Skip to main content

Kanisa la Kifalme

Tatu: Kanisa la Kifalme (313–476 BK)

Tangu kutolewa Hati ya Konstantino mpaka angukola Roma.

Konstantino

Msalaba wa Konstantino

Alipigana vita na Maksentiusi kugombea ufalme katika mapigano ya Daraja la Milviani na mwaka 312 BK. Jeshi lake lilizidiwa nguvu na askari wa Maksentiusi ambaye aliutaka pia ufalme. Mshindi wa vita hii angekuwa mfalme ajaye wa Roma. Konsitantino alidai kuwa na maono ya msalaba ulioandikwa maneno, "katika alama hii shinda vita." Msalaba ulikuwa barua za Kigiriki chi (Χ) na rho (Ρ), ambazo ni barua mbili za kwanza za neno la Kigiriki Christos (ΧΡΙΣΤΟΣ), ambalo tulipata neno letu "Kristo." Konstantino alifanya alama hii ya msalaba kuwa alama ya jeshi lake, na akaiweka katika ngao za askari wake. Konstantino alishinda vita ile na akawa Mfalme wa Warumi.

Konstantini alifanya muafaka wa imani na hii akachukuliwa kama aliyeingia ukristo

Wanahistoria wengi wa kikristo walitilia shaka uaminifu wake.

Hati ya Uvumilivu (Hati ya Konstantini) (313 BK)

Hati ni amri rasmi au waraka maalumu. Hati hii ilitoa uhuru kwa dini zote katika Ufalme wa Kirumi na ikasimamisha mateso yote ya Warumi kwa Wakristo. Mali zote zilizokamatwa wakati wa utawala wa Mfalme Diokletiani zilirudishiwa wenyewe.

Matokeo ya kuvumiliwa kwa kanisa

Mateso kwa Wakristo yalikoma

Ukristo uliostawi katika kipindi cha mateso uligeuka wa kidunia chini ya maelewano na serikali

Makanisa yaliyokamatwa wakati wa mateso yalirudishiwa hadhi yake

Majengo mapya ya kanisa yalijengwa. Kanisa la Roma liitwalo Basilika likawa ndio jengo la mfano wa majengo ya kuvutia ya makanisa. Jengo la Basilika lilikuwa ni mahakama iliyokuwa na umbo la mstatili uliyogawanywa katika safu yanguzo zenye jukwaa lililokuwa nusu mviringo upande mmoja na viti vya maofisa vikiwepo mwishoni mwa upande mmoja. Huu ndio mfumo uliopo bado mpaka leo katika kanisa Katoliki. Mfano wa usanifu wa majengo wa namna hii ni Basilika ya Mtakatifu Petro huko Roma.

Matoleo ya sadaka ambazo ni rasmi yalikoma

Raia wa Roma waliacha kutoa matoleo za sadaka kwa miungu wa kipagani.

Makanisa yalikuwa yakisaidiwa na Dola

Mahekalu ya miungu pia yalikuwa yakipata misaada kutoka katika hazina ya umma. Makanisa na wachungaji wake walipokea fedha kutoka serikalini.

Wachungaji walikuwa wakipewa marupurupu

Makuhani akawa darasa tajiri. Wanaume walipenda nafasi hizi kwa faida ya fedha na nguvu zinazohusiana na nafasi hiyo.

Sehemu zingine za ibada ya kipagani zilikuwa sehemu ya kanisa

Kwa kipindi kirefu, kulikuwa na matendo fulani ya mila za kipagani za Kirumi ambazo zikawa sehemu ya kanisa. Baadhi ya miungu ya kirumi inafanana na watakatifu ambao wakatoliki wanawaomba. Baada ya watu huona ufanano kati ya sanamu ya Maria ikimshikilia mtoto Yesu sanamu za kirumi hufafanua Fortuna na Jupita. Kuna baadhi ya wakristo ambao hawapendi kusherehekea Krismas kwasababu sikukuu hii ina mizizi katika sikukuu za kipagani za kirumi za Satunalia.

Baadhi ya watu watasema Konstantino alianzisha Kanisa la Kikatoliki, lakini lazima ikumbukwe kwamba mapokeo na imani za kile ambacho Kanisa la Kikatoliki liko kwa siku zetu za leo imehusishwa kwa zaidi ya miaka mingi kutoka ile hali ambayo kanisa lilikuwa nayo wakati wa Konstantino.

