wakorinto 3:6 – Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa Roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

    Ufunuo 13:8 – Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana -  Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.

     

    Mpango wa Mungu toka mwanzo wa nyakati ni wa Yesu ambaye ni Kondoo wa Mungu kumwaga Damu Yake Takatifu kwa malipo ya ukombozi wetu.

     

     

     

     

    Mathayo 5:17 – Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; laa, sikuja kutangua bali kutimiliza.

     

    Kristo ndie mtu wa katikati katika Agano Jipya. Kristo ndiye mpatanishi wa Agano Jipya – Ebr. 12:24     

     

     

     

     

     

    Yohana 20:31— Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake.

     

     

     Yohana 5:39—Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia.

     

     

    Yohana 17:3—Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

     

    Yohana 14:23—… mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda …

    I Yohana 2:5—Lakini yeye alishikaye Neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika …

    Yohana 10:27—Kondo wangu waisikie sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.

    Yohana 12:26—Mtu akinitumikia, na anifuate

     

     

     

     Waefeso 5:27—Ili apate kujiletea kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

    II Timotheo 3:1—Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

     

     

    II Petro 1:19-21—Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi,  ambalo, mkiliangalia, kama taa ing’aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. 20. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. 21. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

     

     

     

    I Wakorinto 3:11—Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani,  Yesu Kristo.

     

    II Tim. 3:16—Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kuwaonya watu makosa yao, na kuwaongoza, na kuwaadibisha katika haki:

     

     

     

     

    Ifuatayo ni orodha ya sehemu muhimu za Biblia na maelezo mafupi kuhusu kilichotokea katika kila sehemu mojawapo. Kujifunza kwa moyo sehemu hizi na kujua kilichotokea katika kila sehemu mojawapo kutakupatia picha nzuri ya Biblia yote.

     

     

     

    MAHALI

    MAELEZO

    ANDIKO

    Edeni

    Mungu alimuumba mwanadamu na kumweka katika Bustani ya Edeni. Eneo la anguko la mwanadamu

    Mwanzo. 2:8

    Mlima Ararat

    Mahali safina ya Nuhu ilipokuja kusimama baada ya ile gharika.

    Mwanzo. 8:1-5

    Babeli

    Mnara uliojengwa kuifikia mbingu na Mungu akawafanya wanadamu waongee katika lugha tofauti.  Babeli maana yake mkanganyiko

    Mwanzo. 10:10; 11:4

    Uri wa Wakaldayo

    Mahali abrahamu alipoambiwa mwanzoni aende Kanaani. Nchi ambayo baadaye ilikuja kuitwa Babeli.

    Nehemia. 9:7

    Kanani

    Nchi ya ahadi ambayo walimoishi Abrahamu, Isaka na Yakobo. Yoshua aliiteka na kugawia kila kabila sehemu.

    Mwanzo. 12:5

    Misri

    Nchi Yusufu alikouzwa kuwa mtumwa.  Israeli ikadumu utumwani miaka 400. Musa aliitoa Israeli kutoka Misri.

    Mwanzo. 12:10

    Mlima Sinai

    Mahali Musa alipoona kichaka kinachowaka moto na baadaye akapokea sheria na agano.

    Kutoka. 19:11

    Nyikani

    Watoto wa Israeli walihangaika jangwani kwa miaka 40 kwa kutoamini kwao.

    Matendo 7:42

    Syria

    Mateka wa Israeli walipelekwa Syria.

    2 Fal. 18:11

    Babeli

    Mateka wa Yuda walipelekwa Babeli. Danieli alikuwa mmoja wao

    Danieli 1:1

     

     

    MAHALI

    MAELEZO

    ANDIKO

    Betlehemu

    Mahali pa asili—Kuzaliwa Kristo katika hori.

    Luka 2:7

    Galilaya

    Palistina iligawanywa katika mikoa mitatu, Yudea, Samaria, na Galilaya, ambayo ilijumuisha eneo lote la kaskazini la nchi (Mdo. 9:31), ambao ndio mkubwa zaidi.

    Luka 4:14

    Getsemane

    Mahali pa Kristo pa sala na aliposalitiwa na Yuda.

    Mat. 26:39

    Golgota

    Mahali Kristo aliposulubiwa. “Mahali pa fuvu la kichwa.”

    Marko 15:22-28

    Yerusalemu

    Huitwa pia: Salemu, Arieli, Yebusi, "Mji wa Mungu,"  "mji mtakatifu;" wakati fulani "Mji wa Yuda" Mahali lilipozaliwa kanisa la Agano Jipya.

    Mdo 1:8 (2:25,28)

    Samaria

    Samaria mkoa ulioko katikati ya Palestina lakini hauchukuliwi kama nchi takatifu. Umbali kati ya Samaria na Israeli ambayo ni mji mikuu ya falme mbili ni maili 35 tu katika mstari ulionyooka.

