# Sura ya 4: Kanoni za Biblia

 

Kuorodheshwa kwa vitabu vya  Biblia

 

Mchakato wa ukusanyaji wa vitabu vya Biblia katika mfumo wake wa sasa ndio kunakoitwa: kuorodheshwa kwa vitabu vya Biblia. Jambo hii halikufanyika kwa siku moja.  Ikumbukwe kwamba kila kitabu kimoja ilibidi kiandikwe kwa mkono na kwa umakini mkubwa.  Vitabu hivyo vilitumiwa na kusambazwa na viongozi wa dini wa siku hizo.  Kulikuwepo pia vitabu vingine vilivyodai kuwa na uvuvio ambavyo havikuingizwa katika Biblia. Kulikuwepo na vitabu vya dini na historia ambavyo vilikuwa vinasambazwa wakati wa kuamua ni vitabu gani viingizwe katika Orodha hiyo. Mchakato huu wa kutambua vitabu vyenye uvuvio na vipi havina ndio jambo tutakaloangalia katika somo la sehemu hii.  Tutajaribu pia kulijibu swali: Biblia iliwezaje kufikia katika hali iliyo nayo sasa?

 

 

 

 

 

 

Ni Kigezo gani kilitumika kuamua vitabu gani viingizwe katika Biblia na vitabu vipi visiingizwe katika orodha ya Maandiko Matakatifu?  Hili ni swali muhimu ambalo inabidi lipatiwe majibu na mwanafunzi makini wa Biblia.  Uanapaswa kufahamu bila shaka yeyote kwamba  Biblia katika mfumo wake wa sasa ndio NENO LA MUNGU LENYE UVUVIO

 

 

 

 

Mabaraza ya dini hayakuamua vitabu vya kuorodheshwa katika Biblia.  Mabaraza ya wanadamu hayawezi kufanya kitabu kuwa Andiko Takatifu ambacho katika asili yake siyo maandiko matakatifu.

 

 

 

 

Hali hii ndio inayosemekana kwamba ni sababu pekee ya umoja na uelewano wa Maandiko Matakatifu. Ubishi ni kwamba wanadamu waliondoa vitabu ambavyo havikukubaliana na maoni yao na kuingiza vile ambavyo vilikubaliana na maoni yao.  Maoni haya ya yongo humuweka mwanadamu katika nafasi ya uamuzi wa orodha ya kanoni.

 

 

Mungu alimpatia mwanadamu vitabu ambavyo alitaka viingizwe katika Biblia.  Mungu alilinda na kuhifadhi vile vitabu alivyovivuvia na kuvitunza hadi wakati wa kuviweka katika orodha ya Biblia.

 

 

Kitabu kiliweza kuingizwa katika Kanoni  kwa sababu ya kutambuliwa kwake kuwa na Uvuvio wa Wakiungu wa Neno la Mungu. Kitabu ambacho kilionekana kutokuwa na Mamlaka ya Kiungu hakikuingizwa katika Biblia kama sehemu ya  kanoni ya Maandiko Matakatifu.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Kumbukumbu 31:24-26—Basi ikawa hapo Musa alipomaliza kuandika maneno ya Torati hii katika Chuo, hata yakaisha, 25 ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la Agano la BWANA akawaambia, 26 Twaeni chuo hiki cha Torati, mkiweke kando la agano la BWANA, Mungu wenu, ili kiwepo kama shahidi juu yako.

Sheria iliwekwa kama muongozo kwa Makuhani ili kuitunza pamoja na lile Agano. Makuhani hao waliagizwa kuisoma Sheria kila miaka saba.

 

 

 

 

Mathayo 5:18—Kwa maana Amini, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya Torati haitaondoka, hata yote yatimie.

