Kanisa la Zama za Enzi za Kati
Nne: Kanisa la Zama za Enzi za Kati (476—1473 BK)
Toka anguko la Roma hadi anguko la Konstatinopo.
Kanisa la Zama za Enzi za Kati lilifunikwa na giza
Isaya 9:19—Kwa sababu ya hasira ya BWANA nchi hii inateketea.
Kipindi cha karne ya 5 mpaka ya 15 huitwa kipindi cha zama za Giza.
Ustaarabu na uvumilivu ulifikia mwisho.
Kulikuwepona maendeleo madogo sana katika fasihi, sanaa na sayansi
Kulikuwa na umaskini na ushirikina ulioijaza nchi. Nchi nyingine walivamia Ulaya na kuua watu wengi. Palitokea pia vifo vilivyotokana na ugonjwa wa mtoki ambao ulienea katika bara lote.
Mazungumzo: Je, Mungu bado hutumia hukumu ili kuwaadhibu watu?
Biblia ilikuwa imezuiliwa kutoka kwa watu
Kanisa lilifundisha kwamba ni wachungaji tu ndio wanaoweza kuitafsiri Biblia. Watu wa kawaida walikatazwa kusoma Biblia, Biblia ilikuwa katika lugha yake ya mwanzo au katika lugha ya Kilatini ambayo ni watu wachache waliokuwa wanaielewa hata kama walitaka kujisomea wenyewe.
Watu waliwekwa gizani
Misa ilifanywa kwa Kilatini ambacho hakukuwepo wengi waliokifahamu. Ukweli na sayansi viligandamizwa na kanisa Katoliki. Galileo, yule mtu aliyegundua darubini alikaribia kuuawa kwa sababu kile alichoona kwa kutumia darubini kilikuwa kinyume na msimamo wa Papa ambaye alifikiriwa kwamba hawezi kukosea.
Viongozi wa kanisa walikuwa na tabia mbaya
Mawazo ya kanisa katika kipindi hiki
Ushirika
Ushirika ulikuwa kitovu ni kitovu cha wakristo kuabudu kwa kipindi hiki. Ibada ilizungumzwa kwa Kilatini, na makuhani wengi wa vijijini walikuwa hawaja elimika, hivyo hawakuweza kutoa hotuba. Viongozi ndio waliruhusiwa kuimba, lakini watu wote hawakuruhusiwa kuimba.
Kujikana
Baadhi ya watu hawakupenda jinsi kanisa lilivyo kua katika utajiri na nguvu. Hawa watu walijitenga wenyewe kutoka ulimwenguni na kuishi katika jamii zao. Walisali mara saba wakati wa mchana na kukaririsha sehemu kubwa ya Maandiko. Wanaume waliitwa watauwa na Wanawake waliitwa masista. Watauwa na masista waliishi katika jamii zilizo jitenga.
kuhamisha wenye dhambi (Purgatori)
Kanisa lilijua kwamba wenye haki walienda mbinguni na wasiohaki walienda Jehanamu,lakini nini ilitokea kwa watu ambao hawakuwa na haki wala wale wenye haki zaidi? Kuhamishwa kwa wenye dhambi (pagatori) kulikuwa endelevu kwa kipindi kile kama jibu kwa wale watu wa kawaida walipokuwa wakienda baada ya kufa.Inasemekana kuwa mahali ambapo mtu kawaida hutolewa kutokana na dhambi gani ambazo walikuwa nazo.
Vyeti vya upatanisho Indulgences
Hizi zilikuwa ni hati ambazo zilitolewa na kanisa kuondoa adhabu kwa wenye dhambi.
Falme za Kikristo
Katika kipndi hiki, hapakuwa na tofauti kati ya dini na kidunia. serikali na kanisa walishirikiana (na mara nyingine walipigana kwa ajili ya) mamlaka. Watu wote waliozaliwa katika nchi za Kikristo walifanywa kuwa Wakristo.