Kuanguka kwa utawala wa Kirumi wa Magharibi

Mfalme Konstantino alichagua mji wa Ugriki uitwao Baizantiamu kuwa mji wake mkuu na akauita Konstantinopo (330 BK)

Hali hii ilimwongezea ushawishi askofu wa Roma. Sasa mji mkuu ukawa ukombali sana na Roma na ile Himaya ikiwa imeshaporomoka.

Kugawanywa kwa himaya hiyo kulifuatiwa na ujenzi wa mji mkuu mwingine

Mfalme mmoja peke yake hakuweza tena kulitawala eneo lote kwani lilikuwa kubwa mno. Bahari ya Adriati ikawa ndio mpaka wa asili kati ya sehemu mbili za himaya hiyo. Mwaka wa 395 baada ya Kristo himaya ya Kirumi iligawanyika rasmi kuwa Himaya ya Mashariki na Himaya Magharibi.

Himaya ya Magharibi ilimokuwa Roma kama mji wake mkuu iliendelea kuwepo hadi mwaka 476 BK

Himaya ya Mashariki iliyokuwa na Konstantinopo kama mji mkuu ilikuwepo hadi mwaka 1453 BK

Hii ndio baadaye ikageuzwa kuwa Himaya Takatifu ya Roma ya Nyakati za Kati kuanzia mwaka 500 hadi mwaka wa 1500 BK.

Viongozi wakuu wa Kikristo wa kipindi hiki

Atanasi (296–373 BK)

Alikuwa mlinzi wa imani katika ubishani wa Ariani. Aria ambaye aliongoza mafundisho ya uongo hakuamini kanuni ya Biblia ya Utatu. Alikuwa Askofu wa Alexandria tangu mwaka 325 BK. Mnamo 367 BK yeye aliandika barua kutambua kanuni za Agano Jipya ambazo tunatumia leo. Alipelekwa uhamishoni mara tano kwa sababu ya mafundisho yake.

Yohana Krisostomu (345–407 BK)

Huyu anajulikana kama "mdomo wa dhahabu" kwa sababu aliweza kuongea kwa ufasaha wa ajabu. Alikuwa mhubiri shupavu, kiongozi watu na mwenye uwezo mzuri wa kuifafanua Biblia. Alikuwa askofu wa Konstantinopo mwaka 398 BK. Alifukuzwa nchini kutokana na msimamo wake wa kusema ukweli na alifia uhamishoni.

Augustino (354–430 BK)

Augustino alisema, "Mioyo yetu haina pumziko hadi imekupata wewe." Alikuwa Askofu wa Hippo huko Afrika Kaskazini mwaka 395 BK. Yeye ndiye mtetezi Mkuu wa ubishani wa Pelagia. Mafundisho haya ya uongo yalipambwa na Pelagio ambaye hakuamini dhambi ya asili. Augustino alijenga jina lake kama mhubiri, mwalimu na mwandishi. Yeye alijihusisha katika changamoto nyingi za siku zake (mfano wa Udonatismu na Upelagiasmu).

Ambrosi

Ambrosi alikuwa mtawala wa Milani. Wakati askofu wa Milani alipokufa mnamo mwaka BK 374, kutuliza ghasia juu ya nani angekuwa Askofu baadaye. Ambrosi alipiga hatua katika kujaribu kushusha vitu chini, na watu katika kusanyiko walipiga kelele kwamba yeye angekuwa askofu, hata ingawa yeye alikuwa bado haja batizwa yeye alilalamika lakinni mwishowe akaja kuwa askofu.

Wakati mtawala Theodosi kwenye uwanja wa watu waliouawa, Ambrosi aliwasiliana naye. Theodosi alifanya toba kwa kuvaa mavazi ya magunia na kupiga magoti mbele ya askofu akiomba msamaha. Huu ulikuwa mwanzo wa serikali kunyenyekea mbele ya kanisa.

Tunaona maendeleo ya uhusiano wa kanisa na serikali:

  1. Kanisa lilikuwa ndogo kuliko serikali
  2. Kanisa lilikuwa sawa na serikali
  3. Kanisa lilikuwa kubwa kuliko serikali

Yeromi

Yeromi (aliyejulikana kama Eusebio) alitafasiri Biblia kwenda Kilatini mnamo mwaka 405 BK. Na tafasiri hii ikawa inajulikana kama Vulgate kutoka neno la kilatini vulgus, ambalo humaanisha "kawaida."