 

 

  Waandishi wa Kiyahudi walinakili kwa uangalifu mkubwa na kuhifadhi maandishi ya Agano la Kale.  Augustino alisema, waandishi wa Kiyahudi walikuwa ni Wakutubi wa kanisa la Kikristo. Waandishi wa mwanzo kabisa kati ya hawa waliitwa Tannaim (walimu) walinakili maandishi ya Agano la Kale kwa usahihi mkubwa. Watannaim walifuatwa kwa hadhi na kikundi cha waandishi walioitwa Amoraim (wafichuaji). Hawa walikuwa ni wasomi waliofanya kazi siyo kama wa kunakili tu, bali walizalisha pia ile Talmud ambayo ni kitabu kinachoweka hadharani sheria na mila za Wayahudi.

 

 

 

 

Walimu (Rabi) wa Kiyahudi waliziweka nakala za Maandiko Matakatifu katika heshima ya hadhi ya juu.  Wakati andiko lolote lilipo zeeka au kuchujika na kuonekana halifai kwa matumizi lilipumzishwa kwa heshima kuu.  Iliaminika kwamba ni bora zaidi kuzizika kwa heshima kuliko kuthubutu kuziacha ziangukue mikono isiyofaa au kudharauriwa. Hii ndio sababu ya kuwepo nakala nyingi za Agano la Kale zilizoandikwa.

 

 

 

 

 

Yapo majaribio yaliyotumiwa na viongozi wa Wayahudi ili kuamua kanoni ya kitabu misingi hii ilizingatia walichotaka waandishi wa historia ya Biblia na kanisa.  Ulikuwepo mfumo maalumu wa kuangalia utambuzi wa kanoni ya kitabu.  Sehemu hii inataja waandishi wa kanoni za vitabu vya Biblia. Maelekezo haya ni kuhusu ukweli kwamba walikuwa ni vyombo vya kibinadamu  vya mwandishi wa kiungu.

 

Uandishi wa Musa wa kitabu ulichukuliwa kama jaribio halali la uvuvio na Wayahudi tangu zamani. Musa anatajwa kama nabii mkuu wa Wayahudi. Vitabu ambavyo viliandikwa na Musa vinachukuliwa kama vyenye asili ya Mungu kutoka mwanzoni kabisa mwa taarifa za historia ya Wayahudi.  Ushahidi wa akiolojia wa Palestina unaimarisha sana mtazamo huu wa kitamaduni.  Yesu alithibitisha kwamba Musa ndiye chombo cha kibinadamu kilichopokea ile Sheria. Musa hakuwapa torati? – Yoh. 7:19. Kama tunavyofahamu taarifa iliyoandikwa katika Biblia inaonesha kukubalika mara moja kwa vitabu vya sheria kama vilivyotolewa na Mungu.

 

Iwapo kitabu hicho kiliandikwa na nabii wa Mungu anayejulikana ambaye alifikiriwa kama mwaguzi wa Mungu; kitabu hicho kiliaminiwa kuwa ni Neno la Mungu.

 

Mwandishi alichukuliwa kuwa mtu wa Mungu iwapo alionesha ushahidi wa nguvu za Mungu katika maisha yake.  Kama mwandishi alichukuliwa kama mtu wa Mungu na maandishi yake pia yaliaminika kwamba yametoka kwa Mungu. Watoto wa manabii walitambua mamlaka ya Elisha walipomuona amechukua nafasi ya Eliya na kuutenganisha mtu Yordani. – II Fal 2:15.

 

Ni lazima kuwepo umoja kamili wa Maandiko.  Kanuni katika sehemu moja ya Maandiko ni lazima ielewane na ukweli ulioko katika sehemu nyingine za Maandiko. Kama ilivyokwisha tamkwa wengine watabisha kwamba vitabu vilivyochaguliwa ni vile vinavyopatana na maoni ya viongozi ambao walivichagua.  Hata hivyo kitabu kisingeweza kuhesabika kama cha Kanoni iwapo isingekuwa kinakubaliana na Maandiko mengine yaliyopokelewa.  Kitabu kilitambuliwa kuwa cha Kanoni kwa sababu ya kuwa na uvuvio.  Jambo hili kama tunavyoweza kuona siyo jaribio pekee la kuthibitisha kanoni ya kitabu.  Ni wazi kwamba Kitabu chenye asili ya Mungu hakitapingana na kitabu kingine chenye asili ya Mungu.