Kuongezeka kwa Upapa
Katika kanisa la kwanza, Askofu wa Roma (aliyejulikana baadaye kama papa) alikuwa ni askofu wa maaskofu. Maaskofu wote walikuwa na nguvu sawa. Lakini mwishoni mwa kipindi hiki, Papa alikuja kuwa ni mtu mwenye nguvu zaidi katika kanisa. Hii ilitokeaje? Ilitokea kwa miaka mingi na ilikuwa kwa sababu ya mawazo ya baadhi ya mapapa.
Leo Mkuu (c. 400–461 BK)
Leo alikuwa Papa kutoka mwaka 440–461 BK.Alisema kwamba nguvu ya upapa alipewa na Petro kutoka kwa Kristo na ile nguvu ilipitishwa kutoka kwa petro hadi kwa warithi wake. [1] Yeye alikuwa papa wa kwanza kutegemea nguvu kutoka kwa petro.Yeye aliwashawishi Wahani (wale ambao walitokea katikati mwa Asia) na Wavandali(wale ambao walitokea Mashariki mwa Ujerumani) sio kuvamia Roma.
Gregori Mkuu (c.540-604 BK)
Gregori alitokea katika familia ya kidini-Babu wa Baba yake alikuwa Papa. Alikuwa na elimu nzuri na alikuwa kiongozi wa serikali. Hakutegemea kufanywa papa mwaka590 BK,na aliendelea kuwa papa hadi kifo chake mwaka 604BK. Alijiita mwenyewe ni "mtumishi wa watumishi wa Mungu."
Kulikuwa na matatizo mengi Roma,na waliwasiliana na mtawala wa mashariki kwa ajili ya kuomba msaada. Mtawala alikuwa na matatizo yake ya kushughulikia,kwahiyo hakupeleka msaada Roma.Gregori aliamua kuyatatua hayo matatizo mwenyewe. Alichukua fedha kwa mhasibu wa kanisa kununua chakula kwa ajili ya watu na kushughulikia mifereji wa maji. Walambadi (ambao walikuwa wajerumani) walitawala sana Ulaya. Gregori alifanya mahusiano ya kidiplomasia na wao na kuwashawishi wasiivamie Roma. Kwa kutenda mambo haya ya serikali, Gregori alikuwa ni moja ya mapapa wa kwanza kuhamasisha nguvu ya kidunia ya upapa.Alisema urithi wa Petro ulimpa yeye nguvu ya kufanya maamuzi ya matatizo ya kimaadili.
Mchango wa Pippini (754 BK)
Walambadi walikuwa wakivamia tena eneo linalo zunguka Roma, na Papa stephano II hakutegemea msaada kutoka Byzantine (Mashariki) Himaya. Alitaka kutafuta kiongozi mpya wa kumsaidia matatizo haya. Aliomba msaada kutoka kwa Pippini mfupi, ambaye alikuwa mfalme wa Wafrenki (ambapo baadae iliitwa Ufaransa). Pippini alimuahidi kuwa atapigana na Walambadi na kurudisha ardhi ambayo waliichukua.
Mchango wa Konstantino
Hii ilikuwa hati ya uongo ambayo ilisemekana kuwa Costantino alimpa Papa Sylivesta aridhi iliyo izunguka Roma. Iliaminika kuwa Papa stephano wa II alitumia hati hii kumshawishi Pippini ili kumsaidia.
Charlemagne
Charlemagne alichukua kiti cha enzi 771 BK. Siku ya Christmas miaka 800, papa alimwita yeye mtawala. Tena alikuwa mtawala wa Wakristo. Bado maswali yalikuwepo juu ya kanisa au serikali ndiyo itakayekuwa na kiongozi mkuu.
