HITIMISHO KWENYE VIZIBUO
HITIMISHO KWENYE VIZIBUO:
Mhubiri anapaswa kuandika kwa kifupi kitu alichojifunza
Andika maana ya maneno mapya au yasiozoeleka
Kila mmoja atajenga utaratibu wake mwenyewe wa kujifunza maneno mapya. Baadhi ya maneno ya Biblia yanayo maana tofauti katika lugha ya asili zaidi ya maana yake ya leo. Njia mojawapo ni kuwa na daftari ndogo ya maneno mapya na ufafanuzi wa maneno ya Biblia; hii itakusaidia kukumbuka maelezo yake. Jinsi muhubiri anavyoelewa zaidi kuhusu Neno la Mungu ndivyo Mungu anavyoweza kumtumia awpo katika mimbari.
Andiko unazojiandikia katika daftari ziwe katika lugha rahisi, wazi na zenye lengo
Sio lazima uandike kitabu ili kuwa na andiko nzuri. Panga andiko zako kwa mada na masomo. Weka orodha ya aya muhimu za maandiko zinazohusiana na somo lako. Iwapo utatumia maandishi katika mimbari hayapaswi kuwa na kila kitu ulichojifunza. andiko za somo zinapaswa kuwa fupi fupi na zenye mpangilio. Katika darasa hili tutajifunza namna ya kuandaa ratiba rahisi ya somo la kutumia katika mimbari.
Andika wazo au kichwa cha somo mapema utakavyoweza
Kama hutaandika kitu mara unapokipokea unaweza usikikumbuke baadaye. Mungu anaweza akakuonyesha kitu ukiwa katika maombi au unapolisoma Neno; mambo haya yanapaswa kuandikwa na kuhifadhiwa ili uweze kujifunza au kuyatumia baadaye.
Unaweza kupata faida kwa kuitenganisha Injili katika mawazo yake
Njia nzuri ya kusoma Injili ni kuitenga katika mafungu yake muhimu kama ilivyoandikwa. Unaweza kuendelea kujifunza wazo kuu la kilichoandikwa peke yake. Lengo la mhubiri ni kushirikisha wengine sehemu moja ya ukweli au tukio kwa wakati mmoja. Kuigawa Injili katika vipande kutakusaidia kuhubiri sehemu moja ya Injili halafu ukaendelea na sehemu nyingine kisha ukaijenga yote kwa wakati. Kwa mfano Yohana 3:16 inaweza kutenganishwa katika mawazo yake makuu kama ifuatavyo:
Sehemu ya Injili | Mada ya Kujifunza |
---|---|
Kwa jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu | upendo kubwa wa Mungu—anawapenda wote |
hata akamtoa Mwanaye wa pekee | gharama kubwa ya wokovu wetu—msalaba |
ili kila amwaminiye | mahitaji makubwa—imani |
asipotee | kutoroka kubwa—kutotiwa hatiani |
bali awe na uzima wa milele | zawadi kubwa—mbinguni |
Ukiangalia sehemu ya aya hii na ukajifunza utaielewa vizuri zaidi aya yote. Hii itakusaidia pia kuihubiri kwa kipande kimoja baada ya kingine. Utajifunza maana ya kushirikisha wengine sehemu kwa sehemu na kujenga hatua moja kwa wakati mmoja.
No Comments