Skip to main content

Kanisa la Kisasa

Sita: Kanisa la Kisasa (1678–c. 1950 BK)

Kuanzia mwisho wa vita ya miaka thelathini ya mwaka 1678 hadi miaka ya 1950.

Uamsho Mkubwa (wa miaka ya 1700)

Uamsho mkubwa unahusishwa nakuanzishwa upya jitihada za kuieneza injili Uingereza na Marekani.

Georgi Whitefield (1714–1770)

Bwana Whitefield ambaye alikuwa mhubiri shupavu wa injili iliyokuwa katika lugha rahisi tangu akiwa naumri wa miaka 24, alipingwa marufuku kuhubiri katika kanisa la Anglikana. Aliamua kufundisha mitaani na kufanya viwanja vya wazi kuwa mahali pake pa salana akahubiria maelfu ya watu. Huu ulikuwa mwanzo wa uamsho katika maeneo ya Magharibi ya Uingereza. Alihubiri Uingereza na Marekani.

Yohane Wesley (1703–1791)

Dunia ilikuwa ndio parokia yake. Aliwahubiria watu kwa maelfu katika maeneo ya wazi. Alihubiri kote Uingereza na Marekani akianzia katika makanisa kadhaa. Yeye ndiye mwanzilishi wa Kanisa la Methodisti.

Jonathani Edwardi (1703–1758)

Alikuwa mchungaji eneo la Northampton, Massachusetts akiwa na umri wa miaka 17. Mwaka 1741 alisoma hotuba yake maarufu yenye kichwa cha habari "Watenda dhambi wakiwa mikononi mwa Mungu aliyekasirika" mbele ya waumini wake. Imani ya ajabu iliwapata waumini wake kiasi kwamba walihubiri na kuongoza uamsho ulioenea Uingereza yote mpya.

Kuzinduka kwa ajabu kwa mara ya pili (miaka ya 1820)

Huu ulikuwa ni muondoko mwingine wa Mungu wa kuwasha moto wa matumaini uliosambaa hadi Uingereza.

Charles Finney alikuwa mstari wa mbele katika kuwasha moto wa uamsho mkubwa huko Marekani

Katika miaka ya mwanzoni ya 1820 Finney alihubiri katika mikutano ya injili huko New York ambayo iliwasha moto wa uamsho kwa mara ya pili. Finney alikuwa ni mtu wa imani kali na mwinjilishaji shupavu wa neno la Mungu. Finney ameelezewa mara nyingi kama mwinjili anayeongoza wengine wote wa kutoka Amerika.

D. L. Moody

Moody aliitetemesha Marekani na Uingereza kwa ajili ya Mungu. Alihubiri Injili vizuri kwa Lugha ya watu wakawaida. Inakadiriwa kwamba roho za watu milioni moja ziliokolewa katika huduma yake. Alianzisha chuo cha Biblia cha Moody ambacho kinaendelea kuwepo hadi leo.

Charles Spargeoni

Spargeoni alikuwa ni Mwana wa mfalme wa wahubiri na alikuwa mchungaji wa Kanisa la Kibaptisti tubernakulo mjini Londoni. Aliwahubiria zaidi ya watu 5000 kwa saa 40 kila wiki.

Mungu alikuwa anarudisha mahubiri ya msalaba kwa kanisa lake

Mwenendo wa kisasa kwa kazi za misheni

Hiki ni kipindi cha uamsho mkubwa na jitihada nzito za kimisionari. Dunia ilikuwa ni mlango uliokuwa wazi kwa wamisionari.

Marko 16:15—Naye akawambia enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe. (Mathayo 28:19–20)

William Carey (Uhindi)

William Carey (1761–1834) ni baba wa Umisionari wa kisasa. Alikuwa Mwingereza maskini. Kipindi fulani, alitembea kilomita 13 kila Jumapili kuhubiri kanisani. Alijaribu kuwashawishi watu kwenda kuhubiri katika nchi nyingine, lakini wakasema, "Ikiwa Mungu anataka kuokoa wapagani, atafanya hivyo, bila msaada wako au wangu."

