Sheria na Njema
Sheria ni rahisi, rahisi, na njema (mst. 7-13)
Katika Warumi 7:7-13, Paulo alianza na uzuri wa sheria ya Mungu na udhaifu wa dhambi. Paulo aliwaandikia Wayahudi, wale ambayo waliifahamu sheria (mst. 1), na kujua kujenga vizuri kusudi na asili la sheria. Idhini la barua ya sheria haiwezi kumfanya hata mmoja kuwa na haki, bali katika usahihi wa kuamsha watenda dhambi katika hitaji lao la Kristo.
Swali: Dhambi ni sheria? (mst. 7a)
Kwanini Paulo aliuliza sawli hili? Paulo aliandika katika mstari wa sita kuwa sheria ilikuwa kitu kinachopelekea kitu fulani. Hii ilionekana kushawishi kuwa sheria ni "mbaya."
Jibu fupi: Hapana, sheria ilikuwa kusudi jema (mst. 7b)
Dhamira kuu ya sura ya saba ni mahusiano ya muumini kwenye sheria. Muumini aungane na Kristo, ambaye ni "mme mpya." Tulipozaliwa tulifungwa kwenye sheria kama ndoa. Tuliuwa huru mbali na sheria, kwasababu sheria haitakufa kamwe au sisi kubadilika lazima tufe. Tumekuwa wafu kwenye sheria kwa njia ya mwili wa Kristo, ambao ulituruhusu sisi kuoana na Kristo, alifufuka kutoka wafu.
Kutumikia waraka wa zamani wa sheria haukumfanya Paulo kuwa mwenye haki, bali badala yake ilifunua wazi uovu. Sheria haikuwa sababu ya dhambi zake, bali ilikuwa kama kiongozi mkuu wa shule na ilimfundisha yeye dhambi ilikuwa nini. Kwa kawaida ya jamii, Paulo hakuwa na kosa isipokuwa yeye alifuata matamanio yake, bali sheria ilihusisha kiwango cha Mungu ambaye kwa matokeo wazi ya uharibifu wa moyo wake.
Sheria yake ni mapenzi yake. Ilishauri kile ambacho ni rahisi, na sahihi, na jema na kukataza kile ambacho hakifai, jeuri, na kuumiza.
—Adam Clarke
Sheria ilifunua ukweli wa dhambi (Kol. 3:5; I Thes. 4:5). Matokeo ya ulimwengu yangekuaje bila sheria? Sheria ilikuwa muwakilishi wa agizo (amri) usalama, utulivu, uaminifu, sare, usawa. Kutokuwepo kwa sheria kulizua machafuko, kwa watumishi wabaya. Kama nguvu ya sheria ilizuiliwa matokeo yake yangekuaje? Mwisho wa dunia.
Dhambi huleta mauti (mst. 8)
Paulo alizungumzia dhambi kwa kutolea mwanadamu mfano na kwa kufanya hivyo aliweza kueleza dhambi kutoka kwa mtu. Upanga wa rohoni hukata migawanyo ya hukumu ili kwamba tuweze kuona tunaweza kuwa huru mbali na dhambi. Kama dhambi ina sifa ya kumsubiri adui kudaka na kuchukua faida ya mtu mwingine, ndipo yule mwingine aweze kumpa mwingine kwa njia ya haki, kanusha ile dhambi. Mauaji yapo miongoni mwa mtenda dhambi. Lakini, kama dhambi pekee ina atahari ya asili ya moja kwa moja, hukumu inaweza kufanyika vipi kwa haki?
Nini ilikuwa hoja ya faida kwa dhambi? Sheria inaeleza mtenda dhambi ni kama mfu katika dhambi yake. Kuwa mfu, dhambi ilichukua faida ya uasi na kufanya vifo zaidi.