Mabishano ya Kusimika (1076 BK)
Huu ulikuwa ni ushindani wa kiutawala kati ya Papa Gregori VII na Mtawala Henry IV. Serikali ilikuwa na mamlaka ya kuteua kiongozi wa Dini, hususani Papa. Henry alipaswa kuwa kiongozi alipokuwa na miaka sita tu, na viongozi wengine katika serikali walimsaidia kufanya maamuzi wakati anakua. Kanisa lilitumia faida kwa wakati huu kurudisha nyuma nguvu ya kuteua vingozi wa dini. Walijua Henry alikuwa mdogo kuwakataza wao. Katika mwaka 1059 waliunda baraza ambalo lilitangaza kuwa sifa hazitakuwa na sehemu katika kuchagua viongozi wa kanisa.
Katika mwaka wa 1075 BK Papa Gregori VII alijumuisha hati ambayo ilisema kuwa papa ana nguvu ya pekee ya kumtaja mtawala. Hivyo kanisa sasa halina nguvu tu ya kuwateua vingozi wao, lakini pia viongozi wa serikali. Kwa wakati huo Henry alikuwa mkubwa na alijibu kwa kusema kuwa Gregori sio papa tena na walifanya uchaguzi kwa ajili ya papa mpya. Gregori kisha alimtenga Henry. Mapigano haya ya nyuma na ya mbele yaliendelea kati hawa wawili kwa kipindi kirefu.
Innosenti III (1160–1216 BK)
Innosenti alipigana na viongozi wa serikali kwa ajili ya madaraka.
Mapantano ya Worms (1122 BK)
Huu ulikuwa mwisho wa ugomvi wa uwekezaji. Serikali na kanisa zilifanya makubaliano kuwa kanisa liteue viongozi wa dini. Kama tu kanisa litakuwa na migogoro kati yao serikali itasaidia kutatua huo mgogoro.
Uchunguzi Rasmi
Mahakama maalumu iliundwa mwaka 1200 kushughulikia waasi. Yoyote aliyepingana na kanisa alihesabiwa kama muasi waasi. Waasi waliwindwa na kufikishwa mahakamani na Viongozi wa viongozi wa kanisa.
Vita takatifu ambavyo pia huitwa vita vya Kidini vilidumu tangu mwaka 1095 hadi 1291 baada ya Kristo
Vita hivi vilikuwa ni jaribio la kanisa kuchukua nchi takatifu kutoka kwa Waislam
Kanisa iliweza kuwashauri watawala wa Ulaya kuongoza vita hivyo vya kidini. Kanisa walikuwa wanataka kuwafukuza Waislam kutoka Yerusalemu na kumpatia Papa mji huo kuumiliki.
Askari walishindwa kuichukua nchi takatifu kutoka udhibiti wa waislam
Mgawanyo wa mashariki-magharibi (1054 BK)
Orodha zifuatazo zinaonyesha baadhi ya tofauti kati ya makanisa ya mashariki na magharibi:
Mashariki | Magharibi |
---|---|
Walizungumza Kigiriki | Walizungumza Kilatini |
Makuhani wao waliweza kuoa | Makuhani wao hawakuweza kuolewa |
Makuhani wao walikuwa na ndevu | Makuhani wao hawakuwa na ndevu |
Imani ya Nikia inasema Roho anakuja "kutoka kwa Baba" | Ya kuongeza "na Mwana" (Inaitwa "Maneno ya Filioque") |
Walikuwa na sherehe tofauti za Misa | |
Walikuwa na tofauti za Mafundisho |
Papa Leo IX alimtaka Michaeli, Askofu Mkuu wa Konstantinopo, kutengana naye. Papa alituma wa wakilishi kwa Konstantinopo, lakini Mikaeli alikataa kukutana naye. Wawakilishi walimkataa Mikaeli kuongea naye na yeye kukataa kuongea nao.
Watu wengine wamejitenga na Kanisa Katoliki
Kulikuwapo na mabaki ya vikundi ambavyo havikuwa sehemu ya Kanisa Katoliki.
Waalbigeni walikuwa wakazi wa Albi huko Ufaransa watu hawa waliamini agano jipya ndilo lililotoa ujumbe na ya imani yao
Walimpinga Papa na kanisa Katoliki. Waalbigeni walipewa mateso makali na Papa Innocent III mwaka 1208 baada ya Kristo.
