Skip to main content

Matumizi maalum ya kifungu

Matumizi maalum ya kifungu (Vizibuo)

Utangalizi

II Tim. 2:15—Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.

Mhubiri anahitaji uelewa mzuri wa Neno yeye mwanyewe, ili waweze kuwatangazia wengine ukweli. Darasa hili litamwezesha mwanafunzi kufahamu namna ya kujifunza Neno la Mungu na kuelewa maana ya andiko. Nguvu ya hotuba ipo katika maandalizi. Mhubiri anahitaji ujumbe kutoka kwa Mungu. Maandishi ya andiko yanapaswa kuchaguliwa kwa maombi ya kina na kufikiri. Maandishi yakisha chaguliwa na mhubiri anapaswa kujifunza taarifa hizo za andiko. Lengo ni kufahamu unakoelekea kabla ya kufika katika madhabahu.

Kila mhubiri atajenga muondoko wake wa kuhubiri na wa kuandika dondoo. Baadhi ya wahubiri watahubiri bila kuwa na dondoo chache na wengine wataandika taarifa zote kuhusu hotuba yao yote. Darasa hili litapendekeza njia rahisi ya kuandika taarifa kwa ufupi kwa ajili ya matumizi ya mhubiri. Wahubiri wengine wanaweza kutumia maandishi hayo kwa ajili ya matumizi yao binafsi na wasiyatumie kabisa wakiwa Mimbari. Mhubiri anaweza kutumia njia yoyote lakini ni lazima ajifunze maandiko.

Maana ya vizibuo

Dikishenari ya Webster hufafanua vizibuo kama "sanaa ya kupata maana ya maneno ya mwandishi, ya kuielezea kwa wengine." Vizibuo vya kibiblia ni kujifunza ufafanuzi wa kibiblia. Vizibuo vya kibiblia ni kufanya harakati za kufafanua maandiko kwa usahihi. Vizibuo hushugulika na maswala kama vile:

  • Ni nini ufafanuzi wa kawaida wa kifungu hiki?
  • Ni nini ufafanuzi rasmi wa kifungu hiki?
  • Ni nini ambacho mwandishi anakusudia kusema?
  • Ujumbe gani ambao mwandishi anakusudia kuuwasilisha?
  • Je ni matumizi ya neno maalum, Uundaji wa kisarufi, wakati wa tendo, herufi, umuhimu katika mfano huu?
  • Nani waliokuwa wasomaji au wasikilizaji wa mwandishi, kwakupitia herufi?
  • Jinsi gani kifungu kimefasiriwa na watu wa siku za mwandishi?

Thamani ya vizibuo

Sio ujinga tu, bali ni hatari kupotosha Biblia Uvunjivu wa kipekee kuharibu maandiko kwa makusudi. Kuna kanuni husika za kufasiri zinazo tuongoza katika ufahamu na kufundisha maandiko Hizi kanuni huhudumia kama mistari ya mipaka ambayo hulinda maelezo yetu na uwasilishaji wa wazo la kiBiblia pamoja katika vifungo."

Tunarejelea maswala ya maandiko matakatifu kama kifungu kilicho patiwa mahali na baadhi ya wahubiri kwa kukosea hujaribu kuyafanya maandiko yakae mahali pa elimu yao ya filosofia. Biblia haihusiki na kile tunachotaka imaanishe, bali kujifunza kwetu maandiko sikuzote ingekuwa ni kungundua ujumbe wa Mungu Kufanya hivi lazima tutumie kanuni husika za vizibuo vizuri vya ufasiri na acha andiko lijisemee lenyewe (2 Pet. 1:16–21).

Kazi ya mhubiri ni kuwalisha watu ukweli wa Neno la Mungu (Yer. 3:15). Mhubiri anapaswa kuwafanya watu waweze kuielewa vema Biblia. Ni lazima mhubiri alielewe Neno yeye mwenyewe ndiyo aweze kuwahubiria watu wengine. Nehemia alisoma katika kitabu cha sheria, halafu akawaeleza watu maana yake ili waweze kuelewa Neno la Mungu kwa ajili matumizi yao wenyewe. Hii ndiyo maana ya mahubiri: kutangaza Neno la Mungu kwa njia ambayo watu watalipokea, watalielewa, watashawishika na kulifanyia kazi. Lengo la darasa hili ni kuwasaidia wanafunzi waweze kufahamu namna bora ya kujifunza Neno la Mungu. Hakuna njia maalumu iliyopangwa ya kujifunza; kila mhubiri ataweka utaratibu wake wa kujifunza Maandiko Matakatifu. Mhubiri anapaswa kujenga tabia ya kusoma Biblia kila siku. Mhubiri anapaswa kulijua Neno kabla ya kwenda kulihubiri.

Biblia ni ujumbe wa Mungu kwa mwanadamu, na Mungu anafahamu kwamba alikuwa na maana gani alipompatia mwanadamu Neno lake. Roho Mtakatifu atamwezesha mwanadamu kulielewa Neno (Yoh. 14:26; 16:7–13; I Wakr. 2:13). Mwanadamu hatapata uelewa mara moja wa Neno la Mungu. Mhubiri anaposali, na kujifunza Neno la Mungu, Mungu atamsaidia aweze kulielewa zaidi. Mhubiri ni sharti awe na uelewa angalao wa andiko anayokusudia kuihubiri.