Bila sheria dhambi imekufa
Sheria ni kama msitari wa tamaa: Inaonyesha wapi na nini iko katika macho ya Mungu. Ilikuisudia kuamsha watenda dhambi kwa hitaji lake kwa Kristo. Ndipo sheria ilikuja kuwa mwelekezaji kwa Kristo ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
Sheria ilifua nguvu ya dhambi (mst. 6)
Chini yua sheria, mwanadamu alihukumiwa kifonkwasababu ya dhambi. Warumi 7:5 inaeleza hali ya Wayahudi kimwili wakiitumikia dhambi ambaye waliichukulia wako chini ya sheria. Ilionyesha kuwa ilikuwa laana (Walawi. 27:26; 28:15; Zab. 119:21; Yer. 11:3; Gal. 3:10).
- Laana ilitangazwa hasa usalama wa utii wa maagizo.
- Laana haikumaanisha kuangamiza mtu hata mmoja bali kutengeza toba.
Sheria ilimaanisha uzima, bali ilileta kifo (mst. 10)
Matokeo ya mwisho kwa Paulo aliyefuata sheria kwa nguvu na kuitunza kwa bidii, alikuwa amekufa katika dhambi! Dini zake zote zilifanya kazi kwa pasipo haki—katika nuru ya msalaba, amri zote za Mungu zilikuwa hukumu ya kifo.
Sheria ilidhihirisha udanganyifu wa dhambi (mst. 11)
Dhambi ilichukua faida yetu na ilitudanganya. Sheria ya Mungu ikaja kujulikana kwa njia tofauti: Sheria za sikukuu, sheria za kijamii, sheria za asili, sheria za madili, na sheria za afya. Wayahudi waliamini ukitunza sheria hizi zote utakuwa mtakatifu. Kwa wakati wa Paulo kufanya huduma, Marabi walikuwa na jumla ya sheria 613 katika amri za Agano la Kale. Haikuwa rahisi kuzitunza hizo zote, hasa hasa tangu zilipoharibiwa mbele ya kusudi la Mungu.
Sheria ilifunua madhara ya dhambi. Madhara ya dhambi zote ni kifo cha kiroho. Madhara ya kufa kimwili pasipo kutubu dhambi ni utengano wa milele kutoka kwa Mungu. Kwa kutoweza kutekeleza sheria mkosaji akawa anahukumiwa kifo chini ya sheria. Amri haiwezi kukupa uzima, bali inaweza kukutuhumu kwenye dhambi kwa kupitia hukumu ya kifo na inakusababibsha wewe kutubu na kutafuta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
Sheria yenyewe ni takatifu, ina uadilifu, na njema (mst. 12)
- Ni takatifu kwasababu haikaribii dhambi
- Ina uadilifu kwasababu inahukumu wakosaji
- Ni njema kwasababu kusudi lake ni la kiroho (ni sehamu ya mpango wa mwisho wa Mungu kumleta mwanadamu kwa Mungu)
Sheria inaonyesha (dhihirisha) uovu wa dhambi (mst. 12-13)
Sheria ni takatifu, ya pekee na nzuri, ya kawaida, ni mstari wa kina, amri inatuonyesha wapi na tuko katika upande gani wa Mungu; dhambi inatuonyesha kwa nini "waovu wanaendelea." Mbali sana na alama ya ile ya Mungu aliyetuwekea sisi kwa ajili ya Kristo. Ni kusudi lake kutuhumu wafungwa wa dhambi na njia pekee ni kupitia kwa Kristo pekee kutafuta toba. Ina laana, shutuma, huzuia, na kuongoza kuamsha wakosaji kwa Kristo (3:19, 13; 7:8-11; 8:3; Gal. 3:19-24). Dhambi inaweza kufichwa katika jamii ya watu ikilinganishwa kwa mtu mmoja na mwingine au pia kwa kuhukumiwa tu kwa amri ya moyo wake mwenyewe, lakini katika nuru ya utakatifu kamili, dhambi itakuwa "inazidi sana."
No Comments