Waldensi walikuwa wenyeji wa Ufaransa, Italia na Uswisi
Walipata jina lao kumuenzi kiongozi wao aliyeitwa Perto Waldo ambaye alitafsiri Biblia kwa lugha ya watu hao. Waldo alifundisha kwamba maandiko matakatifu ndiyo mamlaka kuu kwa wakristo. Neno lao la wito lilikuwa, "Neno la Mungu linaongea na, ni busara tukitii."
Viongozi wakuu wa kipindi hicho
Bonifasi
Bonifasi alizaliwa katika 680 BK. Jina lake alilozaliwa nayo lilikuwa Winfred. Alifundishwa kama mtauwa wa Benedicto, na alitumia maisha yake mengi kama mmishenari kwa Wajerumani.
Wahenga walisema kwamba ukichukua shoka kuuendea mti uliyesimama kuusulubu kwa ngurumo ya mungu, ile radi itaupiga mti na utaanguka chini.
Anselm
Anselm alizaliwa kati ya 1033 BK. Mwaka 1903 William II, mwana wa William mshindi, alimfanya Anselm kuwa Mkuu wa maaskofu wa Canterbury, lakini alitaka kuweka nguvu kwa kumtaja Clergy. Anselm alikataa kumwachia William mamlaka haya, na yaliyotokea, yeye alitumia muda wake uhamishoni.
Henry I, kaka wa William wa II, alichukua nafasi baada ya kaka yake kufa, na alimwomba Anselm kurudi. Anselm hakuwa kiongozi kwa muda mrefu, angalau, na alienda kuishi uhamishoni tena. Aliweza kuandika mengi kwa kipindi hiki huko uhamishoni.
Thomasi Aquinas
Thomasi Aquinas alizailwa 1225 BK. Yawezekana alikuwa mwanatheolojia mkuu wa zama za kati. Yeye alisema sababu (zilizohusu wana falsafa wa zaman) katika theolojia yake.
Yohane Wykliffe
Yohane Wykliffe (1330—1384) alikuwa mtu wa kwanza kutafsiri Biblia kwa kiingereza. Anakumbukwa kama nyota ya asubuhi wa mageuzi. Alikuwa na wafuasi, waliyekuwa wanaitwa lollards, ikiwa na maana ya "wahubiri maskini." Alipingana sana na Kanisa Katoliki. Zifuatazo ni baadhi ya mambo aliyoyauliza juu ya kanisa:
- Haki za kanisa kwa wagonjwa na utajiri
- Kuuza vyeti vya upatanisho
- Ibada ya Watakatifu na vifaa vilivyo tumika
- Mamlaka ya papa
- Kugeuka asili ya mwili na damu ya Yesu katika ushirika Mtakatifu.
Huyu angeuawa na kanisa katoliki kama mabwenyenye wa Uingereza hawakumpatia ulinzi. Mahubiri ya Wykliffe na tafsiri ya Biblia iliandalia njia ya mageuzi. Wakatoliki walimchukia sana Wyklif kiasi kwamba alipokufa waliutoa mwili wake kaburini miaka mingi baada ya kuzikwa na kuudhihaki.
Yohane Huss
Yohane Huss (1369—1415 BK) alikuwa msomi wa maandiko ya Wykliffe, na alikataa kabisa mamlaka ya papa. Alisisitiza kwamba Kristo pekee ndiye alikuwa kichwa cha kanisa na Mungu pekee ndiye asameheaye dhambi. Alipopelekwa mbele ya baraza kwenda kuulizwa maswali kuhusu imani yake, alisema, "Mimi sikuwa mhudumu mkuu, dhahabu hujionyesha kutokana na ukweli." Alihukumiwa kama muasi na alichomwa katika mchi kwa amri ya Baraza la Kanisa Kikatoliki.
No Comments