   

Ni lazima kitabu kiwe sahihi katika maelezo yake kumhusu Mungu na kuhusu vitu vya Mungu.  Kitabu hicho kitakaliwa kwa kutokuwa na uvuvio iwapo kutakuwa na makosa kuhusu teolojia.

 

Baadhi ya vitabu vilikubaliwa na viongozi wa Wayahudi kama vya kanoni na vingine vilikataliwa.  Huu ni ushahidi kwamba viongozi wa Kiyahudi walitambua vitabu hivyo ambavyo viliingizwa katika Kanoni kama Maandiko yenye mamlaka.

 

 

 

Luka 24:44—… ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na

katika Manabii na Zaburi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 “hatupaswi kulionyesha kama ni chimbuko la Erasmo la ‘maandishi yaliyopokelewa’ bali kama muendelezo wa kutoka kwenye maandishi ya mkono iliyozooeleka jinsi ilivyopokelewa kwenda kwenye mfumo wa kuchapisha, ambao uliendelea kuwepo kwa karne tatu.” – Kenneth W. Clark, msomi wa Maandishi ya Kiyunani  (msisitizo umeongezwa)

 

 

Mathayo 24:35—Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

 I Petro 1:23—Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili si kwa mbegu iharibikayo bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima lidumulo hata milele.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Yalikuwepo majaribio ambayo yalitumiwa na kanisa la mwanzo kuamua kuwepo kwa kanoni katika kitabu. Walikuwepo viongozi wa kanisa waliohusika kwa wakati mbalimbali ambao waliamua ni vitabu gani vyenye uvuvio na visivyokuwa nao.  Ifuatayo ni miongozo mnne iliyotumiwa na viongozi hawa katika ugunduzi wao wa kanoni ya Agano Jipya.

 

 

Tunaelewa kwamba Mungu ndiye mwandishi wa Agano Jipya.  wale Mitume walikuwa ni baadhi ya watu watakatifu wa Mungu ambao kwa Utukufu wake Mwandishi aliongea kuwapitia wao.  Kama kitabu kiliweza kuthibitishwa kuandikwa na mmoja wa wale mitume wa mwanzo wa Yesu kilichukuliwa kama chenye asili ya Mungu.  Uzito mkubwa uliwekwa katika ufundishaji na maagizo ya mitume wale wa mwanzo. Maandiko yaliyowahusu wao yalisambazwa kati ya jamii za Kikristo za kwanza kabisa.

 

Iliaminika kwamba wale mitume wa kwanza walifahamu zaidi ni vitabu vipi vyenye uvuvio na ni vipi visivyokuwa nao. Kitabu ambacho hakikuandikwa na mtume ambacho kilikuwa na idhini ya Kitume kilichukuliwa kuwa na asili ya Mungu.  

 

Vipo vitabu fulani ambavyo vilikubaliwa haraka na kanisa la mwanzo kuwa Maandiko yenye Utukufu wa Mungu.  Vitabu hivi viliingizwa mara moja katika Kanuni. Kulikuwepo na vitabu vingine ambavyo vilichukua muda kukubaliwa na kanisa kuwekwa katika orodha ya kanoni.

 

 

Tunayo taarifa ya kihistoria kutoka kwa viongozi wa mwanzo wa kanisa zinazoonesha kwamba ni vitabu gani vilisomwa katika makusanyiko ya kanisa.  Vitabu hivi vilitumiwa na kanisa kwa sababu vilichukuliwa kama vyenye uvuvio.

 

 

Kama ilivyokwisha tamkwa kuhusu kukubaliwa kwa Maandiko ya Agano la Kale kwamba ni lazima kitabu kioane vizuri na vitabu vingine vyenye kanoni iliyokwisha kubalika. Pamoja na hayo, vitabu vya Agano Jipya ambavyo vilipokelewa vinapaswa kuwa na uwiano na kanoni ya Agano la Kale na kanoni ya Agani Jipya ya Maandiko Matakatifu.    