Patriki (390 BK)

Patriki alikuwa mmishenari kutoka Uingereza kwenda Ireland. Aliuleta ukristo huko Ireland, na kanisa huko Ireland liliendelea kwa nje ya Utaratibu wa kirumi. Ireland haikuwa wakatoliki hadi 1100s.

Matukio ya ufunguo wa kipindi

Mabishano ya Wadonatusi (312 BK)

Wakati wa mateso ya Diocletiani, baadhi ya viongozi wa kanisa walitoa nakala ya Maandiko kwa mamlaka ya serikali. Viongozi hawa wa kanisa walijulikana kama wasaliti kwa sababu walisalitiwa kanisa.

Katika 311 BK mtu mmoja aitwaye Caecilliani alichaguliwa askofu wa Carthage. Caecilliani alikuwa amewekwa wakfu na askofu ambaye alikuwa msaliti. Mtu wa Kaskazini mwa Afrika aliyeitwa Donatusi alijitenga na kanisa mwaka 312 BK kwa sababu hakuamini kuwa Caecilliani lazima kuruhusiwa kuwa askofu, tangu alipaswa kuteuliwa na msaliti.

Baadaye Wadonatusi walibatiza tena Wakristo waliokuwa alikanusha imani yao kwa sababu ya mateso.

Baraza la Nikia (325–460 BK)

Katika Agano Jipya hasa hasa injili ya Yohana, tunaona kuwa Yesu yuko sawa na Baba, lakini hakuna habari za moja kwa moja kuhusu uhusiano wao. Swali lilikuwa kwamba vipi mtu aweza kuabudu wote Yesu na Baba hata sasa bado kuna swali hili kwa (mtu wanaoamini kwa mungu moja na kumwabudu)?

Ario, aliyekuwa ni mzee katika Alexandria, alianza kuhubiri mnamo mwaka 318 BK kwamba Yesu hakuwa Mungu wakati wote, bali alikuwa ni mtumishi mdogo wa Mungu. Hili lilikuwa jibu lake kwa wana monotheism. Alexanda Askofu wa Ario alisema ikiwa Mungu habadiliki, na yeye siku zote amekuwa Baba basi hiyo humaanisha kuwa lazima siku zote awe na Mwana.

Mjadala huu wa kidini ulimpata Konstantino, kwa sababu vurugu zilianza kwa sababu hiyo. Mnamo mwaka 325 BK Konstantino aliita baraza katika Nikia kutatua mjadala ulioibuliwa na Ario. Maasikofu zaidi ya 300 walihudhuria.

Maaskofu walitengeneza maelezo ya imani, ambayo, baada ya nyogeza zingine zilizofanywa kipindi cha Konstantinopo mnamo mwaka 381, ikajulikana kama shahada ya Nikia. Wote walitolewa pamoja na Ario ispokuwa Maaskofu wawili tuu walikataa saini maelezo ya imani. Kifwatacho ni kifungu kamili cha shahada:

Nasadiki kwa Mungu mmoja,
Baba mwenyezi,
Muumba wa mbingu na dunia
na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.
Nasadiki kwa Bwana mmoja, Yesu Kristo,
Mwanae pekee wa Mungu,
aliyezaliwa kwa Baba tangu milele yote.
Mungu aliyetoka kwa Mungu, mwanga kwa mwanga,
Mungu kweli kwa Mungu kweli,
aliyezaliwa, bila kuumbwa, mwenye uungu mmoja na Baba:
ambaye vitu vyote vimeumbwa naye.
Alishuka kutoka mbinguni,
kwa ajili yetu sisi wanadamu, na kwa ajili ya wokovu wetu.
Akatwaa mwili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kwake yeye Bikira Maria,
akawa mwanadamu.
Akasulubiwa kwa ajili yetu sisi, kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato;
akateswa, akafa, akazikwa,
siku ya tatu akafufuka,
kadiri ya Maandiko,
akapaa mbinguni,
amekaa kuume kwa Baba.
Atakuja tena kwa utukufu,
kuwahukumu walio hai na wafu,
nao ufalme wake hautakuwa na mwisho.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Bwana mleta uzima:
atokaye kwa Baba na Mwana.
Anayeabudiwa na kutukuzwa, pamoja na Baba na Mwana:
aliyenena kwa vinywa vya manabii.
Nasadiki kwa Kanisa moja, takatifu, katoliki, la Mitume.
Naungama ubatizo mmoja kwa maondoleo ya dhambi.
Nangojea na ufufuko wa wafu,
na uzima wa milele ijayo. Amina.

