Skip to main content

Vipindi saba vya historia ya kanisa

Vipindi saba vya historia ya kanisa

KANISA LA KITUME

MWANZO: Tangu siku ya Pentekoste (30 BK)

MWISHO: Hadi kukamilishwa kwa Agano Jipya kwenye (100 BK)

KANISA LA MATESO

MWANZO: Kuanzia kukamilishwa Agano Jipya kwenye (100 BK)

MWISHO: Hadi kutolewakwa Hati ya Konstantino (313 BK)

Hiki ni kipindi cha mateso makuu kwa kanisa. Kanisa liligandamizwa mno chini ya Ufalme wa Kirumi.

KANISA LA KIFALME

MWANZO: Kuanzia kutolewa kwa Hati ya Konstantino (313 BK)

MWISHO: Hadi anguko la Roma (476 BK)

Neno la Ufalme linahusiana na mfalme au mtawala. Hiki ni kipindi ambacho mfalme alikuwa na ushawishi mkubwa sana ndani ya kanisa.

KANISA LA ZAMA ENZI ZA KATI

MWANZO: Tangu anguko la Roma (476 BK)

MWISHO: Hadi anguko la Konstatinopo (1453 BK)

Wakati huu kanisa Katoliki lilikuwa na mamlaka makubwa katika bara la Ulaya.

KANISA LILILOTENGENEZWA

MWANZO: Tangu anguko la Konstantinipo (1453 BK)

MWISHO: Hadi mwisho wa vita vya miaka 30 (1678 BK)

Huu ni wakati ambao Mungu aliwatumia watu kama Martin Luther kusimamia nakupigana na wimbi la ukatoliki na walihubiri kwamba wenye haki wataishi kwa imani yao. Mungu aliamsha wanaume katika eneo lote la Ulaya ili walirudishe Neno la Mungu kanisani.

KANISA LA KISASA

MWANZO: Kuanzia mwisho wa vita ya miaka 30 (1678 BK)

MWISHO: Hadi katika karne ya ishirini (Miaka ya 1950 BK)

Hiki ni kipindi cha uamsho wa hali ya juu na umisionari ulienea sehemu nyingi. Hadi kufikia kipindi hiki kulikuwa hakuna jitihada mahususi zilizofanyika za kuieneza Injili duniani kote. Wakati huu ndio David Livingstone alianzisha vituo vingi vya umisionari katika bara la Afrika.

KANISA LA BAADA YA KISASA

MWANZO: Kwanzia karne ya ishirini (Miaka ya 1950 BK)

MWISHO: Hadi siku yaleo

Tutasoma kila kipindi katika vipindi hivi 7 peke yake. Sura hii ilikuwa ni muhtasari tu wamafunzo yatakayo fundishwa.