    Yoh. 4:1-5

     

    Mungu— Biblia inatueleza kwamba Mungu ni roho (Yohana 4:24).  Mungu ni Roho nao wamuabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli (Strong) Mungu ni zaidi ya mtendaji katika Biblia; Mungu ni chimbuko la kila kiumbe.  Biblia inamfunua Mungu kwa mwanadamu.

    Shetani—Neno shetani maana yake anayeshtaki. Yeye ndiye anayeshtaki kati ya wanaoamini. –  Ufunuo 12:10. Shetani huitwa pia muovu.  Mungu hakumuumba muovu.  Mungu alimuumba malaika Lusiferi ambaye alianguka kwa sababu ya dhambi akawa muovu. – Isaya. 14:12, Lk.10:18.

     Adamu— Mungu alimuumba Adamu, mwanadamu wa kwanza, akamuweka katika Bustani ya Edeni.  Ni yeye ndiye aliyeingiza dhambi katika jamii ya wanadamu. – Rum. 5:12

    Eva—Mungu alimuumba Eva, mwanamke wa kwanza, kutokana na ubavu mmoja wa Adamu. – Mwanzo 2:21-22

    Kaini— Mwanaye Adamu wa kwanza. Alikuwa mkulimaAlimuua nduguye Abeli na kuwa muuaji wa kwanza. – Mwa. 4;1

    Abeli—mwanaye Adamu wa pili aliyeuawa na Kaini. Alikuwa mchungaji. Mwa. 4:2

    Seti—Mwanae Adamu wa tatu. -  Mwa. 5:3

    Nuhu—Alijenga safina kulinda uhai katika dunia. Mwa. 6:13-22

    Abram—Mungu alimwita Abram aondoke nyumbani na kwenda katika nchi isiyojulikana ambako Mungu atamfanya baba wa taifa kubwa, ndio historia ya Wayahudi ikaanza. Mwa. 12:1-3 Mungu alibadili jina lake kutoka Abram Baba Mkubwa kuwa Abrahamu  Baba wa Umati. Mwa. 17:5

    Isaka—Mwanaye Abrahamu wa agano aliyempata kwa ahadi uzeeni. Mwa. 17:19

    Yakobo—Jina lake lilibadilishwa na Mungu likawa Israeli. Wanae 12 ndio waliounda makabila ya taifa la Israeli. Mwa. 32:28

    Yusufu— Mwanaye Yakobo ambaye aliuzwa utumwani Misri.  Mungu alimpandisha cheo hadi nafasi ya pili katika ufalume na akamtumia kuilinda Misri na Israeli.  Yakobo na familia yake walihamia Gosheni wilaya iliyoko Misri. Mwa. 37:36,42:1-3.

    Farao—Cheo cha mtawala wa Misri. Watoto wa Israeli walikuwa utumwani Misri kwa miaka 400. Mungu aliufanya moyo wa Farao aliyetawala wakati wa Kutoka kuwa mgumu na akawaondoa Waisraeli kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu. Kut. 1:11-14, 6:1

    Musa— Mungu alimwinua Musa kwenda kuwatoa utumwani Misri wana wa Israeli.  Alipokea amri zake na agano katika mlima Sinai.  Aliwaongoza Waisraeli kwa miaka 40.  Kut. 3:10-12

    Aroni—Ndugu yake Musa na Kuhani Mkuu kwa utaratibu wa Makuhani. Kut. 28:1-3

    Kalebi—Mmojawapo wa wapelelezi aliowatuma Musa wakamletea taarifa nzuri. Nu. 13:30

    Yoshua—Aliteuliwa na Mungu kuwa mrithi wa Musa.  Yoshua aliwaongoza Waisraeli wakaishinda Kanani. – Nu. 27:18-23

    Waamuzi—Walikuwepo Waamuzi 15 waliotawala Israeli baada ya kifo cha Yoshua.  Hili ni jina la kitabu kimojawapo katika Agano la Kale

    Ruthu—Wamoabi ambao walirudi Betlehemu pamoja na Naomi mume wake alifia Moabu kabla Naomi hajarudi Betlehemu.  Ruthu aliolewa na Boazi akawa mmoja katika uzao wa mstari wa Kristo.  

    Samweli—Aliitwa akiwa kijana na akawa mmoja wa manabii wakuu wa Israeli. I Sam. 3:20

    Saulo—Mfalume wa kwanza wa Israeli. I Sam. 15:1

    Daudi—Kijana mchungaji aliyemuua Goliati. Mungu alimteua kuwa mfalume wa Israeli badala ya Saulo. II Sam. 5:3-12

    Solomoni—Mwanae daudi na mrithi wa ufalme wake. Mungu alimruhusu achague chochote apendacho. Yeya aliomba moyo mnyoofu na Mungu alimfanya awe na busara kuliko binadamu yeyote.  Alijenga hekalu lililojulikana kama Hekalu la Solomoni. I Fal. 3:5-12

    Eliya—Nabii shupavu wa Mungu. Aliilaani Israeli ikapigwa na ukame kwa sababu ya dhambi. Aliomba moto ushuke kutoka mbinguni katika mapambano yake na manabii wa baali katika mlima Karmeli. Alishinda kifo na alipanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli.