(https://sw.wikipedia.org/wiki/Kanuni_ya_Imani_ya_Nisea-Konstantinopoli accessed 2018/08/23)

Shahada inasema Yesu ni "Nuru kutoka Nuru." Je unawezaje kutenga nuru na jua? Kwa mfano huo huo je unawezaje kumtenga Mungu (Baba) kutoka Mungu (Mwana)?

Baraza haikujenga wazo la Utatu, tangu Utatu ilikuwa sehemu ya ibada ya kanisa tangu mwanzo (kwa mfano, ilitumika katika ibada ya ubatizo). Kwa Nicea waliunda msamiati kuelezea yale waliyoamini tayari kuhusu Mungu.

Baraza la kwanza huko Efeso (431 BK)

Baraza la Nikia liliamua kwamba Yesu alikuwa Mungu pia mwanadamu lakini kulibakia maswali kuhusu asili ya Yesu. Yeye ni Mungu kwa kiasi gani? Je, Yesu aliwahi kufanya dhambi kwa upande kibinadamu? Je, yeye ana akili mbili? Yesu angeweza kutenda dhambi kwa kuwa alikuwa mwanadamu? Viongozi wa wawili wa kanisa walitoa majibu kuhusu aina hizi za maswali. Walikuwa ni Nestorius na Cyril.

Nestorius

Nestorius alikuwa Asikofu wa Konstantinopo. Ni mwindaji aliye jaribu kuzuia kuenea kwa mafundisho kama Arianism kutoka kueneza.

Nestorius alipokea mawazo ya viongozi wengine wa kanisa wakati alikataa kutumia neno Theotokos, ambalo linamaanisha "Mama wa Mungu." Aliamini kama Mwana wa Mungu alikuwapo kila wakati, basi hakuweza kuzaliwa. Alipenda neno Christotokos, ambalo linamaanisha "Mama wa Kristo." Nestorius pia hakupenda Theotokos kwa sababu ya msisitizo kwamba Apollinarianism kuwekwa juu ya neno hili. Apollinarianism ilifundisha kwamba Yesu hakuwa na roho ya mwanadamu, lakini alikuwa Mungu amevaa katika mwili wa kibinadamu.

Aliamini kwamba Kristo alikuwa na nafsi mbili, lakini alikuwa bado mtu mmoja. Alisisitiza tofauti kati ya nafsi hizi mbili, hasa katika mateso ya Kristo. Alisema kwamba ilikuwa tu nafsi ya kibinadamu ulioteseka wakati Kristo aliteseka, na sio nafsi ya kimungu.

Cyril

Cyril alikuwa askofu wa Alexandria. Wakati Nestorius alisisitiza zaidi nafsi wa mwanadamu wa Kristo, Cyril alisisitiza zaidi ya nafsi yake kwa Mungu. Aliamini kwamba msisitizo wa Nestorius wa nafsi mbili za Kristo ulikuwa unaharibu wazo la umoja wa Kristo. Ikiwa tu mwili wa Kristo unasumbuliwa, basi Kristo hakuwa kuhani mkuu wa wakika, kwani ilikuwa tu kwa mateso ya kimungu ambayo Kristo angeweza kulipa kwa ajili ya dhambi za ubinadamu.

Uamuzi wa baraza

Kwa sababu Nestorius hakutaka kutumia jina Mama wa Mungu kwa Maria, alitunguliwa mashtaka na Cyril kwamba hakuamini kwamba Yesu alikuwa Mungu. Baada ya barua zenye hasira kati yao, baraza la maaskofu liliitwa kutatua mjadala huo.

Baraza lilivutia kwa kiasi kikubwa kwa sababu za kisiasa. Baraza la Pamoja la 381 liltangaza kwamba Askofu wa Konstantinopo atakuwa askofu wa pili pekee wa Roma (papa). Hasira za baadhi za maaskofu wengine, akiwemo Cyril, kwa sababu ilizuia nguvuu wao kama maaskofu. Pamoja na hivyo kulikuwa na maswali kuhusu mafundisho ya Nestorius, baraza pia liliitwa kwasababu ya wivu wa madaraka yake.

Baraza liliamua kinyume cha Nestorius na alikuwa uhamishoni kama mrithi. Pamojana hivyo alihamishwa, watu waliendelea kuamini mafundisho yake na Unestoria bado upo leo kama tawi la Ukristo.