 

Vitabu 20 kati ya 27 vya Agano Jipya vilikubalika mara moja na vikapokelewa ulimwenguni pote kuwa asilia na kuitwa Homologoumena.  Vitabu hivi  20  ni zile Injili nne, Matendo, Nyaraka za Paulo (isipokuwa Waebrania), na nyaraka za kwanza za Yohana na Petro.

 

Vitabu vile saba vya Waebrania, II Yohana na III, II petro, Yuda, Yakobo, Ufunuo vilipingwa kwa kipindi fulani na kuitwa Antilegomena.  Yalikuwepo maswali kadhaa kuhusu vitabu vilivyoitwa Antilegomena.  Moja ya maswali hayo ni lile la kwamba viliandikwa kweli na wale watu wanaoitwa waandishi wake. Waebrania kilikuwa hakina jina la mwandishi wake na kilitofautiana na mwelekeo wa nyaraka za Paulo uliofahamika; II Petro ilikuwa na tofauti na I Petro; Yakobo na Yuda walijiita watumishi; na siyo mitume; mwandishi wa II Yohana na III Yohana alijiita mzee na siyo mtume. Uandishi wa kitume ulichukuliwa kama kigezo muhimu katika kutambua kanoni ya kitabu. Yalikuwepo maigizo mengi yaliyodai mamlaka ya kitume, kwa hiyo vitabu hivi vilichunguzwa kwa makini kabla ya kuingizwa katika kanoni.

Swali lingine ni kwamba Yuda aliandika taarifa ambazo hazijatajwa mahali pengine katika Maandiko na anamtaja Henoko jambo ambalo lilihusishwa na Apokrifa.  Kitabu cha Ufunuo hakikueleweka kwa viongozi wengi wa kanisa kwa hiyo kikazua maulizo katika akili zao. Vitabu hivi havikukubalika mara moja na kuwekwa mahali pake katika kanoni. Baada ya kuchunguzwa kwa makusudi mwishoni vilipokelewa kama halisi, na ucheleweshaji wake ukathibitisha uchunguzi ambao ulitumika katika mchakato wa kuviweka kanoni. Mwanzoni mwa karne ya nne vilipokelewa katika makanisa mengi na mwishoni mwa karne hiyo vikapokelewa na makanisa yote.

 

 

 

 

 

 

Kanuni ya Kiyahudi inaundwa na vitabu 39 vya Agano la Kale.

 

 

 

Marisiyo ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kutengeneza orodha ya baadhi ya vitabu vya Agano Jipya. Marisiyo alilikataa Agano la kale lote na akamuona Mungu wa Agano la Kale kuwa ni mdogo kwa Yesu.  Kanoni ya Marsiyo iliundwa na vitabu 10 tu ambavyo ni nyaraka za Paulo (ukiondoa ambazo za kichungaji) na injili ya Luka. Vitabu  hivi alivifanyia masahihisho ili vielewane na ufundishaji wake uliokengeuka.

Ingawaje alikuwa muongo kuibuka kwa mafundisho ya uongo kulilifanya kanisa ligundue umuhinu wa kufafanua kanoni ya kweli ya Maandiko.

 

 

Mtawanyiko wa Kanuni Muratoriano unaorodhesha kanoni ya vitabu vya Agano Jipya. Mtawanyiko wa Muratoriano ambao ni maandishi ya kale sana katika miaka ya 200 Baada ya Kristo inayo orodha ya Kanoni kwa vitabu vya Agano Jipya.  Haisomeki yote kwa hiyo inaelezewa kama iliyotawanyika. Inavitambua vitabu vyote isipokuwa Waebrania, Yakobo, II Petro, na III Yohana.  

Lipo pia suala la I Petro ilivyotajwa au hapana. Imejumuisha pia kitabu kimoja kiitwacho Apokalipse cha Petro ambacho kilikataliwa baadaye kwa kutokuwa na Kanuni.

 

Tertuliano (160-221 Baada ya Kristo) anavyo vitabu 22 katika kanoni yake ya Agano Jipya inayohusu Injili nne, Matendo, nyaraka 13 za Paulo, I Petro, I Yohana, Yuda na Ufunuo. Hakukiona kitabu cha Waebrania kama chenye kanoni.

