Kanisa la Baada ya Kisasa
Saba: Kanisa la Baada ya Kisasa (1950—leo)
Kuanzia mwaka wa 1950 wa Kristo hadi leo
Kanisa linaendeshwa kwa sanduku la kura
Laodeshia maana yake utawala wa watu wenyewe. Makanisa mengi ya leo yanaendeshwa na watu wenyewe. Jina la kipindi hiki linaelezea serikali ya kisasa. Kanisa haliongozwi tena na Mungu ila linaendeshwa na watu ambao wanafanya mambo kwa njia zao binafsi watakavyo.
Kanisa la karisma
Kuna upako wa mafuta wakilaghai (Mat. 24:5)
Yesu alikwishaonya kwamba watatokea waongo watakaojiita Kristo katika siku za mwisho. Neno Kristo maana yake mpakwa mafuta. Siku hizi wapo wapakwa mafuta wengi wa uongo wasiokuwa na uhusiano wowote na Mungu.
Wapo manabii wa uongo (Mat. 24:11, 24)
Yesu alisema watakuwepo manabii wa uongo ambao watadanganya wengi. Kati ya wanakarismatiki wa siku hizi kuna manabii wengi wa uongo. Wanaondoa tendo la upako wa mafuta unaofanywa na Roho Mtakatifu.
Vuguvugu la ukarismatiki lilianzia ndani ya Kanisa Katoliki
Kanisa la anasa na rushwa
Injili ya mafanikio imeshaiondoa injili ya Yesu Kristo katika makanisa mengi ya kisasa
Wahubiri wengi wa injili wa kisasa wanafundisha mambo ya mafanikio wa kupata fedha na faida nyingine. Watu wanashauriwa kwa maneno kama, "Otesha mbegu yako kwa mategemeo ya kujipatia mavuno makubwa." Wanaambiwa wakitoa watabarikiwa mara mia. Wanaambiwa watamke watakavyo wabarikiwe.
No Comments