Alikwenda kwa Uhindi 1793. Huyu ndiye misionari wa kisasa kwanza aliwasili nchini Uhindi. Huko, hakuona waongofu kwa miaka saba. Hakuwa na muda mwingi akilaani dini ya Hindu, lakini badala yake alitumia wakati wake akizungumza juu ya Yesu, kifo chake, na Ufufuo Wake. Huyu ndiye mmisionari wa kwanza kufika nchini Uhindi. Maneno mazuri yake ni, "Anatarajia mambo makuu kutoka kwa Mungu, jaribu mambo makuu kwa Mungu."

Adoniramu Judsoni (Burma)

Aliowa 5 Februari, 1812, na ndani ya wiki mbili walikuwa katika mashua kuelekea Uhindi kutoka Marekani. Walianza safari ya kufanya kazi kwa Kanisa la Congregational, lakini kwa sababu Adoniram alifikiri kuwa Kanisa la Congregational lilikuwa baya kuhusu ubatizo, alimshawishi mkewe na mshirika mwingine aliyekuwa pamoja nao kuwa Wabatisti. Alipeleka barua ya kujiuzulu walipofika Uhindi. Mshirika huyo alichukua barua hiyo, na akajaribu kuongeza fedha kutoka kwa Wabatisti.

Serikali ya Uhindi haikuwaacha wapate kukaa huko, na William Carey alipendekeza kuwa wanapaswa kwenda Burma. Walipofika Burma, walianza kujifunza lugha, walifungua shule kwa wasichana, na walitafsiri Agano Jipya. Ilikuwa miaka sita kabla ya kuwa na Mkristo wao wa kwanza kubadilisha. Adoniram alitumia miaka miwili jela. Ann, mke wa Adoniram alikufa akiwa na umri wa miaka 36. Judson alianzisha makanisa 63, hasa kati ya kabila la Karen.

Daudi Livingstone (Afrika)

Anaelezwa kama mtafuta njia barani Afrika. Alijitolea kusafiri hadi ndani kabisa ya bara la Afrika ambako hakukuwa na mzungu yeyote aliyekwisha fika huko kabla yake. Alitumikia miongoni mwa watu wa Tswana kwa miaka kumi, lakini aliona mtu mmoja tu aliyebadilishwa. Alifungua vituo vya misheni na alifanya mengi kuinadi injili barani Afrika.

Hadsoni Taylor (Uchina)

Alianzisha kituo cha Misioni ndani ya Uchina na kikundi chake kilihubiri injili hadi katikati ya nchi hiyo. Alikua na ndevu, alikua na nywele zake kwa muda mrefu, na yeye alisuka nywele zake, ambao ulikuwa mtindo wa wanaume nchini China wakati huo. Yeye alisema, "Sio kuuhamisha utaifa wao, bali tunataka wao kuwa Wakristo." Aliwaweka wamisionari 849 vituoni, kuanzisha vituo vya wamisionari 205, na jamii yake ya umishonari ilikuwa na waongofu 125,000 kwa Ukristo.

Majadiliano: Je, wamishonari husaidia au kuumiza watu wa ndani?

Uamsho wa Mtaa wa Azuza (1906)

Kuanza kwa karne ya 20 kulishuhudia mbubujiko wa Roho Mtakatifu huko Los Angeles katika California, Marekani. Mungu alikuwa analirudishia Kanisa Pentekoste upya.

Wahubiri wengine muhimu

Billy Sunday

Billy Sunday alisimama imara kupinga ulevi na alikuwa ni mhubiri shupavu wa injili.

Smith Wigglesworth

Smith Wigglesworth alikuwa Mtume wa Imani ambaye alikuwa na huduma kubwa ya uponyaji.

Uamsho wa Mahemani wa miaka ya 1950

Oral Roberts, A. A. Alan, Jack Coe, na William Branham walizunguka Amerika na mahema makubwa na wakahubiri. Jack Coe alikuwa mtu wa imani kali. Aliweza kuvunja magongo ya walemavu na kutupa mbali mikongojo wakati alipoombea wagonjwa.