 

Origeni (185-254 Baada ya Kristo) alikiri Injili nne zenye kanuni, matendo, Nyaraka za Mtume Paulo na Waebrania, I Petro, I Yohana na Ufunuo kama vitabu visivyokuwa na upinzani.  Origeni alikiri kwamba Waebrania,  II Petro, II na III Yohana, Yakobo na Yuda ni vitabu visivyokuwa na upinzani.

 

 

Eusebio (260-340 Baada ya Kristo) anachukuliwa kama mwanahistoria wa kanisa.  Anatupatia taarifa kamili yenye maelezo ya nafasi ya kanisa kwa upana. Anaonesha tofauti muhimu kati ya homologoumena (vitabu vilivyokubaliwa) na antilegomena (vitabu vilivyopingwa).  Vitabu vilivyo kubaliwa ni zile Injili, Matrndo, Nyaraka za Paulo pamoja na Waebrania, I Petro, I Yohana, na Ufunuo.  Amevigawanya vitabu vilivyopingwa katika mafungu mawili madogo: (1) vile vinavyoelekea kufaa kuingizwa katika Kanoni - Yakobo, Yuda, II Petro, II na III Yohana (2) vile visivyoelekea kufaa kuingizwa katika kanoni — Matendo ya Paulo, Mchungaji wa Herimesi, Apokalipse ya Petro, Didisi, Barnaba.  Alihoji kuingizwa kwa ufunuo kutokana na wasiwasi wa kuhusika Mtume katika Uandishi wake.  Ukiacha kusita huku kwenye Ufunuo kwa Eusebio yeye katika Agano Jipya anafanana na la wakati wetu.

 

 

Atanasio (298-373 Baada ya Kristo), Atanasio amaorodhesha vitabu 27 vya Agano Jipya la wakati wetu.

 

Kanisa Katoliki la Roma linaingiza ndani vitabu 66 vya Biblia yetu na kukubali pia vitabu vya Apokraifa kama sehemu ya kanoni yao ya Maandiko. Hii ni kanoni ile ile ya Yerome aliyetengeneza Vulgeti ya Kilatini ambayo ni msingi wa Biblia ya Katoliki ya Roma.

 

 

Kanoni ya kweli imeundwa kwa vitabu 39 vya Agano la Kale na vitabu 27 vya Agano Jipya la Biblia.

 

 

Martini Lutheri aliorodhesha vitabu 27 vya Agano Jipya kama lilivyo isipokuwa vitabu vinne alivyoviona kama vyenye utata.  Aliweka Waebrania, Yakobo, Yuda na Ufunuo kwa utenganisho mwishoni mwa Agano Jipya.

Vipindi Saba Maalum katika Maandiko Matakatifu

I

II

III

IV

V

VI

VII

MWANZONI

VIONGOZI

WAKUU

WAFALME

WATAWALA WAGENI

 

UJIO WA KWANZA WA KRISTO

KANISA

UJIO WA PILI WA KRISTO

KUTOKA: Uumbaji

KUTOKA: Musa

KUTOKA: Saulo

KUTOKA: Kutekwa

KUTOKA: Uzalio wa Bikra

KUTOKA: Pentekoste

KUTOKA: Millenia

HADI: Musa

HADI: Paulo

HADI: Kutekwa

HADI: Kristo

HADI: Kupaa

HADI: Mateso

HADI:
Mbingu mpya & Dunia Mpya

VITABU: Mwanzo, Kutoka

VITABU: Kutoka, Walawi, Hesabu, Kumbukumbu, Yoshua, Waamuzi, Ruthu,

I Samweli

VITABU: I & II Samweli,

I & II Wafalme,

I & II Nyakati, Vitabu vya Manabii

VITABU: Ezra, Nehemia, Esta, Danieli, Ezekieli

VITABU: Mathayo, Marko, Luka, Yohana

VITABU:
Matendo Nyaraka

VITABU: Ufunuo