Skip to main content

KANUNI YA SABA

KANUNI YA SABA:HAKUNA MABISHANO KATIKA BIBILIA.

Neno la Mungu halina makosa, haliwezi kupingana lenyewe. Mahali kumeonekana ubishi, ukweli bado hauja patikana endelea kutafuta. Kuna ukamilifu na umoja usio vunjika kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo. Wakati unapofasiri sehemu ya andiko, nilazima tujifunze mukitadha wake. Sio mistari tu kabla na baada yake, bali ni andiko kuanza Mwanzo hadi Ufunuo. Ufasiri wangu wa sehemu ya andiko lazima usiharibu huu umoja mkamilifu na upatanifu wa andiko. Acha andiko liwe mfasiri wake lenyewe. Kumbuka, tunategemea toka Roho wa Mungu kufahamu neno lake (Yoh. 16:13; I Wak. 2:6–14). Muombe Mungu akuonyeshe ukweli wake (Yak. 1:5).

Wakati wakuthibitisha fundisho moja kutoka kifungu, lazima kamwe usiondoe fundisho lolote la maandiko matakatifu mahali pake.