Japokuwa kulikuwa na baadhi ya tofauti ya mafundisho kati ya Cyril na Nestorius, kwa kiasi kidogo hawakukubaliana kw jinsi ya uhamasishaji wa baadhi ya sehemu ya mafundisho ya Kristo na maajabu ya makubaliano yangeweza kuwepo kama wangekaa kuongea pamoja kuhusu mawazo yao. Wote wawili walikuwa na wasiwasi wa kulinda imani dhidi ya mafundisho ya uwongo. Wakati haiwezekani kujua, hatuwezi kushangaa makubaliano gani ambayo wangeweza kuja nao ikiwa walisema pamoja kuhusu mawazo yao.

Ingawa Nestorius mara zote alihusishwa mhamiaji, baraza la Kalsedoni lilifanya maamuzi kuhusu mafundisho ya Kristo ambayo yalikuwa karibu na mawazo ya Nestorius. Nestorius pia alikuwa sahihi kuhusu ni namna gani Mama wa Mungu walimtukuza Maria katika nafasi ambayo ilikuwa ni zaidi ya madai. Kwa miaka mingi, tumeona mila ya Kanisa la Katoliki la Kirumi likimtoa Maria katika nafasi aliyokuwa zaidi wamejihusisha kwa kimungu.

Baraza ya Konstantinople (381 BK)

Watu wengine hawakuamini kwamba Roho Mtakatifu alikuwa Mungu, kwa sababu Yeye hakuzungumza yeye Mwenyewe. Walisema kwamba hakuwa nafsi, bali nguvu ya kiroho. Baraza hii iliitwa ili kuthibitisha uungu wa Roho.

Baraza ya Chalcedon (451 BK)

Hili ndio baraza la mwisho la makanisa yote yaliyokuwa kuhusu asili-mbili za Yesu. Kusudi lake lilikuwa kumaliza mjadala juu ya Utatu. Ndani yake, ilitangazwa kuwa Kristo ni "atambuliwe katika asili mbili, bila kuchanganyikiwa, kugeuzwa, kugawanywa, kutengwa... bali hulka ya kila asili ikihifadhiwa na kukubaliana katika mmoja na katika dutu moja, si kugawanywa au kutengwa kuwa wawili, bali mwana huyo mmoja." Dutu maana "vifaa." Kufuatia ni maandishi kamili ya imani iliyotolewa kwa Chalcedon:

Sisi, basi, tukiwafuata baba zetu watakatifu, sote kwa ridhaa moja, twafunza watu kukiri Mwana yule mmoja, Bwana wetu Yesu Kristo, yeye mkamilifu katika utatu na pia katika ubinadamu; Mungu kweli na binadamu kweli, mwenye roho na mwili zote kamili kawaida; hususan na Baba kulingana na utatu, hususan kama sisi kibinadamu; katika vyote kama sisi, bila dhambi, wa pekee wa Baba kabla ya nyakati kulingana na utatu, na siku hizi za baadaye, kwa ajili yetu na wokovu wetu, mzaliwa wa bikira Maria, mama [wa] Mungu, kibinadamu; Kristo mmoja yule, Mwana, Bwana, wa pekee, atambuliwe katika asili mbili, bila kuchanganyikiwa, kugeuzwa, kugawanywa, kutengwa; tofauti katika asili isiwe nafasi ya kubatilisha hali ya umoja, bali hulka ya kila asili ikihifadhiwa na kukubaliana katika mmoja na katika dutu moja, si kugawanywa au kutengwa kuwa wawili, bali mwana huyo mmoja, pekee, Mungu Neno, Bwana Yesu Kristo; vile manabii tokea mwanzo (wamefunza) kumhusu, na Bwana Yesu Kristo ametufunza, na imani ya baba watakatifu tuliyoachiwa.

(http://www.cprf.co.uk/languages/chalcedon_swahili.html#.W4zxCegzbb1 accessed on 2018/09/03)

Tangu Nikia, kanisa lilikazia kwamba Yesu alishiriki asili na Baba, lakini sasa waliongeza kwa hili jinsi Yesu pia alishiriki asili na mtu.

Ilikuwa ni baraza la kwanza ambalo papa alicheza jukumu kubwa, na ilikuwa baraza la mwisho ambalo Mashariki na Magharibi wote watatambua rasmi.