    II Fal. 2:11

    Elisha— Mtumishi wa Eliya.  Aliyechaguliwa na Mungu achukue nafasi yake kama nabii wa Israeli. I Fal. 19:16

    Isaya—Alimuona Bwana ameketi katika kiti cha Enzi kilicho juu sana na kuinuliwa sana na pindo za vazi lake zikalijaza Hekalu. Nabii aliyeonya Taifa la Israeli kutubu vinginevyo hukumu ya Mungu italiangukia. – Isaya. 6:1

    Yeremia—Aliitwa kuwa nabii wa Mungu akiwa tumboni kwa mama yake.  Alielezewa kama Nabii aliaye aliyeshinda dhambi za Israeli. – Yer.. 1:5

    Ezekieli—Alitabiri kutekwa kwa Yerusalemu kwa sababu ya dhambi zao. –Eze. 3:4

    Danieli—Alichukuliwa na Nebukadneza kama mmojawapo wa mateka ya Yerusalemu. Alitafsiri ndoto ya Nebukadneza na kuelezea kuzuka kwa Himaya nyingi. Alipokea maono ya siku za mwisho na alikuwa mashuhuri katika himaya za Babeli na Persia – Dan. 1:6

    Ezra—Kuhani na Mwandishi aliyerudi Yerusalemu kulijenga tena Hekalu. – Ezra 7:6

    Nehemia—Alikuwa mbeba kikombe aliyerudi Yerusalemu na kuwa kiongozi katika ujenzi mpya wa Hekalu. – Imeelezwa katika kitabu cha Nehemia.

    Esta—Malikia wa Ahesueru ambaye alikuwa mfalme katika mkoa wa Persia.  Alitimiwa na Mungu kusimamisha njama za kuwaangamiza watu wake ambao ni Wayahudi. Imeelezwa katika kitabu cha Ester

     

     

    Yohana Mbatizaji—Aliyemtangulia Kristo.  Alibatiza wale waliotubu dhambi zao katika mto Yordani. Mt. 3:5-6

     Yesu Kristo—Mwana pekee wa Mungu. Mhusika Mkuu katika Agano Jipya. Agano jipya lote kwa kipekee linaweka katikati kazi za Kristo duniani, lakini Biblia kwa ujumla wake inaonyesha kwamba inamhusu kwa njia moja au nyingine.

    Wafuasi 12 – Waliitwa na kufundishwa na Yesu; Kwamba watakuwa viongozi wa kanisa katika Agano Jipya. 1) Petro, 2)Andrea ndugu yake Petro 3)Yakobo mwanaye Zebedayo 4)Yohana ndugu yake Yakobo 5)Filipo, 6)Bartolomeo 7)Tomaso 8)Matayo  aliyekuwa mtumishi 9)Yakobo mwanaye Alfayo 10)Tadei 11)Simoni wa Kanani, na 12)Yuda Iskarioti.

    Stefano—Mmoja wapo wa wale Mashemasi saba wa Kanisa waliochaguliwa kwanza katika Yerusalemu na kutofautishwa kati yao kama "mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu."  Alipigwa mawe hadi kufa chini ya utawala wa Sanhedrin ambao Saulo wa Tarso alikuwa mwanachama wake. Kifo cha Stefano ilikuwa ni mwanzo wa mateso makali kwa juhudi zilizoongozwa na Saulo, ambazo zilisababisha kuenea zaidi kwa Neno la Mungu.

    (Mdo. 8:1,4; 11:19-21)

    Philipo—Shemasi na Mwinjilisti (Mdo. 6:5; 21:8; Efe. 4:11). Alikuwa na watoto wa kike wanne waliojaliwa kipaji cha unabii (Mdo. 2:17; 21:8-9).  Baada ya kifo cha Stefano alihubiri injili toka Samaria na kwa towashi Mhabeshi kwa mafaniko makubwa na kukawepo na miujiza mingi.

    Paulo—Aliinuliwa kuwa Mtume wa Mataifa. Alikuwa chombo cha kibinadamu kilichofikisha sehemu kubwa ya Agano Jipya kwa mataifa.  Mdo. 9:15

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

     

    Waraka ni barua. Hizi ni barua zenye pumzi ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya Kanisa.

     

     

     


    Revision #8
    Created 7 September 2022 15:14:36 by Stephen Reynolds Jr
    Updated 7 September 2022 16:45:42 by Stephen